• ePaper
Thursday, April 16, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

SERIKALI IMEIMARISHA BARABARA – DK. SAMIA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
September 10, 2025
in Habari, Kitaifa, Siasa, Uchaguzi
0
SERIKALI IMEIMARISHA BARABARA – DK. SAMIA
0
SHARES
3
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

NA MUSSA YUSUPH,

Bahi

MGOMBEA Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema serikali imeimarisha zaidi miundombinu ya barabara katika kipindi cha miaka mitano.

Dk. Samia aliyasema hayo katika mkutano wake wa kampeni uliofanyika wilayani Bahi mkoani Dodoma alipokuwa njiani kwenda mkoani Singida.

Alisema katika wilaya hiyo, yamejengwa madaraja tisa na barabara za changarawe zenye urefu wa kilometa 152 zinazopitika kipindi chote cha mwaka.

“Nimejulishwa kuna barabara ya Mwanachungu- Bahi hadi SGR yenye urefu wa kilometa sita ambako kuna changamoto kuvuka eneo la Mto Mkogwa wakati wa masika.

“Hii barabara tumeipanga kuijenga kwa awamu mbili, tutaanza kujenga daraja la Mto Mkogwa ambalo limekuwa kero kubwa katika maeneo hayo,” alisema.

Dk. Samia alisema usanifu wa daraja hilo, umekamilika kazi iliyopo ni kuanza ujenzi kisha litakapokamilika barabara hiyo itajengwa.

Akizungumzia miundombinu, mgombea ubunge Jimbo la Bahi, Kenneth Nollo, alisema barabara nyingi zimeboreshwa na madaraja kujengwa, hatua iliyorahisisha usafiri na shughuli za kiuchumi. 

Hata hivyo, aliomba serikali kuongeza ujenzi wa barabara za lami katika mji wa Bahi kuupa hadhi zaidi.

“Ombi langu kwa serikali ni kutupatia angalau kilomita tano za barabara ya lami, kuuboresha mji wetu wa Bahi ambao unaendelea kukua kwa kasi,” alisema.

Katika sekta ya elimu, alisema shule mpya 14 zimejengwa wilayani humo, jambo linaloonesha jitihada kubwa za serikali katika kuboresha huduma za kijamii kwa wananchi wa Bahi.

Nollo alieleza kufurahishwa na ujenzi wa kituo cha SGR na bandari kavu katika eneo hilo, akisema uwekezaji huo unaifanya Bahi kuwa kitovu muhimu cha biashara na uchukuzi.

Previous Post

1,172,279 KUFANYA MTIHANI WA LA SABA

Next Post

FIDIA YANUKIA WANANCHI WALIOPISHA MRADI SGR

Next Post
FIDIA YANUKIA WANANCHI WALIOPISHA MRADI SGR

FIDIA YANUKIA WANANCHI WALIOPISHA MRADI SGR

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

SIMBA HESABU KALI, YANGA NI USHINDI TU

SIMBA HESABU KALI, YANGA NI USHINDI TU

2 months ago
DK. NCHIMBI AMTAJA DK. SAMIA UJENZI BANDARI YA KWALA

DK. NCHIMBI AMTAJA DK. SAMIA UJENZI BANDARI YA KWALA

6 months ago

Popular News

  • PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SERIKALI YAFUTA LESENI 40 ZA UTAFITI  WA MADINI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TIMU OFISI YA MAKAMU WA RAIS, WIZARA YA MAJI KUCHUANA MEI MOSI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SIMBA, FOUNTAIN GATE SIKU YA HESHIMA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. MWINYI AKAGUA MJI WA AFCON FUMBA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?