• ePaper
Thursday, April 16, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

CCM YAOMBOLEZA KIFO CHA KARDINALI PENGO

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
February 20, 2026
in Habari, Kitaifa
0
CCM YAOMBOLEZA KIFO CHA KARDINALI PENGO
0
SHARES
10
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na MWANDISHI WETU

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimepokea kwa huzuni na masikitiko makubwa taarifa ya kifo cha Baba Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo, Askofu Mkuu Mstaafu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, kilichotokea Februari 19, 2026 jijini Dar es Salaam.

Kupitia salamu zake za rambirambi, CCM kimeeleza kuwa kinatambua na kuthamini mchango mkubwa wa kiongozi huyo wa kiroho katika kulihudumia Kanisa Katoliki na Taifa la Tanzania kwa ujumla.

Chama hicho kimesisitiza kuwa katika kipindi chote cha utumishi wake, Kadinali Pengo alijitokeza kama kiongozi mwenye busara, maadili mema na moyo wa kujitoa kwa ustawi wa jamii.

Katika miaka 55 ya upadre, miaka 43 ya uaskofu na miaka 28 ya hadhi ya Ukadinali, marehemu aliweka alama ya uongozi uliotawaliwa na unyenyekevu, mshikamano wa kijamii na kuhimiza amani na maadili mema katika jamii.

CCM kimeeleza kuwa katika kipindi hiki cha maombolezo, kinaungana na Kanisa Katoliki Tanzania, familia ya marehemu, waumini pamoja na Watanzania wote kuomboleza msiba huo mkubwa wa kuondokewa na kiongozi mahiri wa kiroho.

Chama hicho kimetoa pole kwa wote walioguswa na msiba huo na kuwataka Watanzania kuendeleza misingi ya maadili, upendo na mshikamano aliyoyaenzi marehemu wakati wa uhai wake.

Previous Post

RAIS DK. SAMIA AMLILIA KARDINALI PENGO

Next Post

RAIS DK. SAMIA AFICHUA SIRI TANZANIA KUNG’ARA AU

Next Post
RAIS DK. SAMIA AFICHUA SIRI TANZANIA KUNG’ARA AU

RAIS DK. SAMIA AFICHUA SIRI TANZANIA KUNG’ARA AU

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

USHIRIKIANO WA CHINA NA AFRIKA KATIKA UJENZI WA RELI YA TAZARA

USHIRIKIANO WA CHINA NA AFRIKA KATIKA UJENZI WA RELI YA TAZARA

1 week ago
KIBANO WALIOHARIBU SARUJI MIFUKO 1,262

KIBANO WALIOHARIBU SARUJI MIFUKO 1,262

2 months ago

Popular News

  • PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SERIKALI YAFUTA LESENI 40 ZA UTAFITI  WA MADINI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TIMU OFISI YA MAKAMU WA RAIS, WIZARA YA MAJI KUCHUANA MEI MOSI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SIMBA, FOUNTAIN GATE SIKU YA HESHIMA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. MWINYI AKAGUA MJI WA AFCON FUMBA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?