• ePaper
Thursday, April 9, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

POLISI WATIA MGUU SAKATA LA NYETI ZA WANAUME

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
April 6, 2026
in Habari, Kitaifa
0
POLISI WATIA MGUU SAKATA LA NYETI ZA WANAUME
0
SHARES
7
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na MWANDISHI WETU

JESHI la Polisi nchini, limetoa onyo kali dhidi ya wanaoendekeza upotoshaji na uzushi  wa nyeti za wanaume kutoweka na kuusambaza katika mitandao ya kijamii, ambao umeshasababisha madhara makubwa kwa watu na familia zao.

Limeelekeza kwa yeyote anayejirekodi, anayetengeneza vichekesho kwa kutumia uzushi huo na wanaosambaza nao wasakwe, wakamatwe kwa hatua za kisheria.

Onyo hilo lilitolewa mwishoni mwa wiki kupitia taarifa iliyotolewa na Msemaji wa Jeshi la Polisi nchini, David Misime.

Kwa mujibu wa Misime, imani hizo potofu za uzushi na za kusingizia watu wengine mpaka hivi sasa zimesababisha vifo vya watu saba ndani ya siku nne na wengine majeruhi wakiendelea na matibabu hospitalini. 

“Jeshi la Polisi linatoa onyo kali dhidi ya wanaoendekeza upotoshaji na uzushi huo na kuusambaza katika  mitandao ya kijamii na matokeo yake umeshasababisha madhara makubwa kwa watu na familia zao.

“Maelekezo ya ziada yanatolewa kwa yeyote anayejirekodi, anayetengeneza vichekesho kwa kutumia uzushi huo na wanaosambaza nao wasakwe wakamatwe kwa hatua za kisheria kwa mujibu wa sheria ya Makosa ya Mtandaoni na Sheria zingine za nchi,” aliagiza Misime.

Juzi, jeshi hilo lilitoa taarifa ya kukemea tabia potofu iliyozuka hivi karibuni ya kusingizia watu kuwa, wamemgusa mtu fulani begani na matokeo yake aliyeguswa sehemu zake za siri zimetoweka.

Misime alisema tabia hiyo ya uzushi na inayosukumwa na imani za kishirikina, mihemko ya kishabiki na nia ovu ilianzia  Tunduma, mkoani Songwe, Aprili Mosi, mwaka huu, kisha jijini Mbeya na Dar es Salaam.

“Pia, juzi (Aprili 4, 2026) ilitokea jijini Dodoma, majira ya mchana na usiku kule mkoani Rukwa na kwa bahati mbaya Mwalimu wa Shule ya Msingi wa mkoani Songwe,  Henry Shubati Myuwanga, alisingiziwa amechukuwa sehemu za siri za kijana mmoja muuza duka eneo la Kilyamatundu, Kata ya Laela, baada ya kushindwana bei ya sabuni ambazo mwalimu huyo huwa anauza.

“Baada ya kushindwana bei ndipo kijana huyo kumkomoa kutokana kushindwa kushawishi auziwe kwa bei nafuu, aliamua kumsingizia mwalimu huyo kwa kupiga kelele kuwa, amechukua sehemu zake za siri, ndipo wananchi walijichukulia sheria mikononi na kumshambulia kwa silaha za jadi hadi kumuua, kisha kumchoma moto,” alisema.

Misime alisema Zanzibar pia  mkazi wa Mwanza, Said Hussein Said, Mkazi wa Mwanza, akiwa katika daladala alimsingizia abiria mwenzake kuwa, amemgusa begani na matokeo yake nyeti zake zimetoweka, jambo lililowalazimu askari polisi waliokuwa eneo hilo kumwokoa aliyesingiziwa.

Aidha, aliyemsingizia mwenzake alifanyiwa uchunguzi na madaktari na ikaonekana hana tatizo lolote.

Alisema kutokana na kitendo hicho, kijana huyo  anashikiliwa kwa mahojiano na uchunguzi zaidi, kubaini wanaofanya uhalifu huo nini kilichopo nyuma yao na malengo yao.

“Imani hizi potofu, za uzushi na za kusingizia watu wengine mpaka hivi sasa zimesabisha vifo vya watu saba ndani ya siku nne na wengine majeruhi wanaendelea na matibabu hospitalini,” alisema.

Aliongeza kuwa: “Kibaya zaidi pamoja na madhara ambayo yameshashuhudiwa wapo baadhi ya watu wanaoendelea kushabikia  na kusambaza upotoshaji huo katika mitandao ya kijamii na wengine wameamua kuutumia kutengeneza vichekesho na kusambaza katika mitandao yao na mingine kwa lengo la kutafuta wafuasi (followers) au kwa malengo mengine wanayofahamu wao.”

Jeshi hilo limeendelea kutoa wito kwa kila mmoja kuendelea kuelimishana kuanzia ngazi ya familia, kuachana na tabia hizo potofu za kishirikina zinazoleta madhara makubwa, yakiwemo mauaji na fedheha kubwa katika karne ya sayansi na teknolojia.

Previous Post

AMANI NYENZO MUHIMU YA MAENDELEO AFRIKA

Next Post

USHIRIKIANO WA CHINA NA AFRIKA KATIKA UJENZI WA RELI YA TAZARA

Next Post
USHIRIKIANO WA CHINA NA AFRIKA KATIKA UJENZI WA RELI YA TAZARA

USHIRIKIANO WA CHINA NA AFRIKA KATIKA UJENZI WA RELI YA TAZARA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

STARS: TUNISIA INAKAA

STARS: TUNISIA INAKAA

3 months ago
MATOKEO YA DARASA LA SABA YATANGAZWA

MATOKEO YA DARASA LA SABA YATANGAZWA

5 months ago

Popular News

  • RAIS WA MUZIKI AHIMIZA AMANI

    RAIS WA MUZIKI AHIMIZA AMANI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • HAKUNA ALIYEPOTEZA NYETI-WAZIRI KATAMBI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. MWIGULU ATANGAZA AHUENI WAFANYABIASHARA SIMU 2000

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • USHIRIKIANO WA CHINA NA AFRIKA KATIKA UJENZI WA RELI YA TAZARA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • POLISI WATIA MGUU SAKATA LA NYETI ZA WANAUME

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?