• ePaper
Wednesday, April 29, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Burudani

MENEJA PANTEV ATIMULIWA SIMBASC

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
December 3, 2025
in Burudani, Michezo
0
MENEJA PANTEV ATIMULIWA SIMBASC

MENEJA PANTEV

0
SHARES
9
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na MWANDISHI WETU

BODI ya Wakurugenzi ya klabu ya Simba, imefikia makubaliano Meneja Mkuu, Dimitar Pantev kusitisha mkataba wa kuinoa timu hiyo.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa jana na bodi hiyo imeeleza kuwa uamuzi huo umefikiwa na pande zote mbili jana.

Pantev pamoja na wasaidizi wake wawili  wamesitishiwa miakataba yao na hivi sasa kikosi hicho kitakuwa chini ya kocha Seleman Matola.

Hata hivyo, taarifa ya bodi hiyo imeeleza kuwa, mchakato wa kupata kocha mpya unaendelea kufanyika hivi sasa.

Pantev  ni raia wa Bulgaria, ana umri wa miaka 49 alijiunga na Simba kama Kocha Mkuu akichukua nafasi ya Fadlu David aliyeachana na Klabu hio mapema mwezi Oktoba, mwaka huu.

Kama meneja Dimitar Pantev amewahi kuzifundisha timu za Vladislav Varna, Shabla, klabu ya futsal Grand Pro Varna, timu ya Taifa ya futsal ya Bulgaria.

Amewahi kuzinoa timu za Spartak Varna, klabu ya Palestina Alshoban Almuslimin Hebron, Svetkavitsa Targovishte, Victoria United ya nchini Cameroon.

Timu nyingine ni klabu ya Sierra Leone ya Johansen na Orapa United ya nchini Botswana.

Pantev alianza kazi yake ya usimamizi kama mkufunzi wa vijana katika Jiji la Varna. Wakati wa msimu wa 2008-09 alikuwa mkufunzi msaidizi wa Dobrudzha Dobrich.

Pia alifanya kazi kama kocha Mkuu wa Vladislav Varna na Shabla katika  Ligi ya Bulgaria.

Amewahi kushinda mataji matano mfululizo ya Ligi Kuu ya Bulgarian Premiere Futsal, akiiongoza klabu hiyo,pia alisimamia timu ya taifa ya Bulgaria ya futsal mara mbili.

Mnamo Julai 2022, Pantev aliteuliwa kuwa meneja wa Victoria United huko Cameroon.

Mwezi Machi 21, mwaka  2024, Pantev alirudi Victoria United, baadaye aliongoza Victoria kwa  kutwaa taji lao la kwanza la Elite One katika historia ya klabu hiyo.

Januari 23, mwaka huu, Pantev aliteuliwa kama meneja wa Gaborone United, akiongoza timu hiyo kutwaa taji la Ligi Kuu ya Botswana katika msimu wake wa kwanza katika klabu hiyo.

Previous Post

SIMULIZI YA RAIS DK. SAMIA ALIVYOWABEBA WANASIASA NJE 

Next Post

MAGOLI AFUNGUKA SIMBASC

Next Post
MAGOLI AFUNGUKA SIMBASC

MAGOLI AFUNGUKA SIMBASC

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

SPIKA ZUNGU : NITAZINGATIA HAKI, UWAZI

SPIKA ZUNGU : NITAZINGATIA HAKI, UWAZI

6 months ago
OUNAHI TEGEMEO MOROCCO AFCON 2025

OUNAHI TEGEMEO MOROCCO AFCON 2025

4 months ago

Popular News

  • TANZANIA YAJINADI KIMATAIFA MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

    TANZANIA YAJINADI KIMATAIFA MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • VYALENGA KUIJENGA JAMII KIUCHUMI NA KIROHO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • KUVUMILIANA MUHIMU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WAZIRI SANGU ABAINISHA HIFADHI SKIMU INAVYOENDA KUBADILI MAISHA YA WATANZANIA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TUCTA: WAAJILI WATEKELEZE NYONGEZA YA KIMA CHA MISHAHARA SEKTA BINAFSI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?