• ePaper
Thursday, May 7, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Burudani

YANGA MBELE KWA MBELE

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
May 7, 2026
in Burudani, Habari, Kitaifa, Michezo
0
YANGA MBELE KWA MBELE
0
SHARES
3
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na MWANDISHI WETU

BAO pekee la Allan Okello limeifanya Yanga kuendelea kubaki kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara, uliochezwa jana Uwanja wa KMC Complex, Dar es Salaam.

Hilo ni bao la tatu kwa Okello tangu alipotambulishwa Yanga,  Januari 13, mwaka huu, akianza kufunga dhidi ya Singida Black Stars kisha katika mechi dhidi ya Tanzania Prisons kabla ya jana kufunga bao la ushindi dhidi ya KMC.

Katika mechi ya awali iliyozikutanisha Yanga na KMC, Yanga iliibuka na ushindi wa mabao 4-1, katika mechi iliyopigwa dimba la Benjamin Mkapa.

Ushindi huo, umeiwezesha Yanga yenye maskani yake mitaa ya Twiga na Jangwani jijini Dar es Salaam kufikisha pointi 51, ikiwa kileleni mwa msimamo huku KMC ikiendelea kuburuza mkia ikiwa na alama tisa baada ya timu zote kushuka dimbani mara 21.

Katika mechi hiyo, mchezo ulianza kwa kasi huku timu zote zikishambuliana kwa zamu na kutafuta ushindi, dakika ya 10    Prince Dube alipata nafasi ya kufunga lakini shuti alilopiga liliishia mikononi mwa kipa wa KMC, Ismail Mpank.

Yanga iliendelea kufanya  mashambulizi na dakika ya 25,  mchezaji Maxi Nzengeli alishindwa kufunga baada ya kupiga shuti kali lakini mpira ulipaa  angani.

Yanga iliyokuwa ikihitaji ushindi wa hali na mali iliendelea kucheza kwa kasi na kutafuta alama tatu   muhimu kabla ya dakika ya 37   Laurindo Dilson ‘Depu’ kupiga shuti kali na mpira kutoka nje, Depu alimalizia pasi safi kutoka kwa Dube.

Dakika ya 51, Yanga ilipata nafasi nyingine kupitia kwa Okello baada ya kupiga shuti kali na mpira kupaa angani, Okello alimalizia pasi safi kutoka kwa Duke Abuya.

Mashambulizi yaliyofanywa na Yanga yaliiwezesha timu hiyo kuandika bao la kuongoza dakika ya 65 baada ya Okello kupiga shuti kali na mpira kujaa kambani baada ya kumalizia pasi safi kutoka kwa Shekhan Ibrahim.

KMC nayo ilijibu shambulizi dakika ya 89 baada ya mchezaji wake Darueshi Saliboko kupiga shuti kali na mpira kutoka nje kabla ya

Yanga kujibu mapigo dakika ya 90 wakati Dube akimalizia pasi safi kutoka kwa Emmanuel Mwanengo.

KMC: Ismail Mpank, Juma Shemvuni, Nikson Mosha, Ken Ally, Samson Mwaituka, Redrmtus Mussa, Erick Mwijage, Mudathir Nassor, Kelvin Tondi, Darueshi Saliboko na Oscar Paulo.

Yanga: Djigui Diarra, Frank Assik, Ibrahim Abdullah, Maxi Nzengeli, Laurindo Dilson, Chadrack Boka, Allan Okello, Aziz Andambwile, Prince Dube, Koussi Yao na Duke Abuya.

Wakati huo huo, uongozi wa klabu ya Yanga umemfuta kazi kocha mkuu wa timu hiyo, Pedro Goncalves.

Taarifa iliyotolewa jana, imeeleza kuwa uongozi wa klabu hiyo unamshukuru kocha huyo kwa mchango wake alioutoa  ndani ya klabu hiyo na unamtakia kheri.

Taarifa imesema timu hiyo itakuwa chini ya kocha Abdihamid Moalin na kocha Patrick Mabedi hadi mwisho wa msimu. 

Previous Post

WATAALAMU WAFUNGUKA MITAZAMO YA MIKATABA 8

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

KIHONGOSI AMWASHIA MOTO KIGOGO HOSPITALI MANYONI

KIHONGOSI AMWASHIA MOTO KIGOGO HOSPITALI MANYONI

4 months ago
SADC WAMPONGEZA RAIS DK. SAMIA KWA USHINDI UCHAGUZI MKUU OKTOBA 2025

SADC WAMPONGEZA RAIS DK. SAMIA KWA USHINDI UCHAGUZI MKUU OKTOBA 2025

6 months ago

Popular News

  • YANGA MBELE KWA MBELE

    YANGA MBELE KWA MBELE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WATAALAMU WAFUNGUKA MITAZAMO YA MIKATABA 8

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. SAMIA AKEMEA VIONGOZI ‘KUVIMBA’

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DEMOKRASIA ISIZICHAFUE NCHI ZETU – RAIS DK. SAMIA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • ZIARA YA RAIS KAGAME, RUTO KUIMARISHA DIPLOMASIA KIUCHUMI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?