• ePaper
Thursday, April 16, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Burudani

KOCHA YANGA AFUNGUKA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
February 18, 2026
in Burudani, Habari, Kitaifa, Michezo
0
KOCHA YANGA AFUNGUKA
0
SHARES
5
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na NASRA KITANA

KOCHA Mkuu wa Yanga, Pedro Goncalves, amesema anajivunia wachezaji wa kikosi chake, kwa kuendelea kujitoa kwa moyo wote kuipambania timu katika michuano inayowakabili.

Pia, amesema baada ya kuondolewa katika Ligi ya Mabingwa Afrika (CAFCL) hivi sasa wanarejea katika mashindano ya Ligi Kuu na Kombe la Shirikisho (FA) kusaka ushindi.

Hivi karibuni Yanga iliondolewa katika michuano hiyo, baada ya kuifunga mabao 3-0 JS Kablye katika mchezo wa hatua ya makundi uliochezwa Uwanja wa New Amaan Complex, Zanzibar.

Mabingwa hao watetezi wa Ligi Kuu, leo watashuka dimbani kukabiliana na Cosmopolitian FC, katika mechi ya mzunguuko wa pili Kombe la FA (Shirikisho) itakayopigwa Uwanja wa KMC, Dar es Salaam saa 1:00 usiku.

Akizungumza jijini Dar es Salaam, Pedro alisema kila mchezaji ndani ya kikosi chake alijitoa vizuri katika michuano ya kimataifa na ligi, hivyo ana matumaini ya kufanya vizuri zaidi.

 “Tumetolewa katika michuano ya ligi ya mabingwa Afrika, nguvu zetu zote tunazielekeza katika michuano ya ligi kuu na FA,” alisema.

Pedro aliahidi kuwa, timu hiyo haitakuwa tayari kupoteza mchezo kwa kuwa wamejipanga kupambana mwanzo mwisho kushinda, kufikia malengo waliojiwekea.

Kocha huyo aliwaomba mashabiki na wapenzi wa timu yao kuendelea kuiunga mkono timu yao ifanye vizuri.

Naye, mchezaji wa timu hiyo, Dikson Job alisema kwa upande wao wamejipanga kupata matokeo mazuri na kufikia malengo.

“Tumetolewa ligi ya mabingwa Afrika, lakini hatujakata tamaa, tutapambana kuhakikisha tunashinda kila mchezo wetu tuwe mabingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara na michuano ya FA, msimu ujao tutashiriki tena michuano ya kimataifa,” alisema Job.

Previous Post

MKATABA WA GAMONDI WAWAIBUA MKWASA, PAWASA 

Next Post

TAKUKURU YAFUNGUA MASHAURI MATATU YA UHUJUMU UCHUMI SIHA

Next Post
TAKUKURU YAFUNGUA MASHAURI MATATU YA UHUJUMU UCHUMI SIHA

TAKUKURU YAFUNGUA MASHAURI MATATU YA UHUJUMU UCHUMI SIHA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

GAMONDI AITA JESHI LA MAANGAMIZI, MANULA NDANI

GAMONDI AITA JESHI LA MAANGAMIZI, MANULA NDANI

4 weeks ago
TANZANIA ITAKAVYONUFAIKA KIUCHUMI, MKUTANO WA IPU

TANZANIA ITAKAVYONUFAIKA KIUCHUMI, MKUTANO WA IPU

4 weeks ago

Popular News

  • PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SERIKALI YAFUTA LESENI 40 ZA UTAFITI  WA MADINI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TIMU OFISI YA MAKAMU WA RAIS, WIZARA YA MAJI KUCHUANA MEI MOSI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SIMBA, FOUNTAIN GATE SIKU YA HESHIMA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. MWINYI AKAGUA MJI WA AFCON FUMBA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?