• ePaper
Thursday, April 16, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

WADAU WAFICHUA AMANI INAVYOVUTIA WAWEKEZAJI

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
April 1, 2026
in Habari, Kitaifa
0
WADAU WAFICHUA AMANI INAVYOVUTIA WAWEKEZAJI
0
SHARES
16
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na ZIANA BAKARI

WADAU wakiwemo wasomi wa uchumi nchini, wamesema kuna uhusiano mkubwa kati ya uwekezaji na amani ambayo huvutia wawekezaji wa kigeni popote duniani.

Pia, wamewasihi Watanzania kuendelea kulinda amani ya nchi ambayo ni tunu ya taifa inayopaswa kupewa kipaumbele, huku wakishauriwa kutokubali kushawishiwa na mtu yeyote kuvuruga amani iliyopo.

Wakizungumza UHURU, baadhi ya wadau hao walisema wawekezaji wengi huvutiwa kuwekeza katika nchi yenye amani.

PROFESA WANGWE

Mtaalamu wa uchumi, Profesa Samuel Wangwe, alisema kuna uhusiano mkubwa kati ya uwekezaji na masuala ya amani, kwa sababu asilimia kubwa huvutiwa kuweka mitaji yao katika sehemu zilizo salama.

Alisema siku zote wawekezaji wanapenda sehemu yenye amani na hawawezi kwenda mahali penye vurugu.

“Wawekezaji wanapenda nchi yenye amani, kama kuna vurugu watakwenda nchi nyingine ambayo ina amani, hivyo kuna uhusiano mkubwa kati ya uwekezaji na amani ndani ya nchi,”alisema Profesa Wangwe.

Alifafanua nchi yoyote haiwezi kupata maendeleo bila kuwepo amani inayoambatana na utawala bora ambazo ni nguzo muhimu katika kuhakikisha mazingira ya uwekezaji yanafanikiwa na kuleta tija kwa taifa.

Kwa mujibu wa Profesa Wangwe, uwekezaji unahitaji mazingira ya utulivu kuweza kunufaisha taifa.

“Uwekezaji ni nyenzo muhimu ya maendeleo ya kiuchumi, lakini uwekezaji uweze kuvutia na kukua, lazima kuwa na amani, siku zote machafuko, migogoro au kutokuwepo usalama kunaweza kuzuia wawekezaji kutoka nje na hata kukwamisha wazawa kufanya biashara zao kwa uhuru,” aliongeza.

Alieleza mtu anapotaka kuwekeza hatopenda uwekezaji wake uingie katika dosari sababu ya vurugu, hivyo lazima atakwenda sehemu yenye amani.

Akitaja athari za kutokuwepo amani, Profesa Wangwe alisema ni kupungua uwekezaji nchini, maendeleo yatapungua na hata wananchi watakwama kuendelea na shughuli za kujipatia kipato.

“Amani inapokosekana ndani ya nchi hata ukuaji wa uchumi utashuka na maendeleo yoyote hayawezi kupatikana bila ya uwepo wa amani na tujue tu tutaweza kukosa wawekezaji kwa sababu nchi itakuwa haina amani.

“Tunapaswa kufahamu amani ni jambo muhimu sana ndani ya nchi kwa sababu, maendeleo yote yanahitaji uwepo wa amani kuvutia wawekezaji nchini,” alisema.

NINI CHA KUFANYA

Profesa Wangwe aliwashauri Watanzania kuendelea kudumisha amani, kwani ndiyo nguzo muhimu ya maendeleo.

“Amani ni moja ya hazina kubwa tuliyonayo, tuendelee kudumisha amani na umoja wetu na mshikamano, hii itasaidia maendeleo kuzidi kuonekana.

“Siku zote uwepo wa amani ni jambo ambalo linavutia wawekezaji kuja kuwekeza nchini na linachochea maendeleo ya kiuchumi, hivyo niwaombe sana kulinda tunu yetu ya amani na serikali isichoke kuendelea kusikiliza changamoto za wananchi,” alisema Profesa Wangwe.

MHADHIRI WA OUT

Katika hatua nyingine, Mhadhiri wa Uchumi Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT), Dk. Timothy Lyanga, alisema mwekezaji siku zote anapotaka kuwekeza sehemu anachoangalia ni utulivu na amani katika nchi.

Alisema mwekezaji hawezi kuwekeza sehemu ambayo haina amani kwa sababu anachoangalia ni uhakika wa usalama wa mali zake, wafanyakazi na mazingira ya biashara.

Katika mazingira ya amani, Dk. Lyanga alisema hakuna mwekezaji aliye tayari kuweka mtaji wake katika mazingira ya wasiwasi sababu ya migogoro.

Alibainisha athari za kutokuwepo amani ni chanzo cha shughuli za kiuchumi na kijamii kushindwa kufanyika vizuri.

“Niwashauri Watanzania wenzangu tuendelee kuitunza amani yetu, kwani maendeleo yoyote yanahitaji amani, tuthamini nchi yetu na kuipenda,”alisema Dk. Lyanga.

AMANI, UWEKEZAJI

Akizungumzia uhusiano uliopo baina ya uwekezaji na amani, Mhandiri Mwandamizi wa OUT, Dk. Mohammed Maguo, alisema kuna uhusiano mkubwa baina ya vitu hivyo viwili.

Alisema kama hakuna amani hata uwekezaji hauwezi kufanyika ndani ya nchi, hivyo aliwahimiza Watanzania kutunza amani kuvutia wawekezaji zaidi.

TUSIDANGANYIKE KABISA

Kwa upande wake, Mhadhiri Mwandamizi wa Uchumi na Uongozi kutoka Chuo cha Mwalimu Nyerere, Dk. Philip Daninga, alisema wawekezaji huvutiwa zaidi kuwekeza sehemu yenye utulivu na uongozi mzuri.

“Tuendelee kudumisha amani yetu na tusidanganyike na mtu yeyote kuvuruga amani iliyopo, tusichoke kufundisha vizazi vyetu umuhimu wa amani ndani ya nchi,”alisisitiza Dk. Daninga.

WANANCHI WAHIMIZWA

Naye, Mhadhiri wa Idara ya Hisabati wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Dk. Sylvester Rugeihyamu, alisema hakuna mwekezaji atakayekubali kuwekeza sehemu isiyokuwa na amani hivyo, aliwahimiza wananchi kulinda amani kwani, tatizo dogo likitokea linaweza kuharibu kitu kikubwa.

“Tujifunze yaliyotokea kipindi cha nyuma, tuwe tayari kubadilika na kuilinda nchi yetu ibaki kuwa ya amani izidi kuwavutia wawekezaji kuja kuwekeza,” alisisitiza Dk. Rugeihyamu.

Previous Post

MWENEZI KIHONGOSI NA MSISITIZO WA MAENDELEO, SIYO VURUGU

Next Post

RAIS DK. SAMIA ATETA NA WAGOMBEA URAIS 2025

Next Post
RAIS DK. SAMIA ATETA NA WAGOMBEA URAIS 2025

RAIS DK. SAMIA ATETA NA WAGOMBEA URAIS 2025

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

UPATIKANAJI MAJI DAR SASA KWA USAWA

UPATIKANAJI MAJI DAR SASA KWA USAWA

4 months ago
MAJIJI SITA MOROCCO KUIPAMBA AFCON

MAJIJI SITA MOROCCO KUIPAMBA AFCON

4 months ago

Popular News

  • PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SERIKALI YAFUTA LESENI 40 ZA UTAFITI  WA MADINI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TIMU OFISI YA MAKAMU WA RAIS, WIZARA YA MAJI KUCHUANA MEI MOSI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SIMBA, FOUNTAIN GATE SIKU YA HESHIMA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. MWINYI AKAGUA MJI WA AFCON FUMBA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?