Na MWANDISHI WETU
TIMU ya taifa ‘Taifa Stars’ inatarajiwa kuchuana katika mashindano maalumu ya kirafiki ya Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) ambayo yanajulikana kama FIFA Series 2026.
Katika michuano hiyo itakayofanyika katika maeneo mbalimbali kuanzia Machi 25 hadi Machi 31, mwaka huu, Tanzania imepangwa katika kundi la Rwanda B ambapo mechi zake zitachezwa Uwanja wa Pele, Kigali nchini Rwanda.
Kundi hilo linaudwa na timu za Tanzania kutoka Bara la Afrika, Macau iliyopo Asia, Aruba kutoka Amerika Kusini na Liechtenstein iliyopo Ulaya.
Kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa na FIFA, Tanzania itakipiga na Liechtenstein wakati Aruba ikicheza na Macau na mshindi wa kila mechi atatinga fainali wakati itakayofungwa itacheza mshindi wa tatu.
Mbali na kundi la Rwanda B ililopo Tanzania, makundi mengine ni Australia, Azerbaijan, New Zealand, Kazakhstan, Rwanda A, Indonesia, Puerto Rico, Uzbekhstan na Rwanda B.




