• ePaper
Friday, April 24, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Biashara

TRENI ZA JIJI DAR, DODOMA ZANUKIA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
November 24, 2025
in Biashara, Habari, Kitaifa
0
TRENI ZA JIJI DAR, DODOMA ZANUKIA
0
SHARES
14
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na ELIZBAETH JOHN

MAANDALIZI ya ujenzi wa njia za treni za mijini katika majiji ya Dar es Salaam na Dodoma yameanza rasmi, hatua inayotarajiwa kubadili kwa kiasi kikubwa mfumo wa usafiri wa abiria na kupunguza msongamano wa magari.

Akizungumza Dar es Salaam, Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo ambaye pia ni Msemaji wa Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa, alisema treni hizo zitakuwa za juu na zitaunganishwa na mtandao wa Reli ya Kisasa ya SGR.

Alisema katika jiji la Dar es Salaam, awamu ya kwanza ya ujenzi itahusisha njia itakayoanzia Kawe, Mwenge, Mlimani City, Ubungo hadi Kariakoo, ambako mtandao utaunganishwa na SGR.

Aidha, kutakuwepo na tawi jingine kutoka Bibi Titi, Morocco kupitia Barabara ya Ali Hassan Mwinyi hadi Mwenge.

Alisema serikali imepanga kila baada ya kilometa mbili kuwe na kituo, lengo likiwa ni kujenga mtandao wa kilometa 160 utakaobadili mfumo wa usafiri jijini Dar es Salaam.

“Kwa upande wa Dodoma, serikali imepanga kuanza na njia itakayotoka stesheni ya SGR kuelekea katikati ya jiji, kuendelea hadi Mtumba na Chamwino kupitia stendi mpya ya mabasi.

“Awamu inayofuata itafika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Msalato, huku mtandao mzima ukitarajiwa kuwa wa angalau kilometa 105,” alisema.

Msigwa alisema Tanzania inaendelea kusonga mbele kwa kasi katika utekelezaji wa miradi mikubwa ya kimkakati, ikiwemo SGR ambayo imeendelea kuwavutia wawekezaji kutoka mataifa mbalimbali.

Alisema kazi ya ujenzi wa SGR inaendelea vizuri katika vipande vyote vinane, kutoka Dar es Salaam, Dodoma, Tabora, Isaka, Mwanza, Kigoma hadi Burundi, huku miradi mipya ya reli ikiongezeka ukiwemo ujenzi wa reli ya Tanga-Arusha-Musoma yenye kilometa 1,028 na reli ya Mtwara-Mbambabay yenye kilometa 1,000 kwa ajili ya kusafirisha mizigo kutoka Bahari ya Hindi hadi nchi za kusini.

Alisema katika sekta ya bandari, serikali imeeleza kuongezeka kwa ufanisi wa bandari ya Dar es Salaam maradufu kufuatia ushirikiano wa kimkakati na kampuni ya DP World, hatua iliyosaidia kupunguza muda wa meli kusubiri kutoka siku 46 hadi saba.

“Uwezo wa bandari hiyo kuhudumia mizigo umeongezeka kutoka tani milioni 21 hadi tani milioni 32 ndani ya miaka mitatu, huku mapato yakipanda kutoka sh. bilioni 900 hadi sh. trilioni 1.8.

“Serikali inaendelea kuboresha Bandari za Mtwara, Tanga, Kigoma, Bagamoyo na zile za Ziwa Tanganyika, ukiwemo uzinduzi wa meli mpya ya mizigo yenye uwezo wa kubeba tani 2,000 kati ya meli nne zinazojengwa kuimarisha usafiri na biashara kuelekea Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) na masoko mengine ya ukanda huo,” alisisitiza.

Pia, katika sekta ya utalii, Msigwa alisema Tanzania imevuka lengo lake baada ya kupokea watalii milioni 5.3 mwishoni mwa mwaka jana, idadi ambayo awali ilipangwa kufikiwa mwaka huu. Serikali inalenga kufikia watalii milioni nane ifikapo mwaka 2030.

Kwa upande wa usafiri wa anga, alisema serikali imeimarisha Shirika la Ndege Tanzania (ATCL), ambalo hivi sasa lina ndege 16 na linahudumia vituo 29 vya ndani na nje ya nchi.

“Ndege nane zaidi zinatarajiwa kuongezwa kufikisha jumla 24 ifikapo mwishoni mwa mwaka huu, huku vituo vipya vya Cape Town (Afrika Kusini), Accra (Ghana) na Victoria Falls (Zimbabwe), vikitarajiwa kuongezwa  na kufikia mwaka 2030, malengo ni ATCL kuhudumia vituo 50 ndani na nje ya nchi,” alisema Msigwa.

Msemaji huyo aliongeza uchumi wa taifa unaendelea kukua kwa wastani wa asilimia sita na kwamba akiba ya fedha za kigeni imefikia dola bilioni saba za Marekani.

“Serikali inatarajia kuongeza ajira kupitia miradi yote ya kimkakati inayotekelezwa nchini, ikiwemo ya reli, bandari na sekta ya utalii,” alisema Msigwa.

Previous Post

SERIKALI YATOA TAMKO

Next Post

TUZO YA CAF KWA RAIS DK. SAMIA NI HESHIMA

Next Post
TUZO YA CAF KWA RAIS DK. SAMIA NI HESHIMA

TUZO YA CAF KWA RAIS DK. SAMIA NI HESHIMA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

WACHUMI WATAJA FAIDA 8 UJENZI RELI TAZARA

WACHUMI WATAJA FAIDA 8 UJENZI RELI TAZARA

4 months ago
KETE MUHIMU KWA TAIFA STARS AFCON

KETE MUHIMU KWA TAIFA STARS AFCON

4 months ago

Popular News

  • 4 ZAONGOZA KWA UKAME WA MABAO LIGI KUU BARA

    4 ZAONGOZA KWA UKAME WA MABAO LIGI KUU BARA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WAZIRI MKUU AWASHUKIA WACHOCHEZI MIGOGORO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • UKWELI HADHARANI TUME YA JAJI CHANDE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • YASIJIRUDIE TENA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MSD YABAINISHA DHAMIRA KUIMARISHA USHIRIKIANO NA SEKTA YA AFYA BINAFSI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?