• ePaper
Thursday, April 16, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Burudani

KOCHA SERENGETI BOYS AANIKA SIRI KUTWAA UBINGWA CECAFA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
December 4, 2025
in Burudani, Habari, Kitaifa, Michezo
0
KOCHA SERENGETI BOYS AANIKA SIRI KUTWAA UBINGWA CECAFA

Serengeti Boys

0
SHARES
3
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na VICTOR MKUMBO

KOCHA wa timu ya taifa ya vijana wenye umri wa chini ya miaka 17 ‘Serengeti Boys’, Elieneza Nsanganzelu ametoboa siri ya kubeba ubingwa wa michuano ya kufuzu fainali za Mataifa ya Afrika (AFCON 2026), Ukanda wa Afrika Mashariki na Kati (CECAFA) ni maandalizi mazuri waliyofanya.

Serengeti Boys, ilitwaa ubingwa wa michuano ya CECAFA kufuatia kuichapa Uganda kwa mabao 3-2, katika fainali iliyofanyika Uwanja wa Abebe nchini Ethiopia.

Akizungumza baada ya kumalizika kwa michuano ya CECAFA, Kocha Nsanganzelu alisema wamefanikiwa kutwaa ubingwa huo baada ya kupata muda mzuri wa kujiandaa.

“Tunashkuru Mungu kwa kutwaa ubingwa wa michuano ya CECAFA msimu huu kwani haikuwa rahisi kutokana na upinzani tuliokutana nao.

“Siri kubwa ya kutwaa ubingwa wa michuano hiyo ni kufanya maandalizi ya kutosha na wachezaji wangu walifuata maelekezo kwa kiasi kikubwa huku kila mmoja akitimiza majukumu yake uwanjani,” alisema kocha huyo.

Nsanganzelu alisema michuano ya CECAFA haikuwa rahisi, lakini walipambana kuhakikisha wanafanya vizuri ikiwemo kufuzu kucheza AFCON na kutwaa ubingwa.

Aliwapongeza wachezaji wake kutokana na kila mmoja kutimiza majukumu yake uwanjani na kwamba ana imani wataendelea kutunza kiwango kuhakikisha wanafikia malengo ya kubeba taji la AFCON 2026.

Pamoja na kutwaa ubingwa, timu hiyo ilibeba tuzo za Kocha Bora (Nsanganzelu), Mfungaji Bora (Luqman Mbalasalu) na Kipa Bora akiwa Haji Ally.

Nahodha wa Serengeti Boys, Kassim Selemani alisema walipambana kupata ushindi katika mechi zote kutokana na maandalizi mazuri waliyoyapata na kufuata maelekezo ya benchi la ufundi.

“Tumepambana kila mmoja kwa nafasi kuhakikisha tunafikia malengo tuliyojiwekea na ubingwa huu siyo wetu wachezaji pekee bali ni kwa ajili ya Watanzania ambao wamekuwa mstari wa mbele kutupa sapoti tangu tunaanza michuano ya msimu huu.

“Tutaendelea kupambana kuhakikisha tunatwaa ubingwa wa AFCON 2026 na kulileta kombe Tanzania,” alisema Selemani.

Katika michuano hiyo, Serengeti Boys iliandika historia kufuatia kushinda mechi zote msimu huu, Serengeti Boys ilianza michuano hiyo kwa kuichapa Sudan mabao 6-0, kabla ya kuirarua Djibouti idadi hiyo hiyo, iliifunga Burundi 5-0 na kutinga hatua ya nusu fainali.

Katika mchezo wa nusu fainali iliibuka na ushindi wa mabao 3-1 mbele ya Kenya kabla ya kuishushia Uganda kipigo cha mabao 3-2 juzi.

Kufuatia matokeo hayo, Serengeti Boys imefuzu kucheza fainali za AFCON 2026 ikifuatana na Uganda na Ethiopia katika Ukanda wa CECAFA.

Previous Post

FOUNTAIN GATE KUITIBULIA YANGA?

Next Post

KETE YA KWANZA MUHIMU KWA MATOLA SIMBA SC

Next Post
KETE YA KWANZA MUHIMU KWA MATOLA SIMBA SC

KETE YA KWANZA MUHIMU KWA MATOLA SIMBA SC

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

KIHONGOSI ATOBOA SIRI UIMARA WA CCM

KIHONGOSI ATOBOA SIRI UIMARA WA CCM

3 months ago
TAASISI ZINAZOFANYA VIBAYA KUANIKWA

TAASISI ZINAZOFANYA VIBAYA KUANIKWA

2 weeks ago

Popular News

  • MAFANIKIO YA KISHINDO SGR

    MAFANIKIO YA KISHINDO SGR

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • NYAMBUI AFUNGUKAAMANI KATIKA MICHEZO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • YANGA, MBEYA CITY KAZI IPO LEO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. MWINYI AFICHUA KUWA NA KIPAJI CHA SOKA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?