• ePaper
Friday, June 12, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

BAJETI YA KUJITEGEMEA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
June 11, 2026
in Habari, Kitaifa
0
BAJETI YA KUJITEGEMEA
0
SHARES
1
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

NA MUSSA YUSUPH

NI bajeti inayochochea mageuzi ya kiuchumi, ujenzi wa viwanda na Taifa linalojitegemea.

Hiyo ni kauli ya Waziri wa Fedha, Balozi Khamis Mussa Omar, aliyoitoa alipowasilisha Bajeti Kuu ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2026/2027 ya sh. trilioni 62.3 bungeni jijini Dodoma.

Bajeti hiyo ni ongezeko la asilimia 10.3 ikilinganishwa na bajeti ya mwaka 2025/26 huku mapato yanatarajiwa kuwa sh. trilioni 46.79 ambapo mapato ya kodi ni sh. trilioni 36.99, mapato mengine ni sh. trilioni 9.24 ikijumuisha mapato ya Mamlaka za Serikali za Mitaa sh. trilioni 1.97 na misaada kutoka kwa washirika wa maendeleo sh. bilioni 563.1.

“Ili kuendana na dhamira yetu ya kujitegemea katika uendeshaji wa serikali na maendeleo, takribani robo tatu ya bajeti yote ya mwaka 2026/27, sawa na asilimia 74.2 inatarajiwa kugharamiwa na mapato ya ndani,” alisisitiza.

Kwa mujibu wa Balozi Khamis, bajeti hiyo ni ya kwanza katika utekelezaji Mpango wa Nne wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano (2026/2027 – 2030/2031).

Alisema katika bajeti hiyo iliyojikita katika utekelezaji Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, imezingatia kuweka mazingira bora yenye kugusa maisha ya kila Mtanzania katika nyanja za uwezeshaji kiuchumi na huduma za kijamii.

Balozi Khamis alisema mapendekezo ya hatua mpya za kodi yatajibu maswali na kukidhi kiu ya wananchi, wafanyabiashara na wawekezaji kwa kuweka sera zinazochochea uwekezaji, uzalishaji, kulinda viwanda na kuchangia katika kufikia malengo ya Dira 2050.

“Maboresho haya, yanalenga kukuza uchumi, kuongeza fursa za ajira na hatimaye kupunguza ukali wa maisha ya wananchi. Hatua hizo zinalenga pia kuimarisha usimamizi, ukusanyaji mapato ya ndani na kudhibiti upotevu mapato ya serikali.

Alisisitiza: “Wakati serikali ikiyafanyia kazi kwa kina maoni yaliyotolewa na Tume ya Rais ya Maboresho ya Mfumo wa Kodi, mapendekezo ya kurekebisha mfumo wa kodi kwa mwaka 2026/27 yamezingatia baadhi ya maoni hayo,”

MAFUTA YA KULA

Balozi Khamis alisema serikali imeweka vivutio vya kikodi kuhamasisha kilimo na matumizi ya mbegu za mafuta zinazozalishwa nchini, kuhakikisha upatikanaji bidhaa hiyo kwa gharama nafuu.

Alisema serikali inapendekeza msamaha wa kodi ya ongezeko la thamani kwenye mafuta ya kula yaliyozalishwa kwa kutumia mbegu zinazozalishwa nchini.

Aidha alisema imependekeza kutoza ushuru wa forodha kwa kiwango cha asilimia 10 kwenye mafuta ghafi ya kula yanayoingizwa nchini isipokuwa ya chikichi.

“Ushuru wa mauzo ya kusafirisha nje ya nchi wa asilimia 10 katika mafuta ghafi ya alizeti na mbegu zake, ushuru wa forodha wa asilimia sifuri kwenye mafuta ghafi ya kula ya chikichi na asilimia 10 katika mafuta ya chikichi yaliyochakatwa kwa kiwango cha kati.

URASIMISHAJI SEKTA ISIYO RASMI

Kwa mwaka 2026/2027, alisema serikali inaendelea kuweka mazingira wezeshi ya kuvutia urasimishaji wa sekta isiyo rasmi ambayo inaajiri zaidi vijana na wanawake.

Katika kufanikisha azma hiyo, alisema serikali itatoa msamaha wa kodi ya mapato kwa wafanyabiashara wapya kwa kipindi cha mwaka mmoja tangu tarehe ya kupata namba ya utambulisho wa mlipakodi.

Alisema serikali itafanya maboresho kwenye Sheria ya Fedha za Serikali za Mitaa, Sura 290, kuwezesha Mamlaka za Serikali za Mitaa kutenga asilimia 15 ya mapato yao ya ndani badala ya asilimia 10 iliyopo sasa ya mikopo ya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu.

“Kati ya asilimia 15 itakayotengwa, asilimia 10 itaelekezwa kwenye mikopo ya wanawake, vijana na wenye ulemavu kwa uwiano kama ilivyokuwa awali na asilimia tano itatumika kwa ajili ya uwekezaji miradi ya ujenzi na maboresho ya masoko, maeneo ya biashara na ujasiriamali ili kuvutia na kuongeza fursa za ajira hususan kwa vijana, wanawake na makundi maalumu,” alieleza.

NGUO ZINAZOZALISHWA NCHINI

Balozi Khamis alisema serikali inapendekeza kusamehe kodi ya ongezeko la thamani kwenye nguo na mavazi yanayozalishwa kwa kutumia pamba inayozalishwa nchini.

Alisema lengo la hatua hiyo ni kuhamasisha matumizi ya pamba inayozalishwa nchini, hatua ambayo inatarajiwa kuokoa mapato ya serikali yanayotokana na marejesho kwa mlipakodi kwa kiasi cha sh. bilioni 6.30

USHURU JUU BIDHAA ZA UREMBO

Alisema serikali inapendekeza kuongeza kiwango cha ushuru wa bidhaa kutoka asilimia 10 hadi asilimia 15 kwenye bidhaa za urembo zinazoingizwa ndani ya nchi.

Alisema lengo la hatua hiyo ni kuongeza mapato ya serikali na kuwianisha kiwango husika na viwango vinavyotozwa na baadhi ya nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki ikiwemo Kenya, Uganda na Rwanda.

USHURU MAGARI CHINI YA CC 1,000

Alibainisha kuwa serikali inapendekeza kutoza ushuru wa bidhaa kwa kiwango cha asilimia tano kwenye magari yanayotambulika kwa HS Code 8703.21.90 yenye ukubwa wa injini (CC) kuanzia 1,000 kushuka chini.

Alibainisha kuwa lengo la hatua hiyo ni kuongeza wigo wa kodi na mapato ya serikali.

Katika kujibu kilio cha muda mrefu, alisema serikali inapendekeza kufanya marekebisho ya Sheria ya Usalama Barabarani, Sura 168 ili kuruhusu gari au trela iliyosajiliwa kwa mujibu wa sheria za usajili Tanzania Zanzibar kutumika Tanzania Bara likiwa na namba za usajili za Tanzania Zanzibar, pale ambapo kodi zote kwenye gari au trela husika zimelipwa kwa mujibu wa sheria na taratibu zilizopo.

Aidha, alisema kwa sasa utaratibu huo unatumika kwa magari yanayotoka Tanzania Bara kwenda Tanzania Zanzibar.

NISHATI SAFI

Kwa mujibu wa Waziri wa Fedha, serikali imeendelea kuweka hatua mbalimbali za kodi zinazochochea matumizi ya nishati ya umeme na gesi asilia katika sekta ya usafiri na nyumbani.

Alisema serikali inapendekeza kusamehe kodi ya ongezeko la thamani kwenye vifaa vitakavyotumika katika vituo vya kuchaji magari yanayotumia umeme vinavyoingizwa nchini vinavyotambulika kwa HS Code 8504.40.00.

Hata hivyo, alisema zipo hatua zinazotekelezwa ambazo ni msamaha wa ushuru wa bidhaa kwa kuzingatia uwezo wa injini kwenye magari yanayotumia umeme na gesi.

Alisema uwepo wa msamaha wa kodi ya ongezeko la thamani kwenye gesi asilia iliyoshindiliwa yanayotumika kwenye magari, msamaha wa kodi ya ongezeko la thamani kwenye vifaa vya usambazaji wa CNG na msamaha wa kodi ya ongezeko la thamani kwenye mnyororo mzima wa uzalishaji wa CNG.

TOZO MPYA NIDA

Katika hatua nyingine, alisema serikali inatarajia kukusanya jumla ya sh. milioni 734.4 kupitia kuanzishwa kwa tozo mpya za huduma zinazotolewa na Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA).

Balozi Khamis alisema hatua hiyo inalenga kukabiliana na ongezeko la mahitaji ya taarifa kutoka katika kanzidata ya NIDA ambayo yamekuwa yakiongeza gharama za uendeshaji.

Alieleza kuwa kupitia marekebisho hayo, wananchi watakaohitaji kupata taarifa zao kutoka NIDA watalazimika kulipa tozo ya sh. 500 kwa kila ombi la taarifa.

Alisema taarifa zitakazotolewa ni majina ya wazazi, shule aliyosoma, namba ya simu na taarifa nyingine muhimu zilizohifadhiwa kwenye kanzidata ya mamlaka hiyo.

Hivyo, alisema wananchi watakaohitaji kupatiwa nakala ya taarifa hizo kwa njia ya maandishi watalazimika kulipa ada ya sh. 1,000 kwa kila nakala.

Balozi Omar alisema lengo la hatua hiyo ni kugharamia utoaji huduma hizo ikiwemo gharama za uchapishaji, matumizi ya mifumo ya TEHAMA na kuhakikisha huduma za utambuzi zinaendelea kutolewa kwa ufanisi na kwa muda mrefu.

Alisisitiza kuwa maboresho hayo pia yataisaidia serikali kuimarisha mifumo ya utambuzi wa wananchi na kuongeza uwazi katika utoaji wa taarifa muhimu kwa matumizi mbalimbali ya kijamii na kiuchumi.

ADA MTANDAONI ZAPUNGUZWA

Serikali imetangaza punguzo kubwa la ada za huduma za maudhui mtandaoni katika hatua inayolenga kuwawezesha vijana kushiriki kikamilifu katika uchumi wa kidijitali na kukuza ubunifu nchini.

Balozi Khamis alisema marekebisho hayo yatafanyika kupitia Kanuni za Mawasiliano ya Kielektroniki na Posta (Maudhui Mtandaoni).

Alieleza kuwa ada ya maombi ya leseni ya huduma za maudhui mtandaoni imepunguzwa kutoka sh. 50,000 hadi sh. 10,000 hatua itakayorahisisha upatikanaji leseni kwa vijana wengi wanaojihusisha na shughuli za mtandaoni.

“Ada za mwanzo za mwaka na za kuhuisha leseni zimepunguzwa kwa kiasi kikubwa kutoka sh. 500,000 hadi sh. 50,000 jambo linalotarajiwa kupunguza gharama za uendeshaji kwa watoa huduma,” alisisitiza.

Pia, alisema serikali imepunguza ada ya maombi ya leseni ya mtengeneza maudhui mtandaoni kutoka sh. 100,000 hadi sh. 20,000 ili kuvutia wawekezaji zaidi katika sekta hiyo.

Vilevile, alisema ada za mwanzo za mwaka na za kuhuisha leseni ya watengeneza maudhui mtandaoni zimepunguzwa kutoka sh. 1,000,000 hadi sh. 100,000, hatua inayolenga kuongeza ushindani na ubunifu katika tasnia ya kidijitali.

Balozi Omar alisema lengo la hatua hiyo ni kuweka mazingira rafiki kwa vijana na wabunifu wa maudhui ili waweze kutumia fursa za teknolojia kujipatia kipato na kuchangia ukuaji uchumi wa taifa.

ADA MPYA ZA MAKUMBUSHO

Balozi Khamis alisema serikali inapendekeza kuanzisha ada mpya za usajili na uendeshaji makumbusho binafsi nchini, hatua inayolenga kuimarisha usimamizi sekta ya utalii na kuongeza mapato ya serikali.

Alisema hatua hiyo itatekelezwa kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kuweka utaratibu rasmi wa usajili na uendeshaji wa makumbusho binafsi.

Kwa mujibu wa mapendekezo hayo, raia wa Tanzania watakaotaka kusajili makumbusho binafsi watalipa ada ya sh. 50,000, huku taasisi za ndani zikilipa sh.100,000.

Aidha, raia wa kigeni watakaotaka kusajili makumbusho binafsi nchini watalipa ada ya sh. 500,000 hatua inayolenga kudhibiti na kuratibu uwekezaji wa sekta hiyo.

Previous Post

SERIKALI ITAENDELEA KUBORESHA MAZINGIRA YA UWEKEZAJI – DK. MWIGULU

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

KOCHA SERENGETI BOYS AKOSHWA NA KIWANGO

KOCHA SERENGETI BOYS AKOSHWA NA KIWANGO

7 months ago
MCHUJO MKALI  KOCHA SIMBA

MCHUJO MKALI  KOCHA SIMBA

6 months ago

Popular News

  • BAJETI YA KUJITEGEMEA

    BAJETI YA KUJITEGEMEA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SERIKALI ITAENDELEA KUBORESHA MAZINGIRA YA UWEKEZAJI – DK. MWIGULU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • YANGA, SIMBA VITA KALI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TANZANIA, SINGAPORE KUSHIRIKIANA KIMKAKATI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. SAMIA ANADI FURSA KEMKEMU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Not enough quota to unlock this post
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?