• ePaper
Thursday, April 23, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

WASIRA : VIJANA MSIKUBALI KUTUMIKA KUVURUGA AMANI

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
December 2, 2025
in Habari, Kitaifa, Siasa
0
WASIRA : VIJANA MSIKUBALI KUTUMIKA KUVURUGA AMANI

MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Stephen Wasira

0
SHARES
7
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na MWANDISHI WETU

MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Stephen Wasira, amewataka vijana kutokubali kutumika kuvuruga amani na utulivu nchini kwa madai ya kudai haki.

Amesema Tanzania haina uadui na nchi nyingine, lakini yapo baadhi ya mataifa, yanayoumizwa na kasi ya maendeleo iliyopo nchini.

Amesema wanafahamu Tanzania inaelekea kujikomboa kiuchumi, hivyo kuondoka katika kundi la kuomba misaada kutoka kwao.

Wasira alieleza hayo Zanzibar, alipozungumza na vijana, akiwa ziarani visiwani humo.

“Tanzania haina nchi adui, yaani rasmi kusema sisi nchi yetu adui yetu yule pale, Tanzania hatuna, lakini siyo kweli, duniani watu wote wanatupenda, hiyo nayo siyo sahihi.

“Wako wengine wakiona tunafanya maendeleo makubwa wananuna, wapo, wengine wana sababu zao siyo sababu zetu, wasingependa tujitegemee kwa kuwa, tukijitegemea tutaachana na habari ya kwenda kwao kuomba, wangependa wakati wote iwe ‘spoon feed’ yaani tunakaa tunangoja msaada.

“Wakiona Chama kinafanya jitihada za kutuondoa katika kuombaomba, hawapendi. Wakiona Zanzibar imepiga hatua miaka 60 na miaka mitano iliyopita hapa ya awamu ya nane, wanashtuka, wanashangaa hawapendi,” alisema. 

WOSIA KWA VIJANA

Aliwataka vijana wa Tanzania wasikubali kutumika kuivuruga nchi yao, kwa kuwa hakutawaletea maendeleo.

“Wosia wangu kwa vijana mliosoma mliohitimu na wale waliohitimu mapema na ambao hawajaenda vyuo vikuu, hii ni nchi yetu sote, nchi hii haina mtu maalumu ambaye anasema anaimiliki, wamiliki wake ni Watanzania ambao ni milioni 60 na zaidi.

“Kwa hiyo, mkitaka kuwa na maendeleo makubwa, suala la amani ni lazima wala siyo hiyari, maana ukiondoa amani kwa kudanganyika ukidhani unadai haki tutapoteza haki zote, maana utabaki na ipi? Katikati ya vurugu hata haki ya kuishi unapoteza,” alisema.

Previous Post

SERIKALI YAONDOA HOFU UKOSEFU ARV’S

Next Post

RAIS DK. MWINYI ANADI FURSA Z’BAR

Next Post
RAIS DK. MWINYI ANADI FURSA Z’BAR

RAIS DK. MWINYI ANADI FURSA Z’BAR

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

TRA INAVYOIMARISHA USHIRIKIANO NA WAFANYABIASHARA KUKUZA UCHUMI

TRA INAVYOIMARISHA USHIRIKIANO NA WAFANYABIASHARA KUKUZA UCHUMI

4 months ago
 KOCHA SIMBA AITISHA DODOMA JIJI

 KOCHA SIMBA AITISHA DODOMA JIJI

2 weeks ago

Popular News

  • NDEJEMBI ATAJA VIPAUMBELE 10 SEKTA YA NISHATI

    NDEJEMBI ATAJA VIPAUMBELE 10 SEKTA YA NISHATI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MWIGULU ATOA MAAGIZO ALAT

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RIPOTI YA KUPONYA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MWANDAAJI MISS WORLDTZ AITAJA AMANI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SIMBA, MAFUNZO HAPATOSHI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?