• ePaper
Friday, June 26, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

TANZANIA, SAUDI ARABIA KUIMARISHA USHIRIKIANO

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
December 25, 2025
in Habari, Kimataifa, Kitaifa
0
TANZANIA, SAUDI ARABIA KUIMARISHA USHIRIKIANO
0
SHARES
11
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na MWANDISHI MAALUMU

SERIKALI ya Saudi Arabia imesema itaendelea kushirikiana na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kuimarisha uhusiano zaidi katika nyanja mbalimbali.

Hayo yalisemwa na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje ya Ufalme wa Saudi Arabia, Waleed bin Abdulkarim El Khereiji, alipopokea ujumbe maalumu kutoka kwa Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, uliowasilishwa kwa Mwanamfalme na Waziri Mkuu wa Saudi Arabia Mtukufu Mohammed bin Salman Al Saud.

Taarifa iliyotumwa kwa vyombo vya habari na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, ilisema ujumbe huo uliwasilishwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mahmoud Thabit Kombo akiambatana na Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo Profesa Palamagamba Kabudi.

Akipokea ujumbe huo,  Waleed alisema Saudi Arabia inatambua na kuthamini uhusiano wa muda mrefu na imara wa muda mrefu wa kidiplomasia, kibiashara na kiutamaduni uliopo kati ya Ufalme wa Saudi Arabia na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Aidha, Waleed aliahidi Ufalme wa Saudi Arabia utaendelea kushirikiana kwa karibu na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wa Tanzania kwa kuimarisha zaidi maeneo ya vijana, utamaduni, biashaa, uwekezaji, utalii, elimu, ajira na maeneo mengine yaliyoafikiwa na nchi hizo mbili.

Vilevile, alieleza dhamira ya Ufalme wa Saudi Arabia kuunga mkono jitihada uwezeshaji wa vijana zilizowekwa na Serikali ya Tanzania na Waziri Kombo.

Previous Post

‘TUMUOMBEE KARDINALI PENGO’

Next Post

GAMONDI MATUMAINI KIBAO, WADAU WAIPA TANO STARS

Next Post
GAMONDI MATUMAINI KIBAO, WADAU WAIPA TANO STARS

GAMONDI MATUMAINI KIBAO, WADAU WAIPA TANO STARS

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

KETE YA KWANZA MUHIMU KWA MATOLA SIMBA SC

KETE YA KWANZA MUHIMU KWA MATOLA SIMBA SC

7 months ago
NCHIMBI : NIDHAMU NGUZO KUIMARISHA DEMOKRASIA

NCHIMBI : NIDHAMU NGUZO KUIMARISHA DEMOKRASIA

9 months ago

Popular News

  • SERIKALI YAZITAKA TAASISI ZOTE KUJIANDAA KUKABILIANA NA ATHARI ZA EL-NINO

    SERIKALI YAZITAKA TAASISI ZOTE KUJIANDAA KUKABILIANA NA ATHARI ZA EL-NINO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SAMAMBA AWAFUNDA WAKAGUZI MADINI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RUNGU ZITO KUWASHUKIA WAWEKEZAJI ‘JANJAJANJA’

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • YANGA, SIMBA KAZI KAZI UBINGWA LIGI KUU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • YANGA, AZAM FC HAIJAISHA HADI IISHE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Not enough quota to unlock this post
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?