• ePaper
Thursday, April 16, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Burudani

KETE YA KWANZA MUHIMU KWA MATOLA SIMBA SC

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
December 4, 2025
in Burudani, Habari, Kitaifa, Michezo
0
KETE YA KWANZA MUHIMU KWA MATOLA SIMBA SC

KAIMU Kocha Mkuu wa Simba, Selemani Matola

0
SHARES
6
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na ABDUL DUNIA

KAIMU Kocha Mkuu wa Simba, Selemani Matola, leo atakabiliwa na mtihani wake wa kwanza atakapoiongoza timu hiyo katika mechi ya Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya Mbeya City.

Mtihani huo kwa Matola, unakuja kutokana na rekodi nzuri iliyo nayo Wekundu hao wa Msimbazi waliovuna pointi tisa katika mechi tatu walizocheza, ndiyo timu pekee ambayo haijapata matokeo tofauti na ushindi.

Katika mechi tatu zilizopita, Simba imeshinda dhidi ya Fountain Gate (3-0), Namungo (3-0) na JKT Tanzania (2-1) ambapo Matola anatakiwa kuendeleza moto huo wa ushindi katika ligi hiyo.

 Wapinzani wa Simba, Mbeya City  wenyewe hadi leo, wamefanikiwa kuvuna pointi nane katika mechi tisa ilizocheza katika ligi hiyo yenye ushindani mkubwa.

Mbeya City ilikubali vichapo dhidi ya Mashujaa (1-0), Coastal Union (2-0) na kufungwa 1-0 na timu ya Namungo .

Pambano la Simba na Mbeya City lim epangwa kuanza kufanyika saa 1:00 usiku katika mechi itakayopigwa katika Uwanja wa Meja Jenerali Isamuhyo, Dar es Salaam.

Matola ambaye ataliongoza benchi la ufundi la Simba kwa mara ya kwanza ikiwa ni siku kadhaa tangu alipokaimu mikoba hiyo baada ya klabu hiyo kuachana na aliyekuwa Meneja Mkuu, Dimitar Pantev.

Katika mtanange wa leo, Simba itapaswa kuvuna pointi tatu ili kuendeleza rekodi yake ya ushindi kwa asilimia 100 katika ligi hiyo wakati Mbeya City ikihitaji kupata ushindi wake wa kwanza baada ya kupoteza mechi tatu mfululizo msimu huu.

Akizungumza Dar es Salaam, Matola alisema amekiandaa vyema kikosi chake kuhakikisha kinavuna pointi tatu katika mtanange huo.

“Tumejielekeza zaidi katika ligi, tutahakikisha tunafanya vyema. Ligi ni ngumu na tunaichukulia kwa umuhimu sana mechi ya kesho (leo) na tumejiandaa vizuri kupata ushindi.

Tutatengeneza timu kwa uwiano sasa katika kushambulia na kuzuia, tutaangalia ubora wetu upo wapi kujua tunapataje ushindi,” alisema Matola.

Naye Kocha wa Mbeya City, Patrick Magata alisema licha ya kupata matokeo mabaya katika mechi tatu zilizopita, anaamini watakuwa wapinzani bora kwa Simba katika mtanange wa leo.

“Hatujapata ushindi katika mechi tatu zilizopita, licha ya kutokuwa na muda wa kutosha kujiandaa na mechi , lakini imani yetu ni kwamba tunakwenda kuwania pointi tatu na tunaamini tunaweza kuzipata,” alisema Magata.

Previous Post

KOCHA SERENGETI BOYS AANIKA SIRI KUTWAA UBINGWA CECAFA

Next Post

TANZANIA INAENDELEA KUALIKA WAWEKEZAJI – RAIS DK. SAMIA

Next Post
TANZANIA INAENDELEA KUALIKA WAWEKEZAJI – RAIS DK. SAMIA

TANZANIA INAENDELEA KUALIKA WAWEKEZAJI – RAIS DK. SAMIA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

YANGA YAKUBALI YAISHE

YANGA YAKUBALI YAISHE

2 months ago
KOCHA SIMBA AIPANIA MASHUJAA

KOCHA SIMBA AIPANIA MASHUJAA

3 months ago

Popular News

  • MAFANIKIO YA KISHINDO SGR

    MAFANIKIO YA KISHINDO SGR

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • NYAMBUI AFUNGUKAAMANI KATIKA MICHEZO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • YANGA, MBEYA CITY KAZI IPO LEO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. MWINYI AFICHUA KUWA NA KIPAJI CHA SOKA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?