• ePaper
Thursday, April 23, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Burudani

TAJI LAONGEZA MZUKA YANGA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
January 15, 2026
in Burudani, Michezo
0
TAJI LAONGEZA MZUKA YANGA
0
SHARES
3
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na NASRA KITANA

SIKU moja baada ya kutwaa Kombe la Mapinduzi 2026, Kocha wa Yanga, Pedro Goncalves, amefurahia kiwango cha timu yake na anaamini michuano hiyo itakuwa chachu ya kuendelea kutikisa Ligi Kuu Tanzania Bara na michuano mingine.

Yanga ilibeba taji la Mapinduzi juzi baada ya kushinda kwa mikwaju ya penalti 5-4 baada ya dakika 120 kumalizika kwa suluhu katika fainali iliyopigwa Uwanja wa Gombani, Pemba.

Baada ya michuano hiyo, sasa Yanga itajipanga kwa mechi za Ligi Kuu Bara na Ligi ya Mabingwa Afrika (CAFCL) zinazotarajiwa kuchezwa hivi karibuni.

Akizungumza kutoka Pemba, Pedro raia wa Ureno, alisema michuano hiyo ilikuwa na ushindani mkubwa na itakuwa chachu ya kikosi chake kuwa imara zaidi msimu huu.

Alisema fainali ilikuwa bora kutokana na wapinzani wake kuonyesha ushindani wa hali ya juu, itawasaidia kufanya vizuri katika mechi zake za kimataifa.

Pedro alisema bado ana kazi ya kufanya hasa katika eneo ya ushambuliaji wachezaji wake watumie vyema nafasi wanazozipata.

“Tumechukua ubingwa wa Mapinduzi ni jambo zuri kwetu kwani ndiyo malengo tuliyojiwekea katika kombe hili, lakini pia (michuano hii) imetupa fursa ya maandalizi mazuri hasa katika mechi zetu zijazo,” alisema.

Kocha huyo alisema atakwenda kurekebisha mapungufu yaliyojitokeza katika mchezo huo kufanya vizuri na kushinda kwa magoli mengi katika michezo ijayo.

Naye beki wa timu hiyo, Dikson Job alisema mechi hiyo ilikuwa ngumu lakini anafurahi kuona wakitimiza lengo la kubeba taji.

“Mwisho wa mashindano haya ndiyo mwanzo wa mashindano mengine, hivyo tunajipanga kupambana na kufikia malengo ya timu,” alisema.

Katika Ligi ya Mabingwa Afrika, Yanga ipo kundi B na timu za Al Ahly ya Misri, AS Far ya Morocco na JS Kabylie ya Algeria.

Yanga wiki ijayo itachuana na Al Ahly nchini Misri kabla ya Januari 30 kurudiana katika Uwanja wa New Amaan Complex, Zanzibar.

Previous Post

MANNY PACQUIAO KUTUA BONGO NA MAMBO MAWILI

Next Post

MAKONDA WEMBE ULE ULE AFCON

Next Post
MAKONDA WEMBE ULE ULE AFCON

MAKONDA WEMBE ULE ULE AFCON

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

EDNA LEMA AWAITA MASHABIKI KMC

EDNA LEMA AWAITA MASHABIKI KMC

4 months ago
COMORO YAENDELEA KUDUMISHA USHIRIKIANO NA TANZANIA KATIKA SEKTA YA AFYA

COMORO YAENDELEA KUDUMISHA USHIRIKIANO NA TANZANIA KATIKA SEKTA YA AFYA

6 months ago

Popular News

  • MSD YABAINISHA DHAMIRA KUIMARISHA USHIRIKIANO NA SEKTA YA AFYA BINAFSI

    MSD YABAINISHA DHAMIRA KUIMARISHA USHIRIKIANO NA SEKTA YA AFYA BINAFSI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • NDEJEMBI ATAJA VIPAUMBELE 10 SEKTA YA NISHATI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MWIGULU ATOA MAAGIZO ALAT

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RIPOTI YA KUPONYA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MWANDAAJI MISS WORLDTZ AITAJA AMANI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?