• ePaper
Thursday, April 16, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

RAIS DK. SAMIA ASISITIZA UWEKEZAJI WA KIMKAKATI

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
March 30, 2026
in Habari, Kitaifa
0
RAIS DK. SAMIA ASISITIZA UWEKEZAJI WA KIMKAKATI
0
SHARES
8
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na MWANDISHI MAALUMU

RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan amesisitiza dhamira ya Tanzania ni kuendeleza uwekezaji wa kimkakati unaoendana na vipaumbele vya taifa.

Alisema hayo alipozungumza na Balozi wa Italia nchini, Giuseppe Sean Coppola, aliyemtembelea Ikulu, jijini Dar es Salaam, ambaye aliambatana na ujumbe kutoka Kampuni ya Danieli Group inayoongoza duniani katika teknolojia na uhandisi wa uzalishaji wa chuma.

Kampuni hiyo imeonesha nia ya kuchunguza uwezekano wa kuwekeza katika sekta ya chuma nchini kwa kujenga kiwanda cha kisasa na kikubwa cha chuma mkoani Mtwara, kwa kushirikiana na mwekezaji mzawa.

Ushirikiano huo unatokana na majadiliano ya awali yaliyofanyika wakati wa Jukwaa la Biashara na Uwekezaji kati ya Tanzania na Italia, pamoja na mashauriano ya kitaalamu na taasisi za Tanzania, ikiwemo Mamlaka ya Maeneo Maalumu ya Uwekezaji Tanzania (TISEZA) na wizara husika.

Mradi unaopendekezwa, ambao bado uko katika hatua ya awali ya uchambuzi, unakadiriwa kugharimu takribani Euro bilioni 1.5 (sawa na sh. trilioni 4.2 za Kitanzania), unatarajiwa kutekelezwa kwa awamu kulingana na tathmini zaidi na taratibu za uwekezaji.

Rais Dk. Samia aliueleza ujumbe huo, Tanzania inaendelea kujijenga kama kituo shindani na cha kuaminika kwa uwekezaji, ikitegemea rasilimali zake asilia, nafasi yake ya kimkakati, pamoja na mageuzi yanayoendelea kuboresha mazingira ya biashara.

 “Tunakaribisha ushirikiano unaoongeza thamani ya rasilimali zetu, unaozalisha ajira kwa wananchi wetu na kuchangia dira yetu ya muda mrefu ya kujenga uchumi wa viwanda,”alisema.

Rais Dk. Samia alimhakikishia Balozi Coppola na ujumbe wake, serikali itaendelea kuwa wazi kwa wawekezaji wenye sifa, wanaoleta siyo mtaji pekee, bali pia teknolojia, ujuzi na dhamira ya muda mrefu katika maendeleo ya Tanzania.

BALOZI COPPOLA

Kwa upande wake, Balozi wa Italia nchini, Coppola alisema ushirikiano huo unaakisi kuimarika uhusiano wa kiuchumi kati ya Tanzania na Italia chini ya mifumo mipana ya ushirikiano wa maendeleo.

“Nia iliyooneshwa na Danieli Group ni sehemu ya juhudi pana za kuimarisha ushirikiano kati ya nchi zetu mbili, ikiwemo kupitia Mpango wa Mattei kwa Afrika.

“Mpango huu unalenga kukuza uwekezaji endelevu na wenye manufaa kwa pande zote, Tanzania inaonekana mshirika muhimu katika muktadha huu.

“Kwa sasa, tupo katika hatua ya kuangalia uwezekano na tunatarajia kuendelea kushirikiana kwa karibu na serikali ya Tanzania kadri majadiliano yatakavyoendelea,” alisema.

DANIELI GROUP

Naye, Mtendaji Mkuu wa Danieli Group, Giacomo Danieli, alieleza sababu za kimkakati zilizoifanya kampuni hiyo kuvutiwa na Tanzania.

“Tunaona fursa kubwa nchini Tanzania, siyo tu kutokana na uwepo wa rasilimali kama gesi na madini ya chuma, bali pia kutokana na ukuaji wa soko na nafasi yake ya kimkakati katika ukanda huu.

 “Mtazamo wetu unalenga ushirikiano wa muda mrefu kuleta teknolojia ya kisasa inayozingatia mazingira, huku tukishirikiana na wadau wa ndani kukuza ujuzi na kujenga uwezo endelevu wa viwanda.

“Hii ni hatua ya awali, tumejipanga kuendelea na majadiliano ya kitaalamu kutathmini uwezekano wa mradi huu,” alisema Danieli.

Iwapo utatekelezwa, uwekezaji huo utachangia kwa kiasi kikubwa katika ajenda ya Tanzania ya kujenga uchumi wa viwanda chini ya Dira ya Taifa ya 2050, kwa kuimarisha uzalishaji wa ndani wa chuma, kupunguza uagizaji kutoka nje, kuongeza thamani ya rasilimali za ndani na kutengeneza ajira kwa vijana.

Aidha, unaweza kuimarisha nafasi ya Tanzania kama kitovu cha uzalishaji wa chuma katika ukanda huu, hususan kwa nchi jirani zisizo na bandari, pamoja na kusaidia maendeleo ya miundombinu na usafirishaji katika ukanda wa Mtwara.

Kikao hicho kilionesha kuendelea kuimarika mvuto wa Tanzania kama kituo cha uwekezaji na dhamira ya pamoja ya pande zote mbili kuendelea kuchunguza fursa zitakazozalisha thamani endelevu ya kiuchumi na ukuaji shirikishi.

Previous Post

WAZIRI MKUU : COCO BEACH HAIUZWI, NI YA WANANCHI

Next Post

WANASIASA WAELEZA IMANI YAO TUME YA JAJI CHANDE

Next Post
WANASIASA WAELEZA IMANI YAO TUME YA JAJI CHANDE

WANASIASA WAELEZA IMANI YAO TUME YA JAJI CHANDE

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

MOROCCO ATOA TANO KOMBE LA MAPINDUZI

MOROCCO ATOA TANO KOMBE LA MAPINDUZI

4 months ago
RAIS MSTAAFU MALAWI AWAUSIA WATAZANIA

RAIS MSTAAFU MALAWI AWAUSIA WATAZANIA

4 days ago

Popular News

  • PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SERIKALI YAFUTA LESENI 40 ZA UTAFITI  WA MADINI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TIMU OFISI YA MAKAMU WA RAIS, WIZARA YA MAJI KUCHUANA MEI MOSI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SIMBA, FOUNTAIN GATE SIKU YA HESHIMA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. MWINYI AKAGUA MJI WA AFCON FUMBA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?