• ePaper
Sunday, May 31, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Burudani

EL KAABI ANAWIRI AFCON

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
December 30, 2025
in Burudani, Kimataifa, Michezo
0
EL KAABI ANAWIRI AFCON
0
SHARES
11
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

RABAT, Morocco

NYOTA wa timu ya taifa ya Morocco, Ayoub El Kaabi, juzi alinawiri kufuatia kufunga mabao mawili katika ushindi wa 3-0 dhidi ya Zambia, katika mchezo wa makundi wa michuano ya Mataifa ya Afrika (AFCON 2025), uliofanyika Uwanja wa Prince Moulay Abdallah, Rabat, Morocco.

Kufuatia ushindi huo, Morocco imetinga hatua ya 16 bora ya michuano hiyo kufuatia kumaliza kileleni mwa msimamo wa kundi A, ikiwa na pointi saba ikifuatiwa na Mali yenye pointi tatu huku Comoro na Zambia zikifikisha pointi mbili kila mmoja katika mechi tatu zilizocheza.

Katika mchezo huo, El Kaabi alifunga bao la kwanza katika dakika ya tisa akiunganisha kwa kichwa kona iliyochongwa na Azzadine Ounani na kuujaza mpira kimiani.

Morocco walionekana kulishambulia mara kwa mara lango la Zambia, dakika ya 27, ilipata bao la pili lililowekwa wavuni na mchezaji Brahim Diaz kufuatia kazi nzuri iliyofanywa na Abde Ezzalzouli.

El Kaabi alifunga bao la tatu dakika ya 50 kwa staili ya kibaiskeli pasi ya mwisho ilitoka kwa Ounahi na kuipeleka timu yake hatua ya 16 bora ya michuano hiyo msimu huu.

El Kaabi alisema, amefurahia kuisaidia timu yake kupata ushindi na kusonga mbele katika michuano hiyo huku wakimaliza hatua ya makundi wakiwa kileleni mwa msimamo.

“Tumemaliza hatua ya makundi ya michuano ya AFCON 2025 tukiwa kileleni, nimefurahia kuisaidia timu kutinga hatua inayofuata, tunakwenda kujipanga kuhakikisha tunafanya vizuri zaidi mechi zijazo,” alisema.

Kufuatia ushindi huo, Morocco imetinga hatua ya 16 bora ikiungana na timu za Mali, Afrika Kusini, Misri, Nigeria na Algeria kabla ya mechi za jana.

Previous Post

MAJIHA APANIA KUTETEA MKANDA WBO AFRIKA

Next Post

TAIFA STARS YAWEKA HISTORIAYA KIBABE AFCON

Next Post
TAIFA STARS YAWEKA HISTORIAYA KIBABE AFCON

TAIFA STARS YAWEKA HISTORIAYA KIBABE AFCON

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

WASHIRIKI MISS WORLD TANZANIA WAPEWA SOMO

WASHIRIKI MISS WORLD TANZANIA WAPEWA SOMO

2 months ago
DK. SAMIA AFICHUA FAIDA MAPINDUZI YA VIWANDA

DK. SAMIA AFICHUA FAIDA MAPINDUZI YA VIWANDA

8 months ago

Popular News

  • SERENGETI BOYS KILA KONA, RAIS SAMIA AWAPA MILIONI 500/-

    SERENGETI BOYS KILA KONA, RAIS SAMIA AWAPA MILIONI 500/-

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAS: UTUNZAJI MAZINGIRA AJENDA YA KIPAUMBELE KWA MKOA WA MWANZA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • UPELE UMEPATA MKUNAJI STARS

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • ‎ RAIS DK. SAMIA: POLISI MSIDHARAU TAARIFA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. MWIGULU ATETA NA WAZIRI MKUU WA CONGO BRAZZAVILLE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?