• ePaper
Thursday, April 30, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Burudani

TRA UNITED KAZI KAZI

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
December 16, 2025
in Burudani, Michezo
0
TRA UNITED KAZI KAZI
0
SHARES
6
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na AMINA KASHEBA

TIMU ya soka ya TRA United chini ya Kocha Etiene Ndayiragije kesho itaanza mazoezi ya kujiandaa kwa mechi mbalimbali ikiwemo Ligi Kuu Tanzania Bara.

Akizungumza na UHURU, Ofisa Habari wa klabu hiyo, Christina Mwagala, amesema baada Ligi Kuu Tanzania Bara kusimama kupisha michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON), kikosi chao kitatumia muda huo kujiandaa vyema.

Amesema wachezaji walipewa mapumziko ya siku 10 na sasa wanarejea mazoezi kujiandaa vizuri kwa Ligi Kuu pamoja na Kombe la Shirikisho.

“Baada ya mapumziko ya siku 10 wachezaji wanaingia kambini Jumatano (kesho), ambapo mazoezi rasmi yamepangwa kuanza keshokutwa mkoani Tabora, kuhusu tetesi  juu ya kusaka saini ya mchezaji wa Yanga, Denis Nkane na kuachana na Emmanuel Mwanengo, hivi sasa siwezi kuongea maana hizo ni tetesi.

“Uongozi utasema kila kitu ni wachezaji gani tumesajili na wangapi tumeachana nao, lakini siyo hivi sasa maana katika usajili kila kitu kinaongelewa sio hapa nchini hadi nje ya nchi sio jambo la ajabu,” amesema.

Msemaji huyo amesema hivi sasa kikosi chao kimeimarishwa zaidi baada ya uwepo wa kocha, Ndayiragije katika kikosi hicho.

“Hivi sasa timu yetu imeimarika kwa kiwango kikubwa tuna imani wachezaji watakuwa bora zaidi, mashabiki wategemee mambo mazuri kwani tunakuja kufanya vitu vikubwa zaidi,” amesema.

Katika Ligi Kuu Bara, TRA United ipo nafasi ya 10 ikiwa na alama tisa katika mechi saba.

Previous Post

BONDIA MWAKYEMBE AMKUBALI MMALAWI

Next Post

KIPA NIGERIA ASHUSHA PRESHA

Next Post
KIPA NIGERIA ASHUSHA PRESHA

KIPA NIGERIA ASHUSHA PRESHA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

RONALDO KUTUNDIKA DALUGA

RONALDO KUTUNDIKA DALUGA

6 months ago
KETE MUHIMU KWA YANGA LEO

KETE MUHIMU KWA YANGA LEO

5 months ago

Popular News

  • TANZANIA YAJINADI KIMATAIFA MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

    TANZANIA YAJINADI KIMATAIFA MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • VYALENGA KUIJENGA JAMII KIUCHUMI NA KIROHO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • KUVUMILIANA MUHIMU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WAZIRI SANGU ABAINISHA HIFADHI SKIMU INAVYOENDA KUBADILI MAISHA YA WATANZANIA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TUCTA: WAAJILI WATEKELEZE NYONGEZA YA KIMA CHA MISHAHARA SEKTA BINAFSI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?