• ePaper
Sunday, May 31, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Burudani

SERIKALI KUWABEBA WASANII, WANAHABARI

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
March 13, 2026
in Burudani, Habari, Kitaifa
0
SERIKALI KUWABEBA WASANII, WANAHABARI
0
SHARES
7
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na NASRA KITANA

SERIKALI kupitia Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo imetangaza kuwepo kwa fedha sh. bilioni 50 kwa ajili ya kuwawezesha vijana wanaojihusisha na sekta ya ubunifu nchini.

Fedha hizo pia zimetengwa kwa ajili ya watengeneza maudhui mtandaoni (content creators), wasanii, wanamuziki, waigizaji, waandishi wa habari, watu wenye ushawishi mitandaoni na wabunifu wa kazi mbalimbali za sanaa.

Akizungumza jijini Arusha, Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda alisema kuwa  mfuko huo ni utekelezaji wa maelekezo ya Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, yenye lengo la kuwawezesha vijana kiuchumi kupitia sekta ya habari, sanaa na ubunifu.

“Awali Wizara ilikuwa imepangiwa kupewa sh. bilioni 20, lakini baada ya mazungumzo na Benki ya CRDB, kiwango hicho kimeongezwa na kufikia sh. bilioni 50 ili kupanua wigo wa vijana watakaonufaika na mfuko huo,” alisema Makonda.

Waziri Makonda alisema kuwa mfuko huo ni kwa ajili ya kuwainua vijana kutoka katika sehemu moja kwenda nyingine ili kuweza kunyanyuka kiuchumi na kurejesha tabasamu kwa Watanzania.

Alisema kuwa kwa hivi sasa kinachosubiriwa ni tarehe rasmi ya uzinduzi wa mfuko huo, ambapo baada ya uzinduzi fedha hizo zitaanza kutolewa kwa vijana waliopo katika sekta ya habari, sanaa na ubunifu ili kuwawezesha kukuza kazi zao na kuchochea maendeleo ya uchumi wa taifa.

Makonda alisema kuwa Wizara inapanga kuzindua rasmi mfuko huo katika hafla maalumu inayotarajiwa kufanyika hivi karibuni, ambapo Rais Dk. Samia, anatarajiwa kuwa mgeni.

Hatua hiyo inaelezwa kuwa ni sehemu ya jitihada za serikali kuhakikisha vijana wanapata fursa za kiuchumi na kutumia vipaji vyao kama chachu ya maendeleo ya Tanzania.

Previous Post

SIMBA MZUKA UMEPANDA

Next Post

IBENGE FURAHA TELE

Next Post
IBENGE FURAHA TELE

IBENGE FURAHA TELE

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

DK. MWINYI ACHUKUA FOMU ZANZIBAR, AHADHARISHA CHUKI

DK. MWINYI ACHUKUA FOMU ZANZIBAR, AHADHARISHA CHUKI

9 months ago
RAIS DK. SAMIA APOKEA TUZO TELE ZA UTALII

RAIS DK. SAMIA APOKEA TUZO TELE ZA UTALII

5 months ago

Popular News

  • SERENGETI BOYS KILA KONA, RAIS SAMIA AWAPA MILIONI 500/-

    SERENGETI BOYS KILA KONA, RAIS SAMIA AWAPA MILIONI 500/-

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAS: UTUNZAJI MAZINGIRA AJENDA YA KIPAUMBELE KWA MKOA WA MWANZA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • UPELE UMEPATA MKUNAJI STARS

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • ‎ RAIS DK. SAMIA: POLISI MSIDHARAU TAARIFA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. MWIGULU ATETA NA WAZIRI MKUU WA CONGO BRAZZAVILLE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?