• ePaper
Thursday, April 16, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Burudani

WADAU WAMPA TANO RAIS SAMIA TUZO ZA CAF 2025

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
November 21, 2025
in Burudani, Habari, Kitaifa, Michezo
0
WADAU WAMPA TANO RAIS SAMIA TUZO ZA CAF 2025
0
SHARES
6
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na NASRA KITANA

SIKU moja baada ya kutunikiwa tuzo ya heshima na Shirikisho la Soka Afrika (CAF), wadau wa michezo nchini wamempongeza Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kwa kuipaisha Tanzania kimataifa katika sekta hiyo.

Dk. Samia, Rais wa Kenya, William Ruto na Rais wa Uganda, Yoweri Museveni walitunikiwa tuzo hizo jijini Rabat nchini Morocco katika hafla ya tuzo za CAF (CAF Awards 2025).

Watatu hao walitunukiwa tuzo hizo kutokana na nchi hizo za Afrika Mashariki kuandaa kwa mafanikio fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika kwa Wachezaji wa Ligi za Ndani (CHAN 2024), zilizofanyika Agosti mwaka huu.

Akizungumza baada ya kupokea tuzo hiyo juzi, Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Gerson Msigwa aliishukuru CAF huku akisema kwamba, Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Dk. Samia itaendelea kutoa ushirikiano kuhakikisha soka linapiga hatua.

Alisema serikali inaendelea kuboresha na kujenga viwanja vya michezo nchini ikiwemo kuendeleza programu ya soka la vijana kwa wanawake na wanaume ili kushiriki katika mashindano mbalimbali ya kimataifa.

“Kwanza tunashukuru kwa tuzo hii mliyotupatia na sapoti kubwa ambayo mmeendelea kutupa kuhakikisha tunaendeleza soka nchini, tunaahidi kutoa ushirikiano mkubwa kwa CAF na FIFA kuhakikisha mchezo wa soka unapiga hatua zaidi,’’ alisema Msigwa.

WADAU WAFUNGUKA

Wakizungumza kwa nyakati tofauti, viongozi na wadau mbalimbali wa michezo wamesema tuzo hiyo ni heshima kubwa kwa Tanzania na itaongeza chachu ya kukua kwa soka nchini.

Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Wallace Karia alisema: “Nilifurahia kuona tuzo hiyo inakwenda kwa Rais wetu Dk. Samia kwani anastahili kuipata, aliyoyafanya ni makubwa na nina imani ataendelea kufanya mengi zaidi kwa maendeleo ya soka hapa nchini,’’.

Katibu Mtendaji wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT), Neema Msitha, amempongeza Rais Samia kwa tuzo hiyo huku akisema imeonyesha ni kwa kiasi mchango wake katika soka Afrika umeonekana.

Alisema serikali chini ya Dk. Samia imefanya kazi kubwa katika michezo ambapo imejenga miundombinu mbalimbali ikiwemo viwanja vya soka na kufanikiwa kuwa mwenyeji wa michuano ya CHAN na kupata nafasi ya kuandaa AFCON 2027.

Mchezaji wa zamani wa Yanga na timu ya taifa ‘Taifa Stars’, Ally Mayay, alisema tuzo hiyo ni hatua kubwa katika soka la Tanzania kwani imeonyesha ni kwa kiasi gani nchi imepiga hatua katika soka.

 ‘’Ni furaha kwetu kwa Rais kutunikiwa tuzo hiyo na hapo ndipo inapooonyesha jinsi gani tumeendelea kisoka na kutambulika kimataifa hivyo tuendelee na kasi ya kufanya vizuri kuanzia ngazi za klabu na timu zetu za taifa,’’ alisema Mayay.

Naye nyota wa zamani wa Simba, Zamoyoni Mogella, alisema amefurahia kuona Tanzania imepiga hatua kubwa katika soka.

 ‘’Hii ni ya thamani kubwa kwetu, mpira wetu sasa umepiga hatua kubwa na Rais Samia amechangia kwa kiasi kikubwa, tunaona timu zetu za Simba na Yanga zikifanya vziuri kimataifa lakini timu ya taifa pia kuwa mwenyeji wa mashindano makubwa kiukweli tunatakiwa kujivunia katika hilo,’’ alisema.

Previous Post

FEI TOTO AAHIDI MAKUBWA CAFCC

Next Post

DK. NCHIMBI ATAJA FAIDA UKARABATI RELI TAZARA

Next Post
DK. NCHIMBI ATAJA FAIDA UKARABATI RELI TAZARA

DK. NCHIMBI ATAJA FAIDA UKARABATI RELI TAZARA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

MIILI YA WALIOFARIKI AJALI YA HELKOPTA YATAMBULIWA

MIILI YA WALIOFARIKI AJALI YA HELKOPTA YATAMBULIWA

4 months ago
SIMULIZI MAAJABU MIKOPO YA ASILIMIA 10

SIMULIZI MAAJABU MIKOPO YA ASILIMIA 10

4 months ago

Popular News

  • PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SERIKALI YAFUTA LESENI 40 ZA UTAFITI  WA MADINI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TIMU OFISI YA MAKAMU WA RAIS, WIZARA YA MAJI KUCHUANA MEI MOSI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SIMBA, FOUNTAIN GATE SIKU YA HESHIMA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. MWINYI AKAGUA MJI WA AFCON FUMBA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?