• ePaper
Sunday, May 17, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Burudani

MAMBO YAZIDI KUNOGA AFCON 2027

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
April 14, 2026
in Burudani, Habari, Kitaifa, Michezo
0
MAMBO YAZIDI KUNOGA AFCON 2027
0
SHARES
7
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na SELINA MATHEW, Dodoma

SERIKALI imewahakikishia Watanzania kuwa maandalizi ya mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) mwakani, yanaendelea kama yalivyopangwa na hakuna sababu ya kuwa na hofu juu ya kufanyika kwake.

Hayo yalisemwa jijini Dodoma na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda, alipozungumza na waandishi wa habari.

Makonda alisema Tanzania ipo katika hatua nzuri ya maandalizi ya michuano hiyo mikubwa kwa soka Afrika.

Makonda alieleza kuwa, Rais Dk. Samia Suluhu Hassan ametoa fedha za kutosha kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu, huku mkandarasi akiwa tayari kazini kuhakikisha kila kitu kinakamilika kwa wakati.

Alisisitiza kuwa taarifa zinazosambaa mitandaoni kuhusu uwezekano wa kuahirishwa kwa mashindano hayo hazina ukweli wowote na ni sehemu ya upotoshaji.

“Maneno yanayotapakaa mitandaoni, kejeli na mipango miovu ya kutaka kuhalalisha kuahirishwa kwa AFCON kamwe hayatapata nafasi, ratiba iliyopangwa ipo vilevile,” alisema.

Aliongeza kuwa, Rais wa Shirikisho la Soka Afrika (CAF) na timu yake walishakubaliana na maandalizi ya Tanzania kuwa mwenyeji na fedha zote muhimu tayari zimeshalipwa kuhakikisha mashindano yanafanyika nchini.

Hata hivyo, alisema mijadala inayoendelea mitandaoni ina mchango chanya kwani inachochea ari na kuwakumbusha Watanzania kuwa muda wa mashindano unakaribia, huku akisisitiza kuwa ratiba ipo palepale.

Previous Post

GWAJIMA AKATA MZIZI WA FITNA ‘ISHU’ BEGA NA NYETI KUTOWEKA

Next Post

BARKER MENO NJE MSIMBAZI

Next Post
BARKER MENO NJE MSIMBAZI

BARKER MENO NJE MSIMBAZI

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

MWENEZI KIHONGOSI NA MSISITIZO WA MAENDELEO, SIYO VURUGU

MWENEZI KIHONGOSI NA MSISITIZO WA MAENDELEO, SIYO VURUGU

2 months ago
DK. MWINYI ACHUKUA FOMU ZANZIBAR, AHADHARISHA CHUKI

DK. MWINYI ACHUKUA FOMU ZANZIBAR, AHADHARISHA CHUKI

9 months ago

Popular News

  • DK. MWIGULU AHIMIZA WANANCHI KUIOMBEA AMANI YA NCHI

    DK. MWIGULU AHIMIZA WANANCHI KUIOMBEA AMANI YA NCHI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. KIKWETE ASHIRIKI MAZISHI YA KITAIFA YA RAIS MSTAAFU MOGAE WA BOTSWANA, AKIMWAKILISHA RAIS DK. SAMIA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DANGOTE AIPONGEZA SERIKALI, AANGAZIA FURSA ZA UWEKEZAJI NCHINI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TANZANIA NI NCHI YA PILI AFRIKA KUWA NA HADHI YA  UTALII WA JIOLOJIA (GEOPARK MUSEUM)

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SERIKALI YAIPONGEZA PUMA ENERGY KWA MFUMO MPYA WA KIDIJITALI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?