• ePaper
Sunday, July 26, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Burudani

MBEUMO FURAHA TELE

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
December 25, 2025
in Burudani, Michezo
0
MBEUMO FURAHA TELE

Bryan Mbeumo

0
SHARES
8
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

AGADIR, Morocco

STAA wa timu ya taifa ya Cameroon, Bryan Mbeumo amesema anafurahia kucheza michuano ya Mataifa ya Afrika (AFCON 2025), msimu huu nchini Morocco.

Alisisitiza kuwa ana furaha tele kucheza michuano ya msimu huu baada ya kuzikosa fainali za msimu uliopita zilizofanyikia Ivory Coast kutokana na majeraha yaliyokuwa yakimkabili.

Akizungumza, staa huyo anayekipiga katika kikosi cha Manchester United, alisema hiyo ni fursa ya aina yake kuhakikisha anaisaidia timu ya Cameroon kufanya vizuri katika michuano ya AFCON 2025.

“Nina msisimko mkubwa kucheza michuano ya AFCON 2025, niliisubiri kwa muda mrefu na nina furaha kuwa mmoja wa wachezaji wa kuitumikia timu yangu ya taifa katika msimu huu,” alisema Mbeumo.

Mchezaji huyo wa zamani wa Brentford tayari alishacheza michuano ya Kombe la Dunia msimu uliopita iliyofanyikia Quatar akiwa na Cameroon.

“Hii ni sehemu ya kujivunia kwa Afrika kwani hata familia yangu inanifuatilia jinsi ninavyocheza katika michuano ya AFCON, ni heshima ya aina yake na ni kitu pekee katika maisha yangu.

“Kwangu sina presha kwani mipango niliyonayo ni kuisaidia timu kufanya vyema na kufika mbali zaidi katika michuano ya msimu huu ikiwemo kuweka historia,” alisema.

Katika michuano ya AFCON 2025, Cameroon imepangwa kundi F ikiwa na timu za Ivory Coast, Gabon na Msumbiji.

Staa huyo alishafunga mabao sita katika mechi 16 alizocheza Ligi Kuu ya England ndani ya Manchester United.

(BBC)

Previous Post

MWAKINYO KUPIMA UZITO LEO

Next Post

BOUANGA MATUMAINI KIBAO

Next Post
BOUANGA MATUMAINI KIBAO

BOUANGA MATUMAINI KIBAO

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

RAIS DK. SAMIA AWATAKIA HERI WATANZANIA MIAKA 64 YA UHURU

RAIS DK. SAMIA AWATAKIA HERI WATANZANIA MIAKA 64 YA UHURU

8 months ago
WENYE UMRI HUU HATARINI KUPATA PRESHA YA MACHO

WENYE UMRI HUU HATARINI KUPATA PRESHA YA MACHO

5 months ago

Popular News

  • KATIBA MSINGI WA HAKI – DK. NCHIMBI

    KATIBA MSINGI WA HAKI – DK. NCHIMBI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MABASI YA UMEME REKODI ZANZIBAR

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • KOCHA AIPA JEURI YANGA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MWALIMU, GUEYE WAPO SIMBA SANA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WAZIRI ASHTUKIA ‘USANII’ WA WACHIMBAJI MADINI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Not enough quota to unlock this post
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?