Na DEUSDEDEDIT UNDOLE
KLABU ya Simba imesema kiungo wake Mohamed Bajaber yupo fiti kwa asilimia 100 na anaweza kupatikana katika mechi zijazo.
Bajaber raia wa Kenya, alitua Simba msimu huu akitokea Polisi ya nchini humo ambayo ilitwaa ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara msimu uliopita.
Akizungumza Dar es Salaam, Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Simba, Ahmed Ally alisema ni kweli mchezaji Bajeber alikuwa majeruhi kwa takriban miezi miwili tangu alipojiunga na kikosi hicho msimu huu.
Amwesema hivi sasa mchezaji huyo ameimarika kwa asilimia 100, hivyo mpango wa kumhusisha kikosini ni kazi ya benchi la ufundi chini ya Meneja Dimitar Pantev.
“Tunasafiri na winga wetu Bajaber kwenda nchini Mali kwa mechi ya pili ya makundi ya CAFCL dhidi ya timu mwenyeji ya Stade Malien ya nchini humo. Ninawatoa tu hofu mashabiki wa Simba kuhusiana na utimamu wa afya ya winga huyo, kwani wanachopaswa kukijua ni Bajaber yuko ‘fiti’,” amesema.




