• ePaper
Sunday, May 31, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

TANZANIA INAENDELEA KUALIKA WAWEKEZAJI – RAIS DK. SAMIA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
December 4, 2025
in Habari, Kimataifa, Kitaifa
0
TANZANIA INAENDELEA KUALIKA WAWEKEZAJI – RAIS DK. SAMIA
0
SHARES
10
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na MWANDISHI WETU

RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, ameihakikishia Jumuiya ya Kimataifa kuwa, serikali imefungua milango kwa wawekezaji wenye nia ya kushirikiana na Tanzania katika kusukuma mbele ajenda ya maendeleo ya taifa.

Amesema kuwa, kwa zaidi ya miongo sita, Tanzania imeendeleza ushirikiano thabiti na wawekezaji na wadau wa maendeleo, huku ikiimarisha mazingira ya uwekezaji na kufanya biashara.

Rais Dk. Samia, alieleza hayo, alipokutana na kufanya mazungumzo na Naibu Mwenyekiti wa Biashara wa Jumuiya ya Madola na Baraza la Uwekezaji (CWEIC), Lord Hugo Swire, Ikulu jijini Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa taarifa ya Ikulu kwa vyombo vya habari iliyotolewa jana, viongozi hao, walijadiliana kuhusu kuanzisha ushirikiano wa kibiashara na fursa za uwekezaji, zinazoweza kuchochea ukuaji wa uchumi na ajira nchini.

Rais Dk. Samia, alieleza kuwa serikali imefungua milango kwa wawekezaji wenye nia ya kushirikiana na Tanzania, kusukuma mbele ajenda ya maendeleo ya taifa na kuongeza kuwa, kwa zaidi ya miongo sita, nchi imeendeleza ushirikiano thabiti na wawekezaji pamoja na wadau wa maendeleo, huku ikiimarisha mazingira ya uwekezaji na kufanya biashara.

Akigusia matukio ya uvunjifu wa amani ya Oktoba 29, mwaka huu, Rais Samia, alisisitiza Tanzania inaendelea kuwa nchi yenye utulivu na ina mifumo madhubuti ya kushughulikia masuala yake ya ndani.

Aidha, aliihakikishia jumuiya ya wawekezaji kuwa, serikali itaendelea kuwajibika kwa usalama wa wawekezaji na biashara zao na kudokeza kuwa, nchi ipo katika hatua za awali za mchakato wa mapitio ya katiba unaokusudiwa kuimarisha utendaji wa taasisi na sekta ya biashara na uwekezaji.

Kwa upande wake, Lord Swire alionesha utayari wa CWEIC kuendeleza ushirikiano na Tanzania kama mshirika wa kimkakati kuvutia wawekezaji zaidi kutoka nchi wanachama wa Jumuiya ya Madola.

Pia, alimshukuru Rais Dk. Samia kwa mapokezi na kumtakia kheri katika kuendeleza juhudi za kuimarisha uchumi wa nchi, huku akiiombea Tanzania kurejea katika hali ya utulivu.

Previous Post

KETE YA KWANZA MUHIMU KWA MATOLA SIMBA SC

Next Post

TANZANIA YATAJWA KINARA AFRIKA MAPAMBANO USUGU WA VIMELEA

Next Post
TANZANIA YATAJWA KINARA AFRIKA MAPAMBANO USUGU WA VIMELEA

TANZANIA YATAJWA KINARA AFRIKA MAPAMBANO USUGU WA VIMELEA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

MTWARA KUCHELE! NCHIMBI AAHIDI MAMBO MAKUBWA

MTWARA KUCHELE! NCHIMBI AAHIDI MAMBO MAKUBWA

8 months ago
MWINYI AFICHUA SIRI UUNDAJI SERIKALI YA UMOJA KITAIFA

MWINYI AFICHUA SIRI UUNDAJI SERIKALI YA UMOJA KITAIFA

8 months ago

Popular News

  • SERENGETI BOYS KILA KONA, RAIS SAMIA AWAPA MILIONI 500/-

    SERENGETI BOYS KILA KONA, RAIS SAMIA AWAPA MILIONI 500/-

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAS: UTUNZAJI MAZINGIRA AJENDA YA KIPAUMBELE KWA MKOA WA MWANZA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • UPELE UMEPATA MKUNAJI STARS

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • ‎ RAIS DK. SAMIA: POLISI MSIDHARAU TAARIFA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. MWIGULU ATETA NA WAZIRI MKUU WA CONGO BRAZZAVILLE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?