• ePaper
Thursday, April 23, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Burudani

MAKONDA WEMBE ULE ULE AFCON

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
January 15, 2026
in Burudani, Michezo
0
MAKONDA WEMBE ULE ULE AFCON
0
SHARES
4
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na MWANDISHI WETU

WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda, amesisitiza maandalizi ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2027 kuanza mara moja.

Makonda ametoa kauli hiyo ikiwa bado michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2025 inaendelea nchini Morocco, ambapo fainali inatarajiwa kupigwa Jumapili hii.

AFCON 2027 itafanyika katika nchi za Tanzania, Kenya na Uganda.

Akizungumza jijini Dodoma, Makonda alisema ni muhimu kuanzishwa kwa mashindano ya michezo katika shule zote za msingi na sekondari nchini kama sehemu ya shamrashamra za mashindano ya AFCON 2027.

Alisema mashindano ya shamra shamra za AFCON, yataongeza hamasa na morali kwa Watanzania kuipenda na kuishangilia timu ya Taifa ‘Taifa Stars’, huku yakichochea matokeo chanya na kuibua vipaji vipya vya michezo miongoni mwa vijana.

“Mashindano ya shule hizo yataongeza hamasa na morali kwa Watanzania kuipenda na kuishangilia ‘Taifa Stars’,” alisema.

Pia, Makonda aliitaka wizara hiyo kuandaa programu maalumu itakayowawezesha walimu wa shule za msingi na sekondari wenye mapenzi na michezo, kupata mafunzo ya kitaalamu, ili wahitimu vyuoni wakiwa na uwezo wa kugundua, kukuza na kuongoza vipaji vya watoto katika sekta ya michezo.

Wakati huo huo, Makonda alisema kuelekea katika mwezi mtukufu wa Ramadhani unaotarajiwa kuanza mwezi ujao, atahakikisha michuano ya Ramadhani Cup inafanyika katika mikoa mitano.

“Tunakwenda katika mwezi wa Ramadhani, kwa miaka mingi Dar es Salaam kunakuwa na Ramadhani Cup, hivyo nimeshaongea na viongozi wa mashindano hayo kuhakikisha michuano hiyo hivi sasa itapelekwa katika mikoa mitano,” alisema Makonda.

Waziri huyo alisema watahakikisha wanatumia fursa hiyo michezo iwaunganishe watu kwa pamoja na kuleta maendeleo nchini.

Katika AFCON 2025, Taifa Stars iliishia hatua ya 16 bora baada ya kufungwa bao 1-0 dhidi ya mwenyeji Morocco.

Previous Post

TAJI LAONGEZA MZUKA YANGA

Next Post

MEJA KUNTA AGEUKIA WASANII CHIPUKIZI

Next Post
MEJA KUNTA AGEUKIA WASANII CHIPUKIZI

MEJA KUNTA AGEUKIA WASANII CHIPUKIZI

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

KIHONGOSI ATOBOA SIRI UIMARA WA CCM

KIHONGOSI ATOBOA SIRI UIMARA WA CCM

3 months ago
TANZANIA ITAKAVYONUFAIKA KIUCHUMI, MKUTANO WA IPU

TANZANIA ITAKAVYONUFAIKA KIUCHUMI, MKUTANO WA IPU

1 month ago

Popular News

  • NDEJEMBI ATAJA VIPAUMBELE 10 SEKTA YA NISHATI

    NDEJEMBI ATAJA VIPAUMBELE 10 SEKTA YA NISHATI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MWIGULU ATOA MAAGIZO ALAT

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RIPOTI YA KUPONYA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MWANDAAJI MISS WORLDTZ AITAJA AMANI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SIMBA, MAFUNZO HAPATOSHI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?