• ePaper
Thursday, April 16, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

NANAUKA AWAPA HAMASA VIJANA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
April 13, 2026
in Habari, Kitaifa
0
NANAUKA AWAPA HAMASA VIJANA
0
SHARES
11
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na SUPERIUS ERNEST 

WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais, Maendeleo ya Vijana, Joel Nanauka, amewataka vijana nchini, kushiriki katika shindano maalumu la kutafuta wazo bora bunifu la kiuchumi lenye lengo la kuimarisha ubunifu wa vijana na kupata mawazo chanya ya maendeleo endelevu ya Taifa.

Nanauka, alisema hayo jijini Dar es Salaam, alipozungumza na waandishi wa habari kuhusu shindano hilo na kutangaza kamati maalumu ya kuratibu shindano hilo.

“Baada ya kufanikiwa katika mashindano madogo, hivi sasa tumekuja na shindano kubwa la kupata wazo bora bunifu la kiuchumi, linalojulikana kama Vijana Uchumi Challenge.

“Vijana ndiyo nguvu kazi kubwa ya taifa ambayo ni asilimia 55.6.

“Ni nguvu kazi muhimu, tegemewa kwa taifa, wakitegemewa katika ubunifu mbalimbali wa kiuchumi na kidijitali katika kuchochea maendeleo, ndiyo maana tunakuja na shindano hili muhimu kwako,” alisema.

Alisema kupitia jukwaa hilo, wanawataka vijana kutoa wazo bunifu linalotekelezeka, likiendana na Dira ya Taifa ya Maendeleo katika kulinda na kukuza maendeleo ya taifa dhidi ya changamoto  za kiuchumi.

Alisema swali linalobeba shindano hilo, inapotokea changamoto ya kushuka kwa uchumi wa dunia, kwa sababu ya changamoto za kivita ni athari gani zitajitokeza na nini kifanyike kuepuka athari zinazoweza kujitokeza.

Nanauka, alisema lengo la shindano hilo, ni kupata mchango chanya kutoka kwa vijana katika kipindi cha sayansi na teknolojia kuwezesha kuchochea maendeleo ya taifa.

Alitaja zawadi ya washindi wa shindano hilo ni sh. milioni 50, huku akiwataka vijana kujitokeza kwani shindano hilo litafanyika pasipo na upendeleo.

Kwa mujibu wa waziri huyo, shindano hilo litaratibiwa na vijana wenyewe kupitia kamati maalumu aliyoiunda inayoundwa na vijana, ambapo wataandaa maandalizi ya awali, wataratibu na kuhakikisha washindi wanapatikana kwa uwazi pasipo upendeleo.

Waziri huyo, alisema kupitia Jukwaa la Vijana, wameanzisha mashindano madogo, ikiwemo ‘Idea Challenge’ kwa vyuo na vyuo vikuu na ‘idea kitaa’ maalumu kwa vijana wa mtaani.

Alisema kupitia jukwaa hilo, wamelenga na kupata mawazo ya vijana, kutimiza malengo na ubunifu wao kama inavyoeleza sera ya wizara ya vijana.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa kamati hiyo,  Joseph Malekela, alimshukuru waziri kwa kuwaamini katika kamati hiyo, huku akiahidi kutekeleza jukumu hilo kwa wakati na ushirikiano, ambapo leo  wataanza rasmi.

Naye, Mjumbe wa kamati hiyo, Chrispina Kabale, alimshukuru waziri na viongozi kwa kuwaamini na watafanya kazi kwa ushirikiano kufanikisha malengo yaliyokusudiwa.

Previous Post

WACHUMI WATAKA RAIS DK. SAMIA AUNGWE MKONO

Next Post

IGP MSTAAFU MANGU AWAASA WATANZANIA KUEPUKA VISHAWISHI VYA KUVUNJA AMANI

Next Post
IGP MSTAAFU MANGU AWAASA WATANZANIA KUEPUKA VISHAWISHI VYA KUVUNJA AMANI

IGP MSTAAFU MANGU AWAASA WATANZANIA KUEPUKA VISHAWISHI VYA KUVUNJA AMANI

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

DK. NCHIMBI ATAJA SULUHU FOLENI DAR

DK. NCHIMBI ATAJA SULUHU FOLENI DAR

7 months ago
NITAONGOZA KWA KUZINGATIA USHIRIKIANO – SIMBACHAWENE

NITAONGOZA KWA KUZINGATIA USHIRIKIANO – SIMBACHAWENE

5 months ago

Popular News

  • PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SERIKALI YAFUTA LESENI 40 ZA UTAFITI  WA MADINI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TIMU OFISI YA MAKAMU WA RAIS, WIZARA YA MAJI KUCHUANA MEI MOSI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SIMBA, FOUNTAIN GATE SIKU YA HESHIMA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. MWINYI AKAGUA MJI WA AFCON FUMBA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?