Na ABDUL DUNIA, ZANZIBAR
MENEJA wa Habari wa Simba, Ahmed Ally, amesema nyota wa timu hiyo, Libasse Gueye ni moto wa kuotea mbali kwa mabeki wa timu za Ligi Kuu Tanzania Bara.
Ahmed alitoa kauli hiyo juzi baada ya Simba kutoka suluhu dhidi ya Yanga katika mchezo wa mzunguko wa kwanza wa ligi hiyo uliopigwa Uwanja wa New Amaan Complex, Unguja.
“ Libase ni mwiba kwa mabeki wa timu mbalimbali, Gueye ni kipimo sahihi cha umri wa wachezaji, hakabiki ni mwiba kweli kweli. Hakuna anayeweza kukataa hilo,” alisema.
Kuhusu suluhu, Ahmed alisema timu yake haikustahili kupata matokeo hayo zaidi ya ushindi kwani ilikuwa katika kiwango cha juu kuliko Yanga.
“Najua hata wao wanajua, tulistahili kupata ushindi na sio sare. Hata wasipokiri hadharani lakini mioyoni mwao wanakiri kwamba tulikuwa na kiwango gani leo,” alisema.




