• ePaper
Sunday, July 26, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Burudani

SIMBA, SINGIDA BS MACHO ‘KAGAME CUP’

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
July 10, 2026
in Burudani, Habari, Kitaifa, Michezo
0
SIMBA, SINGIDA BS MACHO ‘KAGAME CUP’
0
SHARES
12
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na NASRA KITANA

WAKATI droo ya michuano ya ‘Kagame Cup’, ikitarajiwa kufanyika leo, timu za Simba na Singida Black Stars  zipo mbioni kutua nchini Rwanda.

Michuano hiyo inatarajiwa kuanza kufanyika Julai 24 hadi Agosti 7, mwaka huu nchini Rwanda,

Jumla ya timu 12 zinatarajiwa kushiriki mashindano ya mwaka huu ambazo ni bingwa mtetezi Singida Black Stars, Simba kutoka Tanzania na KVZ ya Zanzibar.

Zingine ni APR na Rayon Sports za Rwanda, Vipers (Uganda), Al Hilal na El Merriekh (Sudan), Gor Mahia (Kenya), Mogadishu City (Somalia), Jamus (Sudan Kusini) na FC Garde Républicaine ya Djibouti.

Droo hiyo, itafanyika leo katika nchini Rwanda  kuanzia saa 4:00 asubuhi, ikiwa ni maandalizi ya mashindano hayo yatakayochezwa katika viwanja vya Kigali Pele na Amahoro.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi, Mratibu wa klabu ya Simba, Abbasi Ally alisema kuwa timu yao inatarajiwa kutua nchini Rwanda, Julai 21, mwaka huu.

“Angalia Ligi Kuu Tanzania Bara itaanza  mwezi Agosti mwanzoni, tutashiriki mashindano hayo, kwa ajili ya kujiandaa na msimu mpya wa Ligi Kuu.

“Tumefikiria kwa kina  na kuamua kwenda kushiriki mashindano hayo awali tuliona kama ratiba inabana, tunataka kufanya maandalizi yetu ya msimu ujao , tutakuwa na muda mzuri wa maandalizi,” alisema Abasi.

Kwa upande wa Ofisa Habari wa Singida BS, Hussein Massanza alisema timu yao imethibitisha ushiriki katika mashindano hayo, lakini imeweka kipengele cha kulipwa fedha zao za ubingwa wa msimu uliopita ndio washiriki.

Awali, Singida BS walikuwa wakidaiwa kuwa huenda wasishiriki kutokana na kutopewa zawadi ya kutwaa ubingwa wa michuano hiyo msimu uliopita ambapo ni dola 30,000 ambazo ni zaidi ya sh. Millioni 78 milioni.

“Sisi kama Singida BS tumethibitisha kushiriki mashindano hayo, tumeshawasiliana na viongozi wa CECAFA wamesema kuwa walipa zawadi yetu ya ubingwa kabla ya kuanza kwa mashindano hayo,” alisema Massanza.

Massanza alisema mashindano hayo, watayatumia kama sehemu ya maandalizi ya msimu ujao  wa ligi kuu.

Singida Black Stars katika mashindano hayo ndio mabingwa watetezi baada ya msimu uliopita kuifunga Al Hilal ya Sudan  kwa mabao 2-1 katika mchezo wa fainali uliochezwa Dar es Salaam.

Mashindano ya mwaka huu yanatarajiwa kuwa na ushindani mkubwa kutokana na ushiriki wa baadhi ya mabingwa na vigogo wa ukanda wa Afrika Mashariki na Kati, huku yakitumika kama kipimo muhimu kuelekea msimu mpya wa mashindano ya kimataifa ya CAF.

Previous Post

RAIS DK. MWINYI : TAMKO LA PAMOJA CCM NA ACT-WAZALENDO LAFUNGUA NJIA YA UTEKELEZAJI WA SERIKALI YA UMOJA WA KITAIFA

Next Post

CHINA YAZIDI KUSISITIZA USHIRIKIANO KWA AFRIKA

Next Post
CHINA YAZIDI KUSISITIZA USHIRIKIANO KWA AFRIKA

CHINA YAZIDI KUSISITIZA USHIRIKIANO KWA AFRIKA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

‘WALIPENI WAKULIMA, WAFANYAKAZI’

‘WALIPENI WAKULIMA, WAFANYAKAZI’

11 months ago
MWAKINYO KUPIMA UZITO LEO

MWAKINYO KUPIMA UZITO LEO

7 months ago

Popular News

  • KATIBA MSINGI WA HAKI – DK. NCHIMBI

    KATIBA MSINGI WA HAKI – DK. NCHIMBI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MABASI YA UMEME REKODI ZANZIBAR

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • KOCHA AIPA JEURI YANGA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MWALIMU, GUEYE WAPO SIMBA SANA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WAZIRI ASHTUKIA ‘USANII’ WA WACHIMBAJI MADINI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Not enough quota to unlock this post
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?