• ePaper
Sunday, May 31, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

HALI YA USALAMA MKOA WA ARUSHA NI SHWARI – RC MAKALLA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
November 4, 2025
in Habari, Kitaifa
0
HALI YA USALAMA MKOA WA ARUSHA NI SHWARI – RC MAKALLA

MKUU wa Mkoa wa Arusha, CPA Amos Makalla

0
SHARES
10
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na MWANDISHI WETU,

ARUSHA

MKUU wa Mkoa wa Arusha, CPA Amos Makalla, amewahakikishia wananchi wa mkoa huo kuwa, hali ya ulinzi na usalama ni shwari na shughuli za kijamii na kiuchumi zimerejea katika hali ya kawaida.

Makalla ameyasema hayo alipozungumza na waandishi wa habari ofisini kwake, baada ya kumalizika kwa Kikao cha Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa.

Aidha, katika kutekeleza maelekezo ya Rais Dk. Samia Suluhu Hassan aliyoyatoa jana, CPA Makalla amewataka wamiliki wa vituo vya mafuta kufungua vituo vyao pamoja na maeneo mengine ya biashara, huku akiwataka viongozi wa serikali za mitaa na vijiji kuendelea kutimiza jukumu lao la kuhakikisha usalama unakuwepo wa kutosha katika maeneo yao, sambamba na kutoa taarifa za uvunjifu wa sheria kwa mamlaka husika.

Katika hatua nyingine, CPA Makalla amewaagiza wakurugenzi watendaji wa halmashauri zote mkoani humo chini ya usimamizi wa Katibu Tawala wa Mkoa, kuhakikisha huduma za usafi wa mazingira zinasimamiwa kikamilifu.

Previous Post

DK. SAMIA AAPISHWA JIJINI DODOMA

Next Post

RAIS DK. SAMIA APOKELEWA NA WATUMISHI IKULU

Next Post
RAIS DK. SAMIA APOKELEWA NA WATUMISHI IKULU

RAIS DK. SAMIA APOKELEWA NA WATUMISHI IKULU

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

DIARRA, LOEMBA, OURA WALIVYOTIKISA DABI YA K’KOO

DIARRA, LOEMBA, OURA WALIVYOTIKISA DABI YA K’KOO

3 months ago
DK. NCHIMBI AITEKA RORYA | WANANCHI WATHIBITISHA KUTIKI OKTOBA  29 KWA KISHINDO

DK. NCHIMBI AITEKA RORYA | WANANCHI WATHIBITISHA KUTIKI OKTOBA  29 KWA KISHINDO

9 months ago

Popular News

  • SERENGETI BOYS KILA KONA, RAIS SAMIA AWAPA MILIONI 500/-

    SERENGETI BOYS KILA KONA, RAIS SAMIA AWAPA MILIONI 500/-

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAS: UTUNZAJI MAZINGIRA AJENDA YA KIPAUMBELE KWA MKOA WA MWANZA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • UPELE UMEPATA MKUNAJI STARS

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • ‎ RAIS DK. SAMIA: POLISI MSIDHARAU TAARIFA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. MWIGULU ATETA NA WAZIRI MKUU WA CONGO BRAZZAVILLE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?