• ePaper
Thursday, June 18, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Makala

HOFU YA WANAUME KUOA WANAWAKE WAREMBO IKO HAPA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
January 5, 2026
in Makala, MAKALA BURUDANI
0
HOFU YA WANAUME KUOA WANAWAKE WAREMBO IKO HAPA
0
SHARES
28
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na ZIANA BAKARI

BAADHI ya wataalamu wa saikolojia, wametaja mambo matatu yanayosababisha idadi kubwa ya wanaume, kuwa na hofu ya kuoa wanawake warembo katika jamii.

Mambo hayo matatu yaliyotajwa na wataalamu hao wa saikolojia ni athari za kisaikolojia, kijamii na kimtazamo ambazo husababisha wanaume kuwa na hofu.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti na UHURU, wanasaikolojia hao, walisema mwanaume anapaswa kujiamini anapotaka kuoa mwanamke mwenye mwonekano wa kuvutia katika jamii.

Katibu Mkuu Msaidizi wa Chama cha Wanasaikolojia Tanzania (TAPA), Albano Michael, alisema sababu za kisaikolojia zinatokana na mwanaume kutojiamini kupitia malezi na makuzi aliyowahi kupata nazo huchangia.

Alisema baadhi ya wanaume hujihisi kutokuwa na sifa ya kuoa mwanamke mwenye mwonekano wa kuvutia, kutokana na dhana binafsi na kuhisi hataweza kutoa huduma ipasavyo kutokana na mwonekano wake.

Alisema hali hiyo wakati mwingine, hutokana na historia ya nyuma ya mwanaume ambaye huenda aliwahi kukataliwa na wanawake wengi wenye mwonekano wa kuvutia.

Akizungumzia sababu za kijamii, Michael alisema sababu hizo, zinatokana na mazoea ya baadhi ya dhana zilizojengeka ndani ya jamii, mwanamke mwenye mwonekano wa kuvutia, hatadumu katika ndoa, jambo ambalo halina ukweli.

“Zipo baadhi ya jamii zinahisi kuoa mwanamke mwenye mwonekano wa kuvutia huaribu ndoa, kwa sababu, atawavutia wanaume wengi na kusababisha migogoro ya mara kwa mara, mwanaume hupata hofu na kuhisi kumpoteza mwanamke huyo,”alisema.

Pia, alisema sababu za kimtazamo binafsi, zinatokana na baadhi ya wanaume wanahisi wakioa wanawake wenye mwonekano wa kuvutia, watakuwa wasaliti kutokana na mvuto wao, hivyo hujawa hofu ya kuachwa, kujishusha thamani na kuona hawana vigezo vya kuwa nao katika ndoa.

“Wanaume wanapaswa kujua kuwa, mwanamke anatakiwa kuwa na tabia njema, nidhamu binafsi, mshirika mzuri wa mambo ya jamii na mwenye mtazamo chanya katika maisha, siyo mvuto pekee, hivyo, niwaombe wanaume, kuzingatia vigezo vilivyotajwa, wasiogope kuoa mwanamke mwenye mwonekano wa kuvutia kwa sababu, huongeza ladha ya upendo ndani ya ndoa,”alisema.

Mwenyekiti wa Kamati Endelevu ya Taaluma kutoka TAPA, Jesusa Malewo, aliwasihi wanaotaka kuoa kujua kuna suala la kuvumilia haiba ya mtu.

Kwa upande wake, Mhadhiri wa Saikolojia wa Chuo Kikuu cha Tumaini Dar es Salaam (DarTU), Dk. Hyasinta Kessy, alisema jambo muhimu kwa wanaume ni kuzingatia tabia njema, siyo mwonekano wa mwanamke.

Alisema haijalishi mwanamke au mwanaume ana mwonekano gani, jambo muhimu ni kuzingatia mtu mwenye tabia njema.

“Kipindi cha uchumba kinasaidia sana kusomana tabia na kujua namna ya kuishi na uliyemkusudia kumuoa, niwaombe tuzingatie sana tabia kwa sababu ni jambo muhimu na linapaswa kupewa kipaumbele,” alisema.

Previous Post

WAJUE WAKALI WA MABAO AFCON 2025

Next Post

‘PENALTI’ STARS YAIGAWA DUNIA

Next Post
‘PENALTI’ STARS YAIGAWA DUNIA

‘PENALTI’ STARS YAIGAWA DUNIA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

KIHONGOSI AFICHUA SIRI MIKUTANO YA MGOMBEA URAIS CCM ‘KUFURIKA’

KIHONGOSI AFICHUA SIRI MIKUTANO YA MGOMBEA URAIS CCM ‘KUFURIKA’

10 months ago
DK. KIKWETE ASHIRIKI MAZISHI YA KITAIFA YA RAIS MSTAAFU MOGAE WA BOTSWANA, AKIMWAKILISHA RAIS DK. SAMIA

DK. KIKWETE ASHIRIKI MAZISHI YA KITAIFA YA RAIS MSTAAFU MOGAE WA BOTSWANA, AKIMWAKILISHA RAIS DK. SAMIA

1 month ago

Popular News

  • WABUNGE: AMANI ISICHEZEWE

    WABUNGE: AMANI ISICHEZEWE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WABUNGE WAIPONGEZA NSSF NA PSSSF KWA KUANZISHA SKIMU YA HIFADHI KWA WALIOJIAJIRI NA UWEKEZAJI WA KIWANDA CHA NGOZI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WABUNGE WAPONGEZA UWEKEZAJI KLICL

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WAKAGUZI WA CAF WARIDHISHWA NA MAENDELEO YA VIWANJA VYA AFCON 2027

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MKAKATI KUDHIBITI VIFO WAJAWAZITO WAANIKWA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Not enough quota to unlock this post
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?