• ePaper
Monday, June 29, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

RAIS DK. SAMIA AVUTIA UWEKEZAJI WA TIJA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
June 29, 2026
in Habari, Kitaifa
0
RAIS DK. SAMIA AVUTIA UWEKEZAJI WA TIJA
0
SHARES
7
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na MWANDISHI MAALUMU

RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema serikali itaendelea kushirikiana na sekta binafsi katika kuvutia uwekezaji wenye tija, unaochochea ukuaji wa uchumi, maendeleo ya viwanda, uhamishaji wa teknolojia na ajira kwa Watanzania.

Aidha, amesema serikali imepokea nia ya Mwenyekiti na Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Dangote Group, Alhaj Aliko Dangote, ya utayari wa kampuni yake, kupanua ushirikiano wa uwekezaji katika sekta mbalimbali za kimkakati.

Rais Dk. Samia, alisema hayo Ikulu, jijini Dar es Salaam, alipokutana na kufanya mazungumzo na Mwenyekiti na Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Dangote Group, Dangote.

Kutokana na nia hiyo ya Dangote, Rais Samia, alizielekeza wizara na taasisi husika, kuendelea na majadiliano ya kitaalamu kuhusu maeneo yaliyojadiliwa, kwa kuzingatia sera, sheria na vipaumbele vya maendeleo ya nchi.

Dangote, ambaye ni mwekezaji na mfanyabiashara kinara barani Afrika, alieleza utayari wa kampuni yake kupanua ushirikiano wa uwekezaji na serikali katika sekta mbalimbali za kimkakati.

Mazungumzo hayo, yaligusa maeneo ya miundombinu ya usafirishaji, uzalishaji wa mbolea nchini na nishati, ikiwa ni sehemu ya fursa za uwekezaji zinazochochea shughuli za kiuchumi nchini na katika ukanda.

Dangote alisema Tanzania ina mazingira mazuri ya uwekezaji na fursa kubwa za kukuza viwanda vinavyoongeza thamani ya malighafi na kuchochea biashara ya kikanda.

“Tumetambua maeneo yenye manufaa makubwa kwa Tanzania na tuko tayari kushirikiana na Serikali kuyaendeleza kwa manufaa ya pande zote,” alisema.

WALIPOKUTANA MEI 16, 2026

Mei 16, mwaka huu, Rais Dk. Samia, alikutana na kuzungumza na Mwenyekiti na Mtendaji Mkuu wa Dangote Group, Alhaji Dangote, Ikulu, jijini Dar es Salaam.

Katika mazungumzo yao, walijadili kuhusu kuimarisha ushirikiano kati ya serikali na kampuni za Dangote katika nishati, viwanda, bandari, gesi, mbolea na miundombinu.

Rais Samia alimhakikishia ushirikiano na kumwomba Alhaji Dangote, aendelee kuangalia fursa zaidi za biashara na uwekezaji nchini zenye tija na manufaa kwa mwekezaji, serikali na taifa kwa ujumla.

Aidha, Rais Samia, aliikaribisha Dangote Group, kuwekeza katika uzalishaji wa mbolea nchini, akibainisha kuwa, mahitaji ya bidhaa hiyo ni makubwa kuliko uwezo wa sasa wa uzalishaji wa ndani.

Katika mjadala huo, Alhaji Dangote, alitumia fursa hiyo kuipongeza serikali kwa kuboresha mazingira ya biashara, uwekezaji na kutatua changamoto za wawekezaji nchini.

Pia, alielezaa hatua za serikali kutatua changamoto zilizokuwa zikikabili shughuli za Kiwanda cha Saruji cha Dangote, mkoani Mtwara, zimeongeza tija na ufanisi wa uendeshaji na imani ya kampuni hiyo kwa Tanzania kama eneo muhimu na la kimkakati la uwekezaji barani Afrika.

Previous Post

HAKUNA MJADALA AMANI, USALAMA WA NCHI-MWIGULU

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

KISHINDO CHA DK. SAMIA MIKOA 10

KISHINDO CHA DK. SAMIA MIKOA 10

10 months ago
TASWIRA VIGOGO VINNE LIGI KUU BARA IKO HIVI

TASWIRA VIGOGO VINNE LIGI KUU BARA IKO HIVI

4 months ago

Popular News

  • RAIS DK. SAMIA AVUTIA UWEKEZAJI WA TIJA

    RAIS DK. SAMIA AVUTIA UWEKEZAJI WA TIJA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • HAKUNA MJADALA AMANI, USALAMA WA NCHI-MWIGULU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • YANGA, SIMBA SIKU YA KILIO,KICHEKO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • VIJANA 400  WAAGWA KWENDA KUFANYA KAZI NJE YA NCHI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • ‘NAFUU YA MAFUTA KUANZA KUONEKANA JULAI’ NDEJEMBI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Not enough quota to unlock this post
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?