Na ATHNATH MKIRAMWENI, Urambo
KATIBU wa NEC, Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa Chama Cha Mapindizi (CCM), Kenani Kihongosi, amesema Chama kitaendelea kuongoza kwa kuwa kinasimamia misingi ya demokrasia, utu na maendeleo.
Kauli hiyo aliitoa wakati akihitimisha ziara yake katika Wilaya ya Urambo, mkoani Tabora na kusema CCM ndiyo Chama cha kuwaletea maendeleo Watanzania.
“Kuna baadhi ya watu wanasema Chama Cha Mapinduzi hakijafanya kitu si kweli, ukizungumzia umeme, maji, lami huwezi kusema bila kuitaja CCM,”alisema Kihongosi.
Aidha, alisema serikali imetumia sh. milioni 686 kujenga Kituo cha Afya cha Nsenda, kusogeza huduma karibu kwa wanachi 18,998 wa vijiji vitano vya Kata ya Nsenda.
Alieleza CCM imeendelea kusimamia serikali katika utekelezaji wa Ilani yake hasa katika siku 100 za Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, akiwa madarakani.
Alisema ujenzi wa kituo hicho utakamilika Machi 30, mwaka huu ambapo hivi ujenzi umefikia asilimia 69.
Mradi wa Kituo Cha Afya Nsenda ulipokea sh. 686,135,134 kutoka serikali ukihusisha ujenzi wa jengo la wagonjwa wa nje (OPD), jengo la maabara, jengo la mama na mtoto, jengo la kufulia, vyoo vya nje na kichomea taka.
Ofisa Masuuli Mteule, Faid Chagula, alisema kituo hicho kitawanufaisha wananchi wa kata tano na kitapunguza vifo vya watoto wachanga na wajawazito.
“Kuna baadhi ya watu wanasema Chama Cha Mapinduzi hakijafanya kitu si kweli, ukizungumzia umeme, maji, lami huwezi kusema bila kuitaja CCM”
Kenani Kihongosi




