• ePaper
Thursday, April 16, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Burudani

AZAM, SINGIDA BS UTAMU UPO HAPA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
December 3, 2025
in Burudani, Michezo
0
AZAM, SINGIDA BS UTAMU UPO HAPA
0
SHARES
6
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na NASRA KITANA

TIMU za Azam FC na Singida Black Stars leo zinatarajiwa kupambana ambapo utamu utakuwa katika takwimu.

Mchezo huo Ligi Kuu Tanzania Bara, umepangwa kutakaofanyika  katika Uwanja wa Azam Complex, Chamanzi, Dar es Salaam kuanzia saa 3:00 usiku ambapo Singida BS ina pointi saba huku Azam ikiwa na alama tano katika msimamo wa michuano hiyo.

Singida BS ipo nafasi ya 11, Azam ikiwa nafasi ya 15 katika msimamo wa ligi hiyo, baada ya timu zote mbili kushuka dimbani mara tatu tangu ligi hiyo ilipoanza.

Azam imeshinda mechi moja wakati Singida BS wao wameshinda mechi mbili katika ligi hiyo.

Lakini Azam imefunga mabao manne katika michuano hiyo huku Singida BS ikiwa imepachika mabao matatu.

Hata hivyo, timu zote mbili hazijafungwa mchezo wowote katika michuano hiyo ya msimu wa 2025/26.

Vita nyingine katika pambano la leo ni Feisal Salum ‘Fei Toto’ ambaye anaendelea kuwania kiatu cha ufungaji bora baada ya kupachika mabao mawili hadi sasa.

Kinara wa kufunga mabao hadi sasa katika ligi hiyo ni Salehe Karabaka wa timu ya JKT Tanzania ambaye amefunga mabao manne katika ligi hiyo ambapo macho ya mashabiki watataka kuona kama Feisal ataongeza idadi hiyo ya kufunga mabao.

Akizungumza kuelekea katika mchezo huo, Kocha wa Azam FC, Florent Ibenge alisema wanakwenda katika mchezo mgumu, lakini watapambana kupata ushindi.

 “Utakuwa mchezo mgumu na wenye changamoto kubwa, tunakwenda kupambana na timu bora ambayo ina wachezaji wenye kiwango bora,” alisema Ibenge.

Ibenge alisema kuwa amerekebisha mapungufu yaliyojitokeza katika mechi zilizopita ili kufanya vizuri katika michezo inayofuata ikianza na Singida Black Stars.

Mchezaji wa timu hiyo, Lusajo Mwaikenda alisema wachezaji wote wamejipanga vizuri kupambana kupata ushindi.

 “Tunajua wapinzani wetu wana wachezaji wazuri, lakini tumejipanga kucheza kwa ushirikiano mkubwa kuhakikisha tunaibuka na ushindi,” alisema.

Naye Kocha wa Singida Black Stars, Miguel Gamondi alisema kuwa wanakwenda kukutana na timu nzuri hivyo wamejipanga kupambana nayo.

 “Azam ni timu bora na ina wachezaji wazuri, nimewaona jinsi walivyokuwa wanacheza, hivyo nitaingia uwanjani kuhakikisha tunatumia mbinu mbadala ya kupata ushindi na tutafanya mashambulizi mwanzo hadi mwisho wa mchezo,” Gamondi.

Mchezaji wa Singida BS, Kennedy Juma, alisema kuwa mchezo huo ni muhimu kwao na wapo tayari kupamabana kwa dakika zote 90 kuhakikisha wanapata pointi tatu.

“Tunaingia katika mchezo mgumu, sisi kama wachezaji hatutakubali kuona tunapoteza tutapambana mwanzo mwisho ili kupata matokeo mazuri,” alisema Kennedy.

Katika msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Singida BS ipo nafasi ya 11 ikiwa na pointi saba huku Azam ikishika nafasi ya 15 ikiwa na pointi tano ambapo timu zote zimeshuka dimba mara tatu.

Previous Post

SIMBASC NJIA HII HAPA MAKUNDI KIMATAIFA

Next Post

MASHABIKI WA MWAKINYO WATULIZWA

Next Post
MASHABIKI WA MWAKINYO WATULIZWA

MASHABIKI WA MWAKINYO WATULIZWA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

CCM INAHESHIMU HAKI ZA BINADAMU – WASIRA

CCM INAHESHIMU HAKI ZA BINADAMU – WASIRA

6 months ago
STEVE NYERERE, WEMA SEPETU WAMLILIA LUKUVI

STEVE NYERERE, WEMA SEPETU WAMLILIA LUKUVI

3 weeks ago

Popular News

  • PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SERIKALI YAFUTA LESENI 40 ZA UTAFITI  WA MADINI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TIMU OFISI YA MAKAMU WA RAIS, WIZARA YA MAJI KUCHUANA MEI MOSI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SIMBA, FOUNTAIN GATE SIKU YA HESHIMA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. MWINYI AKAGUA MJI WA AFCON FUMBA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?