• ePaper
Sunday, May 31, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Burudani

GAMONDI AITOLEA MACHO MACAU

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
March 29, 2026
in Burudani, Habari, Kitaifa, Michezo
0
GAMONDI AITOLEA MACHO MACAU
0
SHARES
4
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na NASRA KITANA

WAKATI ikijiandaa kuikabili Macau, Kocha wa Taifa Stars, Miguel Gamondi amesema amejipanga vyema kuhakikisha wanaibuka na ushindi katika mchezo huo.

Stars leo itashuka dimbani kumenyana na Macau katika mchezo wa pili wa michuano ya FIFA Series 2026 utakaochezwa katika Uwanja wa Pele, Kigali nchini Rwanda.

Timu hiyo ilikubali kichapo cha bao 1-0 katika mchezo wa kwanza dhidi ya Liechtenstein uliochezwa uwanja huo huo.

Akizungumza kuelekea mchezo huo, Gamondi alisema kuwa amejipanga vyema ikiwemo kuongea na wachezaji wake ili kuwajenga kisaikolojia, kuhakikisha wanaibuka na ushindi katika mchezo huo.

Alisema kuwa kila mchezaji anajua majukumu yake, hivyo ana imani kuwa watapambana mwanzo hadi mwisho ili kuweza kushinda mchezo huo muhimu.

“Japokuwa hatukuwa na muda mwingi wa kufanya maandalizi lakini, nimekaa na wachezaji wangu nimewajenga kiakili na kisaikolojia ili tuweze kufanya vizuri na kupata ushindi,” alisema Gamondi.

Kocha huyo alisema kuwa anajua hautakuwa mchezo rahisi, lakini amefanyia marekebisho mapungufu yaliyojitokeza katika mechi ya kwanza ili kuweza kushinda mchezo huo.

Naye kipa wa timu hiyo, Aishi Manula alisema kuwa walipoteza mchezo wa kwanza lakini watapambana ili kupata ushindi katika mchezo unaofuata.

Alisema kuwa ni aibu kubwa endapo watapoteza tena katika mchezo dhidi ya Macau, hivyo wachezaji wote wamekuwa wakihamasishana mazoezini kuhakikisha wanapata ushindi.

“Sisi wachezaji tumejiandaa vizuri kuhakikisha tunapambana kwa kila hali ili kupata ushindi katika mchezo huo muhimu, tulishapoteza mchezo wa kwanza lakini benchi la ufundi limefanyia kazi makosa kuhakikisha tunawapa raha Watanzania,” alisema Manula.

Manula alisema kuwa wanawaahidi Watanzania kwa ujumla kuwa watapambana kuhakikisha wanashinda mchezo huo muhimu.

Ofisa Habari wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Cliford Ndimbo alisema kuwa wachezaji wote wapo vizuri na wana morari ya kutosha kuelekea katika mchezo huo.

“Tulipoteza mchezo wa kwanza lakini hatutakubali kupoteza mchezo wetu wa pili, tunawaomba Watanzania waendelee kuipa sapoti timu yao ili izidi kufanya vizuri zaidi,” alisema Ndimbo.

Hii ni mara ya pili Stars kushiriki michuano hiyo ambayo imekuwa ikisimamiwa na Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA).

Previous Post

SIFA KEMKEMU ZA LUKUVI

Next Post

SIMBA YATAKA KULIPA KISASI AZAM

Next Post
SIMBA YATAKA KULIPA KISASI AZAM

SIMBA YATAKA KULIPA KISASI AZAM

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

WIZARA YA VIWANDA YAZALISHA AJIRA LUKUKI

WIZARA YA VIWANDA YAZALISHA AJIRA LUKUKI

2 months ago
AMANI NGUZO KUU YA USTAWI – RAIS DK. SAMIA

AMANI NGUZO KUU YA USTAWI – RAIS DK. SAMIA

6 months ago

Popular News

  • SERENGETI BOYS KILA KONA, RAIS SAMIA AWAPA MILIONI 500/-

    SERENGETI BOYS KILA KONA, RAIS SAMIA AWAPA MILIONI 500/-

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAS: UTUNZAJI MAZINGIRA AJENDA YA KIPAUMBELE KWA MKOA WA MWANZA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • UPELE UMEPATA MKUNAJI STARS

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • ‎ RAIS DK. SAMIA: POLISI MSIDHARAU TAARIFA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. MWIGULU ATETA NA WAZIRI MKUU WA CONGO BRAZZAVILLE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?