• ePaper
Sunday, June 14, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Burudani

TPLB YAGUSIA WAZO LA FIFA USAWA WA KALENDA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
December 16, 2025
in Burudani, Habari, Kitaifa, Michezo
0
TPLB YAGUSIA WAZO LA FIFA USAWA WA KALENDA

OFISA Habari wa TPLB, Karim Boimanda

0
SHARES
9
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na ABDUL DUNIA

SIKU moja baada ya Rais wa Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA), Gianni Infantino, kusisitiza umuhimu wa usawa katika kalenda za soka duniani kote, Bodi ya Ligi Kuu Tanzania Bara (TPLB), imesema wazo hilo ni muhimu na litakuwa na manufaa makubwa katika soka hapa nchini.

Infantino alitoa maoni hayo katika Kongamano la FIFA kuhusu Uongozi lililofanyika jijini Doha, Qatar juzi na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa soka akiwemo Mwenyekiti wa Chama cha Klabu za Soka Afrika (ACA), Mtanzania Mhandisi Hersi Said.

Rais huyo alisema FIFA na wadau mbalimbali walijadiliana mambo mengi ikiwemo uhitaji wa kutafuta usawa sahihi katika kalenda ya klabu, kuhakikisha timu zinacheza idadi sahihi ya mechi na juu ya yote, mechi zenye maana.

“Kombe la Klabu Bingwa Dunia 2025 (lililofanyika Juni hadi Julai mwaka huu) lilionyesha ni kwa kiasi gani klabu kutoka maeneo yote duniani zinaweza kushiriki katika jukwaa kubwa na kuungana na mashabiki duniani bila ya kuathiri ratiba nyingine,” alisema Infantino.

Pia, Infantino alisema: “FIFA ina jukumu muhimu katika kusaidia soka ngazi ya klabu kukuwa duniani kote kwa kuwa wabunifu na kuunda matukio ambayo yatavuka mipaka na kuzipa klabu majukwaa wanayostahili,”.

Akizungumzia uhitaji wa kutafuta usawa sahihi katika kalenda ya klabu, Ofisa Habari wa TPLB, Karim Boimanda, amesema wazo hilo ni bora na anaamini litakuwa na manufaa makubwa katika soka ikiwemo la Tanzania.

“Wazo hilo ni bora, unapokuwa na kalenda iliyo sawa na sahihi maana yake itatoa fursa kubwa kwa wachezaji kucheza mechi zinazoedana na uwezo wao wa ufiti na kupunguza baadhi ya majeraha tofauti na mechi zinaporundikana.

Pia, itasaidia kufanya ratiba ya michuano fulani katika shirikisho moja kutoingiliana na ratiba nyingine, jambo ambalo litatoa nafasi kubwa ya ushindani na ufanisi katika kushiriki mashindano,” alisema.

Pia, Boimanda alisema kunapokuwa na usawa katika kalenda ya soka kiuhalisia viwango vya wachezaji upanda na hali ya ushindani huongezeka.

Previous Post

TAIFA STARS KUTUA MOROCCO KWA KISHINDO

Next Post

BONDIA MWAKYEMBE AMKUBALI MMALAWI

Next Post
BONDIA MWAKYEMBE AMKUBALI MMALAWI

BONDIA MWAKYEMBE AMKUBALI MMALAWI

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

KIBAIGWA IMEFUNIKA, OKTOBA WANATIKI KWA DK. SAMIA

KIBAIGWA IMEFUNIKA, OKTOBA WANATIKI KWA DK. SAMIA

10 months ago
AZAM KUSAKA MAKALI KUIVAA SIMBA

AZAM KUSAKA MAKALI KUIVAA SIMBA

3 months ago

Popular News

  • RAIS DK. SAMIA ATAKA MIKOPO ISIWE MZIGO

    RAIS DK. SAMIA ATAKA MIKOPO ISIWE MZIGO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • AFRIKA KUCHOCHEA UTUNZAJI MAZINGIRA KUPITIA NISHATI SAFI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MWAKINYO AOMBA RADHI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • YANGA, SIMBA NI KIVINGINE ZAIDI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MEXICO YAANZA KWA KISHINDO WC, KADI ZATEMBEA HATARI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Not enough quota to unlock this post
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?