• ePaper
Sunday, August 16, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Burudani

MPINZANI WA MWAKINYO HADHARANI

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
December 14, 2025
in Burudani, Michezo
0
MPINZANI WA MWAKINYO HADHARANI

MWAKINYO

0
SHARES
25
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na AMINA KASHEBA

ZIKIWA zimebaki siku 13 kuelekea pambano la ‘Boxing On Boxing Day’ mpinzani wa ngumi za kulipwa, Hassan Mwakinyo ametangazwa ni Stanley Eribo kutoka Nigeria.

Mwakinyo atapanda ulingoni kuzichapa na Eribo, katika pambano la raundi 10, lisilo la ubingwa litakalofanyika Desemba 26, mwaka huu katika Ukumbi wa Warehouse, Dar es Salaam.

Akizungumza na UHURU jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Kampuni ya Peak Time, Meja Selemani Semunyu ambao ndiyo waandaji wa pambano hilo alisema Mwakinyo atatoana jasho na Mnigeria huyo katika mtanange huo.

“Kila kitu kinaendelea vizuri hivi sasa na mabondia wanaendeleza kufanya mazoezi katika gym zao, Watanzania wengi walikuwa wanahitaji kufahamu mpinzani wa Mwakinyo, ambaye tunamtangaza rasmi ni Eribo,” alisema.

Meja Semunyu aliongeza kuwa mwaka huu, kutakuwa na mapambano mengi zaidi kuhakikisha mabondia mbalimbali wanatoa burudani kwa mashabiki wao tofauti na ilivyokuwa awali.

“Kuna mapambano mengi ambayo kila atayekuja hapo atafurahi kwa sababu maandalizi ni mazuri mno, kila kitu kinaendelea kama kilivyopangwa,” alisema.

Kocha wa Mwakinyo, Kanda Kabongo alisema kwao wako tayari na pambano hilo, hivyo bondia wake anaendelea kufanya mazoezi kuhakikisha anamchakaza mpinzani wake katika raundi za awali.

“Bondia wangu yupo fiti na ninaendelea kumpatia mazoezi ya kutosha kuhakikisha anampiga mpinzani katika raundi za awali.

“Tunatambua pambano litakuwa na upinzani mkubwa kutokana na rekodi za mpinzani, hivyo lazima tufanye maandalizi ya kutosha kuhakikisha tunaubakisha ushindi nyumbani.

“Watanzania na mashabiki wajitokeze kwa wingi kuja kupata burudani na kumpa sapoti ya kutosha bondia wao,” alisema.

Baadhi ya mabondia wengine ambao watakaopanda ulingoni siku hiyo ni Hamadi Furahisha akizichapa dhidi ya Mmalawi Hanock Phiri, Ally Ngwando na Mussa Makuka, Issa Simba atapepetana na Wilson Phiri kutoka Malawi, huku kwa upande wa wanawake, Hidaya Zahoro atapanda ulingoni na Leila Macho, Debora Mwenda akirushiana makonde na Mmalawi Mariam Dick.

Previous Post

KAPOMBE AFUNGUKA STARS

Next Post

HERSI ACHOMOZA FIFA

Next Post
HERSI ACHOMOZA FIFA

HERSI ACHOMOZA FIFA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

OMR YANAWIRI KARATA WANAWAKE MEI MOSI

OMR YANAWIRI KARATA WANAWAKE MEI MOSI

4 months ago
MAKONDA ASISITIZA KUTOVUMILIA WAKANDARASI WAZEMBE AFCON

MAKONDA ASISITIZA KUTOVUMILIA WAKANDARASI WAZEMBE AFCON

7 months ago

Popular News

  • KIINI DABI KARIAKOO KUPIGWA ZANZIBAR

    KIINI DABI KARIAKOO KUPIGWA ZANZIBAR

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TAMU, CHUNGU DABI YA K’KOO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. SAMIA AKUTANA NA VIONGOZI WA TEC

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. SAMIA AWAPA RAHA VIGOGO USHIRIKA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • BILIONI 30/- KUJENGA UWANJA WA KISASA SIMBA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Not enough quota to unlock this post
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?