• ePaper
Sunday, May 10, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

RAIS DK. SAMIA AMLILIA KARDINALI PENGO

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
February 20, 2026
in Habari, Kimataifa, Kitaifa
0
RAIS DK. SAMIA AMLILIA KARDINALI PENGO
0
SHARES
15
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na MWANDISHI WETU

RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan amepokea kwa masikitiko taarifa za kifo cha Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo, Askofu Mkuu Mstaafu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, kilichotokea usiku wa tarehe 19 Februari, 2026, katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) jijini Dar es Salaam.

Taarifa kutoka Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu imesema “Rais Dk. Samia anamkumbuka Kardinali Pengo kama kiongozi wa kiroho na mzalendo aliyetoa mchango mkubwa katika kuimarisha imani, maadili, umoja na mshikamano wa kitaifa, kupitia uongozi wake wa muda mrefu ndani ya Kanisa Katoliki.

Ameongeza kuwa, Taifa limepoteza kiongozi aliyelitumikia kwa uadilifu na kujitolea, na kwamba mchango wake katika malezi ya kiroho na maadili utaendelea kukumbukwa, kuthaminiwa na kuenziwa.

Rais Dk. Samia ametuma salamu za rambirambi kwa Mhashamu Jude Thaddaeus Ruwa’ichi, OFMCap – Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam; Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), viongozi wa dini, pamoja na waumini wote walioguswa na msiba huu mzito.

Aidha, Rais Dk. Samia ameungana na Kanisa, waumini na Watanzania wote kwa ujumla katika kipindi hiki cha majonzi, na anamuomba Mwenyezi Mungu aipumzishe roho ya Marehemu mahali pema peponi, Amina.

Previous Post

CARDINAL PENGO AFARIKI DUNIA

Next Post

CCM YAOMBOLEZA KIFO CHA KARDINALI PENGO

Next Post
CCM YAOMBOLEZA KIFO CHA KARDINALI PENGO

CCM YAOMBOLEZA KIFO CHA KARDINALI PENGO

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

DK. MWIGULU AONGOZA KIKAO CHA KAMATI YA KITAIFA YA AFCON 2027

DK. MWIGULU AONGOZA KIKAO CHA KAMATI YA KITAIFA YA AFCON 2027

3 months ago
TANZANIA, SAUDI ARABIA KUIMARISHA USHIRIKIANO

TANZANIA, SAUDI ARABIA KUIMARISHA USHIRIKIANO

5 months ago

Popular News

  • MTIHANI MZITO KWA MOALIN

    MTIHANI MZITO KWA MOALIN

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MWIGULU ATAJA MWAROBAINI MAFURIKO DARAJA LA DUMILA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. SAMIA ATIA NENO BEI MAFUTA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • YANGA MBELE KWA MBELE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WATAALAMU WAFUNGUKA MITAZAMO YA MIKATABA 8

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?