• ePaper
Thursday, April 30, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Burudani

SINGIDA BS, YANGA SC KAZI IPO LEO

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
March 5, 2026
in Burudani, Habari, Michezo
0
SINGIDA BS, YANGA SC KAZI IPO LEO
0
SHARES
3
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na NASRA KITANA

TIMU za soka za Singida Black Stars na Yanga, leo zinashuka dimbani kuchuana katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara.

Mchezo huo wa 12 kwa timu hizo unatarajiwa kupigwa saa 10:00 jioni katika Uwanja wa Airtel uliopo Singida.

Akizungumzia mchezo huo, Kocha wa Yanga, Pedro Goncalves amesema timu yake ipo vizuri kuwania pointi tatu.

Pedro alisema anajua wachezaji wake wanajua umuhimu wa kucheza kwa kujituma, licha ya mechi kuwa ngumu watahakikisha wanapata ushindi.

“Hakuna jambo muhimu kuliko alama tatu, ili upate alama tatu dhidi ya timu kama Singida unahitaji ufanye kazi ya ziada, kuwa makini dakika zote 90 na kuwa na utimamu wa kimwili ili kukabiliana na kasi ya mchezo, ili tushinde hii mechi lazima tuoneshe njaa ya kutaka alama tatu.

 “Nikiri tunapitia changamoto kadhaa ikiwemo baadhi ya wachezaji muhimu kupata majeraha, kwa bahati mbaya Dickson Job naye ameongezeka katika idadi ya wachezaji ambao wanakabiliwa na majeraha, mtumaini yetu ni kuwa majeraha hayo siyo makubwa sana, unapokosa wachezaji wako muhimu ni wazi lazima kuna kitu kitapungua katika ufanisi wa timu,” alisema Pedro.

Naye mchezaji wa Yanga, Abubakar Nizar Othman ‘Ninju’, alisema Singida ni timu nzuri lakini amekiandaa kikosi chake kupata pointi tatu.

Alisema timu bora siku zote inatengenezwa na mwalimu na wachezaji kuwa na utayari wa kupokea maelekezo na kuyafanyia kazi.

“Mpira wa miguu ni mchezo ambao hubadilika kulingana na mazingira na wapinzani unaokutana nao, Yanga ni timu kubwa ambayo ina wajibu wa kusaka alama tatu lakini pia kutoa burudani kwa mashabiki. Hatuwezi kuwa bora katika kila nyakati, kuna nyakati tutapata alama tatu lakini katika mazingira magumu, katika mchezo huu tutamkabili mpinzani kwa namna atakavyokuja,” alisema Ninju.

Naye Kocha wa Singida BS, Othmen Najjar, alikiri wanakwenda kucheza na timu yenye wachezaji wengi wazuri lakini hawatakubali kupoteza.

 “Kwa mechi kama hii, kisaikolojia kila mmoja hujiandaa vizuri kwa sababu ni mchezo muhimu na wanapaswa kucheza katika kiwango cha juu kabisa, kama tulivyofanya katika michezo mingine.

“Tunaelewa huu utakuwa mchezo mkubwa, kila mmoja husubiri aina hii ya mechi dhidi ya timu kubwa kama Yanga, ambao ni vinara wa ligi na wameshinda mataji mengi katika misimu iliyopita,” alisema Najjar.

Naye mchezaji wa timu hiyo, Kennedy Juma, alisema kila mchezaji amejiandaa vizuri kushindana kwa kiwango cha juu na kutumia kila nafasi watakayoipata kuvuna pointi tatu.

“Tunawaomba mashabiki wajitokeze kwa wingi kutushangilia kwa nguvu. Tutawapa burudani. Hizi ni alama tatu muhimu katika uwanja wetu wa nyumbani,” alisema.

Katika msimamo wa Ligi Kuu Bara, Yanga inashika nafasi ya kwanza ikiwa na pointi 29 huku Singida Black Stars ikishika nafasi ya tisa na kujizolea pointi 19 baada ya wote kushuka dimbani mara 11.

Previous Post

VIJANA MSIKUBALI KUBEBA AJENDA MSIZOZIJUA

Next Post

MAKATIBU WAKUU VYAMA VYA UKOMBOZI WAJADILI HALI YA KISIASA KUSINI MWA AFRIKA

Next Post
MAKATIBU WAKUU VYAMA VYA UKOMBOZI WAJADILI HALI YA KISIASA KUSINI MWA AFRIKA

MAKATIBU WAKUU VYAMA VYA UKOMBOZI WAJADILI HALI YA KISIASA KUSINI MWA AFRIKA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

PAPA LEO XIV APOKEA UJUMBE WA RAIS DK. SAMIA

PAPA LEO XIV APOKEA UJUMBE WA RAIS DK. SAMIA

3 months ago
KIBADENI, MANARA, MAYAY WAFUNGUKA MANUFAA YA AMANI

KIBADENI, MANARA, MAYAY WAFUNGUKA MANUFAA YA AMANI

4 months ago

Popular News

  • TANZANIA YAJINADI KIMATAIFA MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

    TANZANIA YAJINADI KIMATAIFA MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • VYALENGA KUIJENGA JAMII KIUCHUMI NA KIROHO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • KUVUMILIANA MUHIMU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WAZIRI SANGU ABAINISHA HIFADHI SKIMU INAVYOENDA KUBADILI MAISHA YA WATANZANIA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TUCTA: WAAJILI WATEKELEZE NYONGEZA YA KIMA CHA MISHAHARA SEKTA BINAFSI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?