• ePaper
Sunday, May 17, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

AHUKUMIWA KUNYONGWA KWA KUTIWA HATIANI KUUA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
November 29, 2025
in Habari, Kitaifa
0
AHUKUMIWA KUNYONGWA KWA KUTIWA HATIANI KUUA
0
SHARES
5
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na REHEMA MOHAMED

MAHAKAMA Kuu Masijala Ndogo ya Dodoma, imemhukumu Augustino Amos, kunyongwa hadi kufa baada ya kutiwa hatiani kwa kosa la mauaji ya Michael Mwimba.

Pia, Mahakama hiyo, imemwachia huru Emmanuel Ngosha na Emmanuel Molla kwa sababu, ushahidi haujatosha kuwatia hatiani.

Hukumu hiyo, ilisomwa mahakamani hapo na Jaji Evaristo Longopa, baada ya kupitia ushahidi wa pande zote mbali.

Washitakiwa hao, walidaiwa kutenda kosa hilo Februari 9, 2023 eneo la Shule ya Masingi Manyoni, Singida.

Ilidaiwa walimjeruhi Mwimba katika jicho la upande wa kushoto na nyuma ya kichwa.

Katika hukumu hiyo, Mahakama ilimtia hatiani Amosi kwa sababu alikiri kutenda kosa kupitia maelezo yake ya ungamo.

Ilielezwa kuwa, kupitia maelezo hayo yaliyoandikwa kwa hiyari yake, mshitakiwa huyo alikiri kutenda kosa hilo.

Ilielezwa kuwa, maelezo ya onyo ya mshtakiwa huyo, yalithibitishwa na ushahidi wa upande wa mashtaka kwamba, kulikuwa na majeraha mawili makubwa katika mwili wa Mwimba, yaani sehemu ya nyuma ya kichwa na upande wa jicho la kushoto.

Katika maelezo hayo, mshitakiwa alikiri kutenda kosa hilo akishirikiana na mtu aliyemtaja kwa jina la Ndutu na Ngosha.

Alieleza walifanya hivyo baada ya kutumwa na mfanyabiashara Molla (mshitakiwa wa tatu), ambaye alikuwa akihitaji damu ya mzee.

Pia, ushahidi wa daktari na ripoti yake iliyopokelewa kama kielelezo namba moja, unaonesha kuwa, Mwimba alipata majeraha hayo ambayo yanalingana na maelezo yaliyomo katika maelezo ya onyo.

Kutokana na hali hiyo, mahakama iliona ushahidi unatosha kuthibitisha kwamba kulikuwa na kifo cha mtu kisicho cha kawaida, hivyo ilimtia hatiani na kumhukumu kunyongwa hadi kufa.

Previous Post

WAZIRI NANAUKA AWAONYA VIONGOZI WANAOKWAMISHA SHUGHULI ZA VIJANA

Next Post

DK. MWIGULU : POLISI WAACHE KUMTAFUTA ASKOFU GWAJIMA

Next Post
DK. MWIGULU : POLISI WAACHE KUMTAFUTA ASKOFU GWAJIMA

DK. MWIGULU : POLISI WAACHE KUMTAFUTA ASKOFU GWAJIMA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

WAZIRI CHONGOLO AELEKEZA MIFUMO TOSCI ISOMANE

WAZIRI CHONGOLO AELEKEZA MIFUMO TOSCI ISOMANE

6 months ago
SIKU 100 ZA RAIS DK. MWINYI IKULU ZANZIBAR

SIKU 100 ZA RAIS DK. MWINYI IKULU ZANZIBAR

3 months ago

Popular News

  • DK. MWIGULU AHIMIZA WANANCHI KUIOMBEA AMANI YA NCHI

    DK. MWIGULU AHIMIZA WANANCHI KUIOMBEA AMANI YA NCHI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. KIKWETE ASHIRIKI MAZISHI YA KITAIFA YA RAIS MSTAAFU MOGAE WA BOTSWANA, AKIMWAKILISHA RAIS DK. SAMIA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DANGOTE AIPONGEZA SERIKALI, AANGAZIA FURSA ZA UWEKEZAJI NCHINI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TANZANIA NI NCHI YA PILI AFRIKA KUWA NA HADHI YA  UTALII WA JIOLOJIA (GEOPARK MUSEUM)

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SERIKALI YAIPONGEZA PUMA ENERGY KWA MFUMO MPYA WA KIDIJITALI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?