• ePaper
Thursday, April 16, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Burudani

AZAM FC YAIZAMISHA SIMBASC

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
December 8, 2025
in Burudani, Michezo
0
AZAM FC YAIZAMISHA SIMBASC
0
SHARES
3
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na MWANDISHI WETU

TIMU ya Azam FC, iliizamisha Simba baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 2-0, katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara, uliofanyika Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam.

Mchezo huo, ulianza kwa kasi pande zote ambapo kila timu ikitaka bao la mapema kujiweka katika mazingira mazuri.

Katika dakika ya saba, mchezaji wa Simba, Joshua Mutale alishindwa kuitumia nafasi aliyoipata baada ya shuti lake kupaa juu nje ya lango, kabla ya Elie Mpanzu kufumua shuti kali lililogonga mwamba.

Azam FC walijibu shambulizi katika dakika ya 15, Iddy Selemani alipiga shuti kipa wa Simba, Yakoub Suleiman akapangua ikawa kona ambayo haikuzaa matunda.

Dakika ya 20, Simba walifanya shambulizi jingine lakini umakini mdogo wa Anthony Mligo alishindwa kukwamisha mpira wavuni akiwa eneo la hatari, mpira ukatoka nje ya lango.

Kipa wa Azam, Zubery Foba alionekana kufanya kazi ya ziada katika dakika ya 34, baada ya kuokoa shuti la Mpanzu.

Katika dakika ya 45, Simba nusura wapate bao la kuongoza ambapo Stephen Mukwala alipiga shuti likatoka sentimeta chache nje ya lango, hadi mapumziko ya kipindi cha kwanza timu hizo zilitoka zikiwa suluhu.

Kipindi cha pili kilianza kwa Simba kulishambulia lango la Azam, dakika ya 46 Mpanzu alikosa utulivu ambapo shuti lake lilitoka nje kabla ya Selemani Mwalimu kurudia kosa dakika ya 70.

Azam ilionekana ikilishambulia lango la Simba kama nyuki, dakika ya 81, Japhet Kitambala alipachika bao la kuongoza baada ya kuunganisha krosi iliyochongwa na Nassor Saadun na kuujaza mpira wavuni.

Katika dakika ya 88, Azam ilipata bao la pili lililowekwa kimiani na Iddy Selemani kufuatia kazi nzuri iliyofanywa na Saadun na mpira kujaa kimiani moja kwa moja.

Simba alijibu shambulizi dakika ya 90 lakini Kibu Denis alishindwa kuitumia vyema nafasi hiyo baada ya kuingia na mpira eneo la hatari kipa wa Azam akaokoa hatari hiyo langoni mwake, hadi mchezo unamalizika, Azam iliibuka na ushindi wa mabao 2-0.

Kufuatia ushindi huo, katika msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Azam imepanda hadi nafasi ya tisa ikijikusanyia pointi tisa huku Simba ikibakia nafasi ya tano kwa pointi 12 kabla ya mechi ya jana kati ya Yanga na Coastal Union.

Simba: Yakoub Suleiman, Shomari Kapombe, Karabou Chamou/Jonathan Sowah, Steven Mukwala/Selemani Mwalimu, Anthony Mligo, Kante Alasane, Joshua Mutale/Kibu Denis, Morice Abraham, Yusuph Kagoma, Wilson Nagu na Elie Mpanzu.

Azam FC: Zuberi Foba, Lusajo Mwaikenda, Yoro Diaby, Landry Zouzou, Feisal Salum, Sadio Kanoute/ Nassor Saadun, Zidane Sereri/ James Akaminko, Idd Selemani. Pascal Msindo, Himid Mao na Japhet Kitambala.

Previous Post

KIHONGOSI: TANZANIA HAIWEZI KURUDI UKOLONI

Next Post

AMANI YAWAIBUA WABUNGE

Next Post
AMANI YAWAIBUA WABUNGE

AMANI YAWAIBUA WABUNGE

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

YANGA, DODOMA JIJI KITAELEWEKA LEO

YANGA, DODOMA JIJI KITAELEWEKA LEO

3 months ago
IBENGE ALIA NA WASHAMBULIAJI

IBENGE ALIA NA WASHAMBULIAJI

4 months ago

Popular News

  • MAFANIKIO YA KISHINDO SGR

    MAFANIKIO YA KISHINDO SGR

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • NYAMBUI AFUNGUKAAMANI KATIKA MICHEZO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • YANGA, MBEYA CITY KAZI IPO LEO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. MWINYI AFICHUA KUWA NA KIPAJI CHA SOKA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?