• ePaper
Tuesday, April 21, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

TANZANIA YAINGIA 10 BORA KUVUTIA UWEKEZAJI AFRIKA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
January 18, 2026
in Habari, Kitaifa
0
TANZANIA YAINGIA 10 BORA KUVUTIA UWEKEZAJI AFRIKA
0
SHARES
5
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na ATHNATH MKIRAMWENI

TANZANIA imeingia katika orodha ya nchi 10 bora zinazovutia zaidi kwa uwekezaji barani Afrika, ikishika nafasi ya tisa, yakiwa matokeo ya mageuzi makubwa ya kisera yaliyofanywa na serikali chini ya Rais Dk. Samia Suluhu Hassan.

Kauli hiyo ilitolewa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, Profesa Kitila Mkumbo, katika  mkutano na wawekezaji wa kimkakati, jijini Dar es Salaam, jana.

TAKWIMU

Kupitia mkutano huo ulioratibiwa na Mamlaka ya Uwekezaji na Maeneo Maalumu ya Kiuchumi (TISEZA), waziri huyo alitoa takwimu zinazoonesha kukua kwa kiwango cha uwekezaji nchini na kusema mwaka 2021 nchi ilisajili jumla ya miradi 256 pekee, wakati mwaka 2025 idadi ilipanda hadi kufikia miradi 915.

Profesa Mkumbo alisema thamani ya uwekezaji imepanda kutoka chini ya dola za Marekani bilioni tatu mwaka 2021, hadi dola bilioni 11 mwaka jana.

WAZAWA

Katika hatua nyingine, Waziri Mkumbo aliwataka Watanzania kuacha tabia ya ‘kukodisha majina yao’ kwa wawekezaji wa kigeni kwa malipo madogo kufanikisha uwekezaji. 

Alisema kitendo hicho kinadhoofisha azma ya serikali ya kuhakikisha wazawa wanamiliki uchumi wa nchi yao.

Profesa Mkumbo alifichua mbinu inayotumiwa na baadhi ya wawekezaji wageni kukwepa sheria zinazowataka kushirikiana na wazawa na kusema, baadhi ya Watanzania wamekuwa wakikubali kuandikwa kama wamiliki wa hisa

kwa mfano wa asilimia 30 kwa kupewa kiasi kidogo cha fedha, wakati kiuhalisia hawana uamuzi wala umiliki wowote.

Profesa Mkumbo alibainisha kuwa, wazawa wengi wanashindwa kukua kibiashara kwa sababu hawajui fursa na vivutio vinavyotolewa na serikali, tofauti na wawekezaji wa kigeni ambao hufanya utafiti kabla ya kuingia nchini.

Kutokana na hali hiyo, Profesa Mkumbo aliiagiza TISEZA kuzunguka nchi nzima kutoa elimu kwa wazawa kuhusu fursa, mazingira ya biashara, na vivutio vinavyopatikana kuwajengea ujasiri wa kuwekeza na kutengeneza ajira.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa TISEZA, Gilead Teri alisema mamlaka hiyo imejiwekea lengo la kuvutia na kusajili miradi isiyopungua 1,500 katika kipindi kijacho.

Meneja wa Mawasiliano na Uhusiano wa Kampuni ya Sukari ya Kilombero, Victor Byemelwa aliipongeza serikali kupitia TISEZA kwa kuendelea kushughulikia changamoto za wawekezaji na kuboresha mazingira ya biashara nchini.

Previous Post

DK. SAMIA AMREJESHA MAKONDA AFCON

Next Post

SAFARI KUMALIZA CHANGAMOTO UMEME IRINGA, DODOMA YAIVA

Next Post
SAFARI KUMALIZA CHANGAMOTO UMEME IRINGA, DODOMA YAIVA

SAFARI KUMALIZA CHANGAMOTO UMEME IRINGA, DODOMA YAIVA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

DK. NCHIMBI : SIKU 100 TUME YA MARIDHIANO ITAANZISHWA

DK. NCHIMBI : SIKU 100 TUME YA MARIDHIANO ITAANZISHWA

8 months ago
WATANZANIA 37,647,235 KUPIGA KURA LEO

WATANZANIA 37,647,235 KUPIGA KURA LEO

6 months ago

Popular News

  • MAAJABU YA DP WORLD SIKU 730 BANDARINI DAR

    MAAJABU YA DP WORLD SIKU 730 BANDARINI DAR

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MUDATHIR KUIKOSA SIMBA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • ‘MISS WORLD’ KUIPAISHA TANZANIA DUNIANI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • BIL. 195.66/- KUJENGA BONDE MTO MSIMBAZI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • ULEGA AJIBU MAPIGO KUHUSU MTANDAO WA BARABARA NCHINI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?