• ePaper
Thursday, April 16, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Burudani

FIFA YADHAMIRIA KUWEKA NGUVU TANZANIA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
January 21, 2026
in Burudani, Habari, Michezo
0
FIFA YADHAMIRIA KUWEKA NGUVU TANZANIA
0
SHARES
4
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na MWANDISHI WETU

RAIS wa Shirikisho la Soka Duniani (FIFA), Gianni Infantino, amesema shirikisho hilo lipo tayari kushirikiana na Tanzania katika programu zake za maendeleo kusaidia kutengeneza fursa kwa vijana kunufaika na mpira wa miguu.

Pia, Infantino alisema hatua hiyo itasaidia ujenzi wa miundombinu na uendelezaji wa vituo vya ufundi.

Infantino aliyazungumza hayo jijini Rabat, Morocco, alipokutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda na ujumbe wake.

Rais huyo wa FIFA, aliipongeza Tanzania kwa kazi kubwa iliyofanywa na inayoendelea kufanywa na serikali katika ujenzi wa miundombinu ya michezo kuelekea Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2027 na shirikisho hilo litaunga mkono jitihada hizo.

Kwa upande wake Waziri Makonda alimshukuru Infantino kwa ushirikiano mkubwa anaoutoa kwa Tanzania katika maendeleo ya mpira wa miguu na amemhakikishia kuwa Rais Dk. Samia Suluhu Hassan na serikali anayoiongoza inaunga mkono jitihada hizo na ipo tayari kushirikiana na FIFA.

Aidha, Makonda alimkaribisha Infantino kutembelea Tanzania, huku akisisitiza kuwa Tanzania ipo tayari kuwa mwenyeji wa matukio mbalimbali ya FIFA ikiwemo mashindano mbalimbali, mikutano na ziara za viongozi na wataalamu.

Previous Post

PEDRO RAHA TUPU YANGA

Next Post

MAKOCHA YANGA, SIMBA WAZITAMBIA  AL AHLY, ESPERANCE

Next Post
MAKOCHA YANGA, SIMBA WAZITAMBIA  AL AHLY, ESPERANCE

MAKOCHA YANGA, SIMBA WAZITAMBIA  AL AHLY, ESPERANCE

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

SHULE YA BILIONI 1.23/- YAMKOSHA MWIGULU

SHULE YA BILIONI 1.23/- YAMKOSHA MWIGULU

2 months ago
KAMATI KUU CCM YATEUA, WAMO MAKONDA, LUSINDE

KAMATI KUU CCM YATEUA, WAMO MAKONDA, LUSINDE

3 months ago

Popular News

  • PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SERIKALI YAFUTA LESENI 40 ZA UTAFITI  WA MADINI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TIMU OFISI YA MAKAMU WA RAIS, WIZARA YA MAJI KUCHUANA MEI MOSI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SIMBA, FOUNTAIN GATE SIKU YA HESHIMA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. MWINYI AKAGUA MJI WA AFCON FUMBA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?