• ePaper
Thursday, April 30, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

RAIS DK. SAMIA AHIMIZA AMANI, MSHIKAMANO

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
January 13, 2026
in Habari, Kitaifa
0
RAIS DK. SAMIA AHIMIZA AMANI, MSHIKAMANO
0
SHARES
1
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na ATHNATH MKIRAMWENI

RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, ametoa ujumbe mzito wa mshikamano na matumaini kwa wananchi wa Zanzibar na Watanzania wote katika maadhimisho ya miaka 62 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.

Amesisitiza Mapinduzi hayo, yameendelea kuwa nguzo ya kujenga jamii ya watu huru, yenye utu na maendeleo.

Amesema kuwa, maadhimisho hayo ni kumbukumbu ya historia muhimu na dira ya mustakabali wa Taifa.

Akitoa salamu za maadhimisho hayo kupitia ukurasa wake wa mtandao wa kijamii, Rais Dk. Samia, alisema kwa kipindi cha miaka 62, dhamira ya msingi ya Mapinduzi, imeendelea kulenga katika kujenga jamii inayozingatia misingi ya umoja, haki, amani na mshikamano.

Alieleza kuwa, tunu hizo zimeiwezesha Zanzibar kudumisha utulivu wa kijamii na kuendelea kupiga hatua za maendeleo katika nyanja mbalimbali.

Rais Dk. Samia, alisisitiza kuwa, mafanikio yaliyopatikana ni matokeo ya kulindwa misingi ya Mapinduzi iliyoasisiwa na waasisi wake.

Alisema tunu za Mapinduzi, zimeendelea kuwa dira ya uongozi na mshikamano wa wananchi, ndiyo msingi wa kuimarisha utu na usawa katika jamii.

Vilevile, Rais Samia, aliwataka wananchi kuendelea kubeba dhamana ya kulinda na kuendeleza tunu hizo kwa vitendo.

Alisisitiza kila kizazi kina wajibu wa kuzirithisha tunu za Mapinduzi kwa vizazi vijavyo, kulinda amani, umoja na maendeleo ya Zanzibar na Taifa kwa ujumla.

“Ninawatakia nyote kheri katika maadhimisho ya miaka 62 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar. Kwa miaka 62, tumeendeleza dhamira ya msingi ya Mapinduzi ya kujenga jamii ya watu huru, yenye utu, yenye maendeleo, umoja, haki, amani na mshikamano.

“Sote tunao wajibu wa kuendelea kuzilinda tunu hizi na kuzirithisha kwa vizazi vijavyo, kama tulivyorithi kutoka kwa waasisi wetu,” alisema Rais Dk. Samia.

MAKAMU WA RAIS

Kwa upande wake, Makamu wa Rais Balozi, Dk. Emmanuel Nchimbi, naye alituma salamu za Mapinduzi kwa kuwatakia Watanzania wote kheri ya kumbukizi ya Siku ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.

Alisema siku hiyo ni ya kihistoria, inapaswa kutumika kama fursa ya kutafakari misingi na thamani ya Mapinduzi hayo kwa Taifa.

Balozi Dk. Nchimbi, alisisitiza kuwa, Mapinduzi yanapaswa kuenziwa siyo kwa kufanya kazi kwa bidii pekee, bali kwa kuoanisha kazi hizo na utu.

Alieleza kuwa, kufanya hivyo, Taifa litaendelea kusonga mbele kwa mshikamano, huku likijenga jamii yenye tabasamu la utu na maelewano.

Aidha, Makamu wa Rais, aliwataka wananchi kusherehekea kumbukizi hizo kwa amani na utulivu.

Pia, aliwahimiza Watanzania kuendelea kuulinda na kuudumisha Muungano wa Tanzania, huku akisisitiza mshikamano wa kitaifa ni nguzo muhimu ya maendeleo na ustawi wa nchi.

“Ninaungana na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Samia Suluhu Hassan, kuwatakia Watanzania wote kheri ya kumbukizi ya Siku ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.

“Tuyakumbuke na kuyaenzi Mapinduzi haya, siyo kwa kufanya kazi kwa bidii pekee, bali kuoanisha kazi zetu na Utu.  Hapo ndipo tutasonga mbele kwa mshikamano, tukijenga tabasamu la utu. “Tusherehekee kwa amani na utulivu, huku tukiendelea kuulinda na kuudumisha Muungano wetu,” alisema.

WAZIRI MKUU

Kwa upande wake, Waziri Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba, aliungana na Rais Dk. Samia, kuwatakia Watanzania wote kheri ya kumbukizi ya Siku ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.

Alisema kumbukizi hiyo ni fursa muhimu kwa Taifa, kukumbuka historia na misingi iliyojenga amani na maendeleo ya nchi.

Dk. Miwgulu, alisisitiza umuhimu wa kuendelea kuimarisha uzalendo, umoja, mshikamano na utulivu miongoni mwa wananchi.

Alieleza kuwa, tunu hizo, zimekuwa msingi imara wa amani na maendeleo ya taifa, ndiyo nguzo ya kudumisha mshikamano wa kitaifa.

Aliwahimiza Watanzania kuyaenzi Mapinduzi hayo siyo kwa kufanya kazi kwa bidii pekee, isipokuwa kuoanisha kazi zao na utu, kwani kufanya hivyo taifa litaendelea kusonga mbele kwa mshikamano, huku likijenga jamii yenye tabasamu la utu.

“Ninaungana na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Samia Suluhu Hassan, kuwataki Watanzania wote kheri ya kumbukizi ya Siku ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.

“Tuendelee kuimarisha Uzalendo, Umoja, Mshikamano na Utulivu ambavyo vimekuwa msingi imara wa Amani na Maendeleo ya Taifa Letu.

“Tuyakumbuke na kuyaenzi Mapinduzi haya, siyo kwa kufanya kazi kwa bidii pekee, bali kuoanisha kazi zetu na utu.

“Hapo ndipo tutasonga mbele kwa mshikamano, tukijenga tabasamu la utu,” alisema.

Previous Post

YANGA, AZAM FC FAINALI YA KIBABE

Next Post

MASHINA NI MOYO WA CCM – DK. ASHA-ROSE MIGIRO

Next Post
MASHINA NI MOYO WA CCM – DK. ASHA-ROSE MIGIRO

MASHINA NI MOYO WA CCM – DK. ASHA-ROSE MIGIRO

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

MAELFU WAMSUBIRI DK. SAMIA MWANZA

MAELFU WAMSUBIRI DK. SAMIA MWANZA

7 months ago
NDOTO YATIMIA

NDOTO YATIMIA

4 months ago

Popular News

  • TANZANIA YAJINADI KIMATAIFA MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

    TANZANIA YAJINADI KIMATAIFA MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • VYALENGA KUIJENGA JAMII KIUCHUMI NA KIROHO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • KUVUMILIANA MUHIMU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WAZIRI SANGU ABAINISHA HIFADHI SKIMU INAVYOENDA KUBADILI MAISHA YA WATANZANIA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TUCTA: WAAJILI WATEKELEZE NYONGEZA YA KIMA CHA MISHAHARA SEKTA BINAFSI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?