• ePaper
Wednesday, March 18, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

DK. MIGIRO AJA KIVINGINE CCM

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
January 8, 2026
in Habari, Kitaifa
0
DK. MIGIRO AJA KIVINGINE CCM

KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Balozi Dk. Asha- Rose Migiro

0
SHARES
6
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na IRENE MWASOMOLA

KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Balozi Dk. Asha- Rose Migiro, amekuja kivingine kuhakikisha wanachama wanashiriki usimamizi wa miradi mbalimbali ya maendeleo.

Ametumia kaulimbiu; ‘Shina lako linakuita,’ akitaka kila mwanachama kushiriki kusimamia miradi ya maendeleo ngazi ya mashina.

Amesema kuwa, mashina ndiyo chimbuko la uhai wa Chama kupima utekelezaji wa kazi za serikali zinazofanyika kuanzia ngazi za chini.

Dk. Migiro aliyasema hayo jijini Dar es Salaam, alipozungumza na mabalozi wa mashina na wanachama wa CCM, katika Wilaya za Temeke na Kigamboni, ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya siku tatu.

Alisema mabalozi ni watu muhimu katika usimamizi wa miradi kuanzia chini, hivyo ni vyema wakapewa ushirikiano na viongozi wengine kuanzia ngazi ya tawi hadi mkoa.

Pia, aliwataka viongozi wa mashina, kushirikiana na madiwani kufuatilia miradi inayotekelezwa na vitega uchumi vya Chama.

“Viongozi wa ngazi za wilaya na maeneo mengine tukiwa kwenye mashina, lazima tushiriki katika vikao, viongozi wa mashina, matawi na kata, tuwe madhubuti kuwavuta viongozi wenzetu washiriki mikutano na utatuzi wa yale tunayopitia katika mashina na matawi yetu,” alisema.

Dk. Migiro, alisema maelekezo ya Mwenyekiti wa CCM, Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, kwa viongozi wa Chama ni kuzingatia utaratibu wa kufanya vikao kwa mujibu wa kanuni na utaratibu za Chama.

“Tuzingatie kanuni za Chama tujitahidi kufanya vikao vyetu kama tunavyotakiwa kwa mujibu wa kanuni na utaratibu wetu wa CCM, kupitia vikao, tutakuwa tunapima utekelelezaji wa kazi za serikali na uimara wa Chama Cha Mapinduzi,”alisema.

Alisema dhamira ya Rais Samia ni kuhakikisha Chama kinakuwa madhubuti kuanzia ngazi ya shina.

Vilevile, aliwataka wanachama wa CCM, kutumia wazee waliopo ndani ya Chama kupata maarifa na ujuzi wa kukijenga Chama.

“Katika ujenzi wa Chama chetu, tuna wakereketwa wengi, tuwatumie kukijenga Chama,”aliongeza Balozi Dk. Migiro.

Balozi Dk. Migiro, aliwataka wanachama wa CCM, kuendelea kusimamia utekelezaji wa Ilani, kusoma na kufuatilia kwa karibu vitabu vidogo vya Ilani vilivyotolewa maeneo mbalimbali katika kipindi cha kampeni kabla ya kufanyika uchaguzi Mkuu Oktoba 29, mwaka jana.

Aliwataka viongozi wa mashina, kuhakikisha wanaendelea kuwaeleza wananchi mambo mazuri yanayofanywa na Chama katika kuwaletea maendeleo wananchi.

Dk. Migiro, alisema ni muhimu viongozi wa shina na ngazi zingine, kufanya kazi kwa kuzingatia utu wa Mtanzania.

Chama kilitumia kaulimbiu yake ya ‘Kazi na Utu Tunasonga Mbele’ wakati wa kampeni ya chaguzi mkuu ambapo CCM ilipata ushindi wa kishindo.

Pia, Balozi Dk. Migiro, wakati wa kampeni, alikuwa na kinogesho akisema; ‘Samia eeeh..Samia rahaaa’.

KAULI YA MNEC DAR

Kaimu Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (MNEC), Juma Simba, alimpongeza Dk. Migiro kuanza ziara yake mkoani humo na dhamira ya kukutana na wajumbe wa mashina.

Alisema kwamba, ziara hiyo, ina lengo la kuendelea kukijenga Chama.

Balozi wa Shina namba nne Temeke, Abdu Bilali, alimshukuru Balozi Dk. Migiro kwa kuona umuhimu wa kuzungumza nao.

RC CHALAMILA

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila, alisema serikali chini ya CCM, inaendelea na utekelezaji wa miradi mbalimbali, ikiwemo ya barabara, ambayo inalenga kumaliza changamoto ya foleni kwa wakazi wa jiji hilo.

Alitaja baadhi ya miradi hiyo ni ujenzi wa Daraja la Jangwani linalogharimu zaidi ya sh. bilioni sita, Daraja la Mzinga sh. bilioni 54 na Daraja la Mkwajuni sh. bilioni 11.

Ziara ya Balozi Dk. Migiro inatarajiwa kuendelea kesho na Januari 13 katika majimbo ya Ubungo, Kibamba na Kinondoni.

Previous Post

BARKER, IBENGE VITA YA MBINU ‘MZIZIMA DERBY’

Next Post

DK. SAMIA ATEUA, ATENGUA VIGOGO

Next Post
DK. SAMIA ATEUA, ATENGUA VIGOGO

DK. SAMIA ATEUA, ATENGUA VIGOGO

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

WAZIRI KAIRUKI ASISITIZA MAPINDUZI MAKUBWA SEKTA YA MAWASILIANO

WAZIRI KAIRUKI ASISITIZA MAPINDUZI MAKUBWA SEKTA YA MAWASILIANO

5 days ago
UKWASI MIFUKO HIFADHI YA JAMII NCHINI, WAPAA

UKWASI MIFUKO HIFADHI YA JAMII NCHINI, WAPAA

1 month ago

Popular News

  • MANDONGA AJA KIVINGINE

    MANDONGA AJA KIVINGINE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SERIKALI YATUMIA BILIONI 64/- KUBORESHA UWANJA WA NDEGE IRINGA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MWIGULU AWAWEKA MTEGONI VIGOGO WILAYA, HALMASHAURI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • ALAMA TATU KUMUENZI JPM

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SERIKALI KUIFANYA TANZANIA KITOVU CHA BIASHARA – DK. YONAZI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?