• ePaper
Thursday, April 16, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

WAZIRI NANAUKA AWAONYA VIONGOZI WANAOKWAMISHA SHUGHULI ZA VIJANA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
November 29, 2025
in Habari, Kitaifa
0
WAZIRI NANAUKA AWAONYA VIONGOZI WANAOKWAMISHA SHUGHULI ZA VIJANA

WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais, Maendeleo ya Vijana, Joel Nanauka

0
SHARES
7
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na MWANDISHI MAALUMU,
Songea

WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais, Maendeleo ya Vijana, Joel Nanauka, amewaonya watendaji wa serikali wanaokwamisha shughuli za maendeleo ya vijana katika maeneo yao, hawatavumiliwa.

Akizungumza wilayani Songea, Mkoa wa Ruvuma, ambako alikutana na vijana wajasiriamali, wanaofanya shughuli katika Soko la Bombambili na Stendi ya magari ya Ruhuwiko, jana, Nanauka alisema kwamba, Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, ana dhamira ya kweli kuhakikisha vijana wanafanikiwa.

Nanauka ambaye alitumia mikutano yake wilayani humo kukutana na kusikiliza mawazo na ushauri wa vijana ikiwemo kutatua kero zao.

Alisema Rais Dk. Samia, ana dhamira ya dhati kuona vijana wanashiriki kikamilifu ujenzi wa nchi, hivyo aliwasihi waitunze amani na kutumia njia ya mazungumzo, kutatua changamoto ndiyo maana akaunda wizara maalumu inayohusika na vijana.

Aidha, Waziri Nanauka, aliwataka viongozi wa mikoa na wilaya, kuweka utaratibu wa kutoka ofisini na kuwafuata vijana walipo, kusikiliza hoja na kero zinazowakabili.

DC SONGEA

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Songea, Wilhelm Ndile, alisema wamepokea maelekezo ya waziri huyo na kwamba, wataratibu vikao na wajasiriamali vijana na waendesha bodaboda kuzitafutia suluhisho changamoto walizozitoa katika ziara ya Nanauka.

Akizungumza katika kikao na Waziri Nanauka,  Arnold Mgawo, Mkazi wa Bombambili, alisema anapenda kuona Rais Dk. Samia, anadhibiti vitendo vya utekaji na kuimarisha demokrasia hasa vijana kuwa na uhuru wa kuzungumza .

Naye Benedict Tembo, alimshauri Waziri Nanauka, kutowasikiliza watendaji wa serikali wasiochapa kazi, wenye kupotosha ukweli wa changamoto zao, badala yake, achukue hatua dhidi ya wazembe.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu Tawala Mkoa wa Ruvuma, Mary Maganga, mkoa huo una vijana 676,144 kati ya watu 1,848,394. Mary alisema

Previous Post

SERIKALI YAIVALIA NJUGA TANZANITE

Next Post

AHUKUMIWA KUNYONGWA KWA KUTIWA HATIANI KUUA

Next Post
AHUKUMIWA KUNYONGWA KWA KUTIWA HATIANI KUUA

AHUKUMIWA KUNYONGWA KWA KUTIWA HATIANI KUUA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

KAHAWA YA TANZANIA KUONGEZEWA THAMANI KABLA YA KUPELEKWA NJE

KAHAWA YA TANZANIA KUONGEZEWA THAMANI KABLA YA KUPELEKWA NJE

7 months ago
BONDIA MWAKYEMBE AMKUBALI MMALAWI

BONDIA MWAKYEMBE AMKUBALI MMALAWI

4 months ago

Popular News

  • PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SERIKALI YAFUTA LESENI 40 ZA UTAFITI  WA MADINI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TIMU OFISI YA MAKAMU WA RAIS, WIZARA YA MAJI KUCHUANA MEI MOSI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SIMBA, FOUNTAIN GATE SIKU YA HESHIMA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. MWINYI AKAGUA MJI WA AFCON FUMBA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?