Na AMINA KASHEBA
BONDIA wa ngumi za kulipwa, Mtanzania Hassan Mwakinyo, leo atawaongoza mabondia wenzake k upima wa uzito kwa ajili ya pambano la ‘Boxing On Boxing Day’.
Mwakinyo atapanda ulingoni kuzichapa na Stanley Eribo kutoka Nigeria kesho katika pambano lisilo la ubingwa, raundi 10, uzito wa kati litakalofanyika katika Ukumbi wa Warehouse jijini Dar es Salaam.
Akizungumza Dar es Salaam jana, Mkurugenzi wa Kampuni ya Peaktime Promotion, Meja Selemani Semunyu alisema mabondia wote kutoka nje ya nchi wameshafika na leo kutakuwa na upimaji uzito kuhakikisha uwepo wa mtanange huo.
Alisema maandalizi ya pambano hilo yamefikia hatua za mwisho hivyo mabondia wamejipanga vyema kutoa burudani nzuri kwa watanzania amboa watajitokea katika matanange huo.
“Zoezi la upimaji uzito litafanyika katika Ukumbi wa Warehouse ambapo pambano hilo litafanyika, wito wetu kwa wadau kujitokeza kwani siku zote wamekuwa bega kwa bega na sisi katika kuhakikisha vijana wanafikia malengo yao,” alisema Semunyu.
Semunyu alisema pambano hilo litakuwa la historia kutokana na aina ya mapambano ambayo mabondia watacheza kuwa na rekodi nzuri ulingoni na katika mtandao wa ngumi boxrec.




