• ePaper
Monday, May 25, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

KILIO CHA BANDO CHATUA BUNGENI

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
May 23, 2026
in Habari, Kitaifa
0
KILIO CHA BANDO CHATUA BUNGENI
0
SHARES
3
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na MUSSA YUSUPH, Dodoma

KAMATI ya Kudumu ya Bunge, Viwanda, Biashara, Kilimo na Ufugaji, imeishauri serikali kupitia Wakala wa Vipimo (WMA), kuanza kuhakiki vipimo vinavyotumika katika muda wa maongezi na bando za intaneti.

Pia, imeishauri Wizara ya Viwanda na Biashara na Wizara ya Nishati, kuhakikisha mita zote mpya za umeme zinahakikiwa kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu zilizopo kabla ya kusimikwa kwa watumiaji.

Makamu Mwenyekiti wa kamati hiyo, Mariam Ditopile, aliyasema hayo bungeni jijini hapa jana, alipowasilisha taarifa kuhusu utekelezaji majukumu ya Wizara ya Viwanda na Biashara (Fungu 44) kwa Mwaka wa Fedha 2025/2026  na maoni ya kamati kuhusu makadirio ya mapato na matumizi mwaka wa fedha 2026/2027.

Ditopile alisema kumekuwepo na malalamiko ya wananchi, kuhusu thamani halisi za matumizi ya huduma za muda wa maongezi na bando za intaneti.

“Kamati inaishauri wizara kupitia WMA kuanza jukumu la kuhakiki vipimo vinavyotumika kwenye muda wa maongezi na bando za intaneti, ili wananchi waweze kupata thamani halisi ya huduma wanazolipia,” alisema.

AGIZO MITA ZA UMEME

Ditopile ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Kondoa Mjini (CCM), alisema kuna mwitikio hafifu kutoka kwa baadhi ya wazabuni wanaouza mita za nishati ya umeme katika kutekeleza takwa la kisheria la kuhakiki mita hizo WMA kabla ya kuwasilishwa katika ununuzi.

Makamu mwenyekiti huyo alisema hali hiyo inaathiri usahihi wa ankara, kuibua malalamiko ya walaji na kudhoofisha uadilifu wa mifumo ya mapato.

“Kamati inaishauri Wizara ya Viwanda na Biashara kushirikiana na Wizara ya Nishati, kuhakikisha mita zote mpya za umeme zinawasilishwa ili kuhakikiwa kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu zilizopo kabla ya kusimikwa kwa watumiaji,” alieleza.

CHANGAMOTO YA LUMBESA
Kwa mujibu wa Ditopile, changamoto ya lumbesa haijapata suluhu ya kudumu, jambo linalosababisha baadhi ya wafanyabiashara wasio waaminifu kuendelea kutumia mfumo huo kuwanyonya wakulima na kuikosesha serikali mapato.

Alisema kamati inaishauri serikali kushirikisha mamlaka zote zinazohusika na vipimo, ili kupata suluhu ya kudumu kwa kuwa usimamizi wa pamoja utasaidia kubaini chanzo cha tatizo na kuweka mkakati madhubuti ya kulidhibiti.

MAONI YA WABUNGE
Akichangia mjadala, Mbunge wa Gairo (CCM) Ahmed Shabiby, alisema vipo baadhi ya viwanda vya kigeni vinazalisha nondo zenye vipimo ambavyo siyo sahihi.

Alisema badala ya wahusika wenye viwanda kukamatwa, lakini wamiliki wa maduka wamekuwa wakikamatwa na kutozwa faini, hivyo kuwarudisha nyuma wafanyabiashara.

“Tuwaangalie wenye viwanda, siyo mnawapiga faini, vifungwe. Vipo viwanda vinavyozalisha nondo feki. Vipo viwanda vya juisi vinaweka picha ya embe lakini ndani ni kemikali. Mgonjwa anapelekewa juisi ya embe lakini kumbe ni kemikali. Hili tuliangalie,” alisisitiza mbunge huyo.

Mbunge wa Buchosa (CCM) Erick Shigongo, alitilia mkazo suala la uwepo wageni wanaofanya biashara zinazowezwa kufanywa na wazawa.

Alisema wizara ihakikishe wageni hawafanyi biashara ambazo zinazoweza kufanywa na wazawa, kwa kuwa wapo baadhi yao ambao wamekuwa wakiwarudisha nyuma wazawa kwa kuuza bidhaa kwa bei ya chini.

Mbunge kutoka Baraza la Wawakilishi, Simai Mohammed Said, alisema katika mkakati wa kupunguza umaskini Zanzibar imechagua maeneo matatu ambayo ni biashara, huduma na utalii.

Mbunge huyo alisema ni muhimu wizara hiyo ikajikita katika maeneo mengine kama ya kilimo na utalii ili kukuza biashara.

Previous Post

ZIARA YA KIHONGOSI YAACHA NEEMA KWA WANAWAKE MARA

Next Post

WAZIRI MKUU AVITAKA VYOMBO VYA ULINZI NA USALAMA KUWA MACHO DHIDI YA WAVUNJA AMANI

Next Post
WAZIRI MKUU AVITAKA VYOMBO VYA ULINZI NA USALAMA KUWA MACHO DHIDI YA WAVUNJA AMANI

WAZIRI MKUU AVITAKA VYOMBO VYA ULINZI NA USALAMA KUWA MACHO DHIDI YA WAVUNJA AMANI

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

DK. SAMIA AMELETA MIRADI MIKUBWA LINDI – MAJALIWA

DK. SAMIA AMELETA MIRADI MIKUBWA LINDI – MAJALIWA

9 months ago
RAIS DK. SAMIA KUNG’ARA AU

RAIS DK. SAMIA KUNG’ARA AU

3 months ago

Popular News

  • WAZIRI MKUU AHIMIZA MALEZI YA KIMAADILI NA USHIRIKIANO WA KIJAMII

    WAZIRI MKUU AHIMIZA MALEZI YA KIMAADILI NA USHIRIKIANO WA KIJAMII

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WAZIRI MKUU AVITAKA VYOMBO VYA ULINZI NA USALAMA KUWA MACHO DHIDI YA WAVUNJA AMANI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • KILIO CHA BANDO CHATUA BUNGENI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • ZIARA YA KIHONGOSI YAACHA NEEMA KWA WANAWAKE MARA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TANZANIA YAJIPANGA KUDHIBITI MIJI HOLELA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?