• ePaper
Sunday, March 15, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

RAIS DK. SAMIA ATAJA SABABU MABADILIKO BARAZA LA MAWAZIRI

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
January 10, 2026
in Habari, Kitaifa
0
RAIS DK. SAMIA ATAJA SABABU MABADILIKO BARAZA LA MAWAZIRI
0
SHARES
6
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na MWANDISHI WETU

RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan ametaja sababu za kufanya mabadiliko ya Baraza la Mawaziri hususan kumbadilishia majukumu Waziri Profesa Palamagamba Kabudi amsaidie kipindi hiki kuendana na mabadiliko ya siasa za dunia zenye mtazamo chanya na hasi kwa Tanzania.

Pia, amewateua Makamu wa Rais Mstaafu Dk. Philip Mpango kuwa mshauri katika Uchumi na Miradi na Waziri Mkuu mstaafu, Kassim Majaliwa kuwa mshauri wake mambo ya jamii.

Rais Dk. Samia aliyasema hayo jana Ikulu jijini Dar es Salaam, alipokuwa akizungumza na wanamichezo mbalimbali wakiwemo wachezaji wa Taifa Stars kuwapongeza kwa kufanya vizuri katika mashindano ya AFCON yaliyofanyika nchini Morocco.

“Jambo lingine ambalo limeingia katika shughuli ya leo ni kumuaga Profesa Palamagamba Kabudi kutoka Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo na kuja kwangu Ikulu . Imekuwa mapema kubadilisha kwasababu ya kwendana na siasa za dunia zinavyokwenda zenye mtazamo chanya na hasi  kwa Tanzania.

“Pale Ikulu, nahitaji akili iliyopevuka yenye maarifa mapana, uzoefu mkubwa na mtu ambaye yuko vizuri katika kujieleza na kueleza jambo likaeleweka. Nimepiga picha serikalini kwangu kote, nikasema Profesa Kabudi atanifaa, hivyo wale washauri wangu wengine wanahitaji mtu mtulivu atakayeweza kudili nao,”alisema.

Ameeleza kuwa, viongozi wengine ambao ni wa umri wa watoto wake wanaweza wasiwe na majibu mazuri lakini kwa uwezo wa Profesa Kabudi, anaweza kufanya vizuri katika nafasi hiyo. “Kwahiyo hizo ndiyo sababu zilizosababisha nimchague Profesa Kabudi aje ofisini kwangu Ikulu anisaidie kazi,”alieleza.

Vile vile Rais Dk. Samia amesisitiza umoja na mshikamano kwa Taifa kuendeleza uzalendo ambao ni msingi wa maendeleo nchini.

Pia, ameipongeza Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kazi kubwa ambayo wameendelea kuifanya vizuri katika nyanja za kimataifa na kupata vikombe vitano huku akipokea vikombe vitatu kikiwemo cha Tanzania kuwa nchi bora kwa Utalii Afrika na Duniani na kingine cha hifadhi ya Serengeti, kingine ni Zanzibar kutambulika kuwa sehemu nzuri ya mikutano ya utalii na Hoteli bora ya Utalii Tanzania ikiwa ni sifa nzuri kwa Taifa.

Kuhusu amani,  Rais Dk. Samia amesisitiza “Kwa wale wanaotaka kutuvurugia kuchafua sifa yetu washindwe na walegee, Tanzania itaendelea kuwa kitovu cha amani, haya tuliyoshinda tuendelee kushinda hata huko mbele,”alisisitiza.

Awali,  Waziri Profesa  Kabudi amesisitiza uzalendo wa kulipenda Taifa na kuimarisha maadili mema ya Kitanzania.

Amempongeza Rais Dk. Samia kwa kuongoza vyema na kuliunganisha taifa kupitia farsafa yake ya 4R ambayo imekuwa na tija kubwa kuwaunganisha watanzania na kuchochea maendeleo.

Amesema watanzania wazalendo wanasisitiza umoja wa kitanzania siyo mbadala wake, kuiheshimu Tanzania kama mama kwani hakuna nyingine.

Previous Post

DIAMOND KUTOKA KIVINGINE

Next Post

TUMEJIPANGA AFCON 2027

Next Post
TUMEJIPANGA AFCON 2027

TUMEJIPANGA AFCON 2027

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

DK. SAMIA AAHIDI WAKULIMA DAWA YA KUPULIZIA MIKOROSHO BILA MALIPO

DK. SAMIA AAHIDI WAKULIMA DAWA YA KUPULIZIA MIKOROSHO BILA MALIPO

6 months ago
HOFU YA WANAUME KUOA WANAWAKE WAREMBO IKO HAPA

HOFU YA WANAUME KUOA WANAWAKE WAREMBO IKO HAPA

2 months ago

Popular News

  • DK. MWIGULU AKERWA MICHANGO SHULENI

    DK. MWIGULU AKERWA MICHANGO SHULENI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. SAMIA AWALILIA WATUMISHI WALIOFARIKI AJALI YA BOTI KIGOMA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WATANZANIA SABA WAWASILI NCHINI KUTOKEA IRAN

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • ZIARA YA KIHONGOSI MWANZA YAREJESHA MATUMAINI KWA WANANCHI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • IBENGE FURAHA TELE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?