• ePaper
Friday, May 8, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Burudani

SADIO MANE, SHUJAA WA SENEGAL AFCON 2025

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
January 20, 2026
in Burudani, MAKALA BURUDANI, MAKALA MICHEZO, Michezo
0
SADIO MANE, SHUJAA WA SENEGAL AFCON 2025
0
SHARES
3
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

RABAT, Morocco

NYOTA Sadio Mane juzi aligeuka kuwa shujaa wa Senegal baada ya kuwaongoza Simba hao wa Teranga, kutwaa Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2025.

Mane aliiongoza miamba hiyo juzi katika mchezo wa fainali uliopigwa Uwanja wa Prince Moulay Abdellah jijini Rabat, Morocco wakati Senegal ikishinda 1-0.

Licha ya bao la ushindi kufungwa na kiungo Pape Gueye, lakini kitendo cha Mane kuwaongoza wenzake kumaliza mchezo huo ni sababu tosha ya kuwa shujaa wa kweli wa miamba hiyo.

Mane alionyesha ukongwe, nidhamu na ustaarabu wake katika dakika za nyongeza kipindi cha pili wakati nyota wenzake walipogomea mechi na wengine kurejea vyumbani kufuatia kupinga uamuzi wa refa Jean-Jacques Ndala wa kuizawadia penalti Morocco.

Morocco ilipata penalti hiyo kufuatia staa wake, Brahim Diaz kuanguka baada ya kuvutwa na beki Malick Diouf ndani ya eneo la hatari wakati wa kona, ambapo Senegal walipinga kwa kudai haikupaswa kuwa penalti.

Baada ya dakika kadhaa za kubishana huku nyota wa Senegal wakiongozwa na kocha Pape Thiaw kugoma kuendelea na mchezo, Mane aliwaamuru wenzake warejee uwanjani hatua ambayo iliwafanya kumtii na kuiruhusu Morocco kupiga penalti.

Hata hivyo, Morocco ilikosa mkwaju huo kufuatia kipa Edouard Mendy penalti ya Diaz aliyepiga katikati mwa goli kipa huyo.

Baada ya mechi hiyo kwenda katika dakika 30 za nyongeza, Gueye aliiandikia bao Senegal dakika ya 94, akiweka mpira kimiani kwa shuti kali na kuipa ubingwa wa pili Senegal baada ya mwaka 2021 kufanya hivyo kwa mara ya kwanza.

Mane alisema michuano ya mwaka huu ndiyo itakuwa AFCON yake ya mwisho kukipiga Senegal.

“Mpira wa miguu ni kitu fulani cha kipekee sana, dunia ilikuwa inatazama, dunia inaupenda mpira na nafikiri mpira ni starehe hivyo tunapaswa kuonyesha taswira nzuri juu ya mpira.

Nafikiri kingekuwa kitendo cha ajabu kama tusingecheza hii mechi kwa sababu mwamuzi ametoa penalti. Nafikiri hiko kingekuwa kitendo cha ajabu sana hususan katika mpira wa Afrika, ni bora ningepoteza mechi kuliko kitendo kama hicho kitokee katika mpira wetu,” alisema Mane.

Mchezaji wa zamani wa Nigeria, Daniel Amokachi aliiambia BBC: “Mane alikwenda mbali zaidi kuirudisha timu mchezoni na imemlipa,”.

Mchezaji wa zamani wa Morocco, Hassan Kachloul alisema “Mpira wa Afrika na mpira wa dunia ulikuwa unapoteza hadi pale Mane alipoingilia. Kitu ambacho nilipenda zaidi ni kwamba, mchezaji pekeee kutoka Senegal (aliyewarudisha wenzie uwanjani) alikuwa Sadio Mane. Hii inaonyesha ubora wa mtu huyu,”.

MANE MCHEZAJI BORA AFCON

Baada ya mchezo huo, Mane alitangazwa kuwa mchezaji bora wa mashindano hayo makubwa ya soka barani Afrika.

Katika michuano hiyo, Mane anayekipiga klabu ya Al Nassr ya Saudi Arabia, ameifungia Senegal mabao mawili na kutoa pasi tatu za mabao katika mechi saba za kombe hilo msimu huu.

DIAZ, BONO

Pia, mshambuliaji wa Morocco, Diaz alitangazwa kuwa mfungaji bora wa mashindano hayo baada ya kufunga mabao matano katika mechi saba.

Aidha, kipa wa Morocco, Yassine Bounou ameshinda tuzo ya kipa bora wa mashindano hayo baada ya kuonyesha kiwango bora kuanzia mechi ya kwanza hadi fainali.

CAF YALAANI

Shirikisho la Soka Afrika (CAF), limelaani vitendo visivyo vya kiungwana vilivyoonyeshwa na baadhi ya wachezaji na viongozi katika fainali hiyo.

“CAF inapitia upya vipande vyote vya picha mjongeo na itapeleka suala hilo katika bodi zake kuhakikisha uamuzi sahihi unachokuliwa kwa watakaokutwa na hatia,” ilisema taarifa ya CAF.

KOCHA SENEGAL AOMBA RADHI

Kocha wa Senegal, Thiaw, ameomba radhi kwa kitendo cha kuwaamuru wachezaji wake kugomea kuendelea na mechi wakati Morocco ilipozawadiwa penalti.

Kitendo hicho kilisababisha mechi hiyo kutoendelea kwa zaidi ya dakika 17.

“Hatukubali (uamuzi wa refa). Ninaomba radhi kwa ajili ya mpira wa miguu. Hatukupaswa kufanya vile lakini tulishafanya na sasa tunaomba radhi,” alisema Thiaw, 44 alipozungumza na BeIN Sport.

Previous Post

BARKER ALIA NA NAFASI SIMBA

Next Post

RAIS DK. SAMIA ATAJA SIFA ZA MZEE MTEI

Next Post
RAIS DK. SAMIA ATAJA SIFA ZA MZEE MTEI

RAIS DK. SAMIA ATAJA SIFA ZA MZEE MTEI

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

VIJANA MSIKUBALI KUBEBA AJENDA MSIZOZIJUA

VIJANA MSIKUBALI KUBEBA AJENDA MSIZOZIJUA

2 months ago
MATARAJIO YA WASOMI TUME YA JAJI CHANDE

MATARAJIO YA WASOMI TUME YA JAJI CHANDE

1 month ago

Popular News

  • YANGA MBELE KWA MBELE

    YANGA MBELE KWA MBELE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WATAALAMU WAFUNGUKA MITAZAMO YA MIKATABA 8

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. SAMIA AKEMEA VIONGOZI ‘KUVIMBA’

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DEMOKRASIA ISIZICHAFUE NCHI ZETU – RAIS DK. SAMIA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • ZIARA YA RAIS KAGAME, RUTO KUIMARISHA DIPLOMASIA KIUCHUMI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?