• ePaper
Saturday, June 6, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Burudani

MASHABIKI WA MWAKINYO WATULIZWA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
December 3, 2025
in Burudani, Michezo
0
MASHABIKI WA MWAKINYO WATULIZWA
0
SHARES
10
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

AMINA KASHEBA 

KOCHA wa ngumi za kulipwa, Kanda Kabongo amewataka mashabiki wa bondia, Hassan Mwakinyo kuwa na imani naye kuelekea katika pambano la ‘Boxing On Boxing Day’.

Mwakinyo atapanda ulingoni Desemba 26, mwaka huu, ukumbi wa Superdome, Dar es Salaam katika pambano hilo ambalo mpinzani wake bado hajawekwa hadharani.

Akizungumza Dar es Salaam, Kabongo alisema asilimia kubwa ya mazoezi ya Mwakinyo yamekamilika, hivyo aliwaomba Watanzania wategemee mambo mazuri kutoka kwake.

“Mwakinyo kila siku anafanya mazoezi ndiyo maana sina wasiwasi na yeye kwa sababu mimi ndiye napanga programu nzima ya mazoezi yake.

“Pia, tumekuwa tukifanya mazoezi kabla ya kutangazwa pambano hilo kwa sababu ngumi ndiyo mchezo wake, hivyo Watanzania wategemee mambo mazuri kutoka kwa Mwakinyo,” alisema.

Kocha huyo alisema mbali ya mpinzani wake kutofahamika hadi leo, bado ana imani atapambana na b ondia mwenye uwezo mkubwa.

Mkurugenzi wa Peak time Media, Meja Selemani Semunyu ambao ni waandaji wa pambano hilo, alisema mpinzani wa Mwakinyo atafahamika muda wowote ndani ya wiki hii.

“Tupo katika upangaji wa orodha ya mabondia ambao watapanda ulingoni katika pambano la ‘Boxing On Boxing Day’, pia wiki ijayo Watanzania watafahamu mpinzani wa Mwakinyo, ambaye atakuwa (main card),”alisema.

Meja huyo aliongeza kuwa milango ya kudhamini pambano hilo, ipo wazi kwa kampuni, taasisi za umma na binafsi.

Previous Post

AZAM, SINGIDA BS UTAMU UPO HAPA

Next Post

TUMEJIPANGA

Next Post
TUMEJIPANGA

TUMEJIPANGA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

MIAKA 64 YA UHURU YAWAIBUA BAYI, RAGE

MIAKA 64 YA UHURU YAWAIBUA BAYI, RAGE

6 months ago
WASIRA : MAENDELEO YALIYOPO, UTHIBITISHO WA UONGOZI MAHIRI

WASIRA : MAENDELEO YALIYOPO, UTHIBITISHO WA UONGOZI MAHIRI

9 months ago

Popular News

  • MWANZA KINARA USIMAMIZI MAAFA

    MWANZA KINARA USIMAMIZI MAAFA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WFP KUENDELEZA USHIRIKIANO NA TANZANIA USIMAMIZI WA MAAFA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • HESHIMA KUBWA KWA TANZANIA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MWIGULU: MAMBO MAZURI YANAKUJA, AIPA TANO SERENGETI BOYS

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SERENGETI BOYS HESHIMA KILA KONA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Not enough quota to unlock this post
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?